MAOMBI NI CHANZO CHA MAFANIKIO YA WATU WA MUNGU



Maombi ni neno ambalo limetumika sana katika Biblia. Mara nyingi maombi yanafanyika makanisani, kwenye mikutano mbalimbali ya injili, katika vikundi mbalimbali, na  hata kwa mtu binafsi. Maombi yana umuhimu mkubwa sana katika huduma. Na yakipata nafasi mafanikio makubwa yanakuwepo. Maombi ya mtu binafsi nayo pia ni muhimu sana. Mimi mwenyewe nimeona maombi yakifanya mambo mengi makubwa sana katika maisha yangu.
 
Yote ambayo Mungu ameyafanya na anaendelea kuyafanya katika maisha yangu hata sasa yamenifanya mimi binafsi kusikia msukumo mkubwa na wa kipekee sana moyoni mwangu wa kutaka kujua zaidi na zaidi kuhusu maombi. Hili ni jambo kubwa sana na linatufaa sisi sote ambalo Mungu mwenyewe ameliweka ili tupate nafasi ya kuwasiliana naye. Mungu ameiweka njia hii ya maombi ili apate kutusikiliza wakati tunapozungumza naye.

Kwa hiyo kuomba ni  njia pekee ya kutuunganisha na Mungu.
Yeye anayemtafuta Mungu wa kweli inampasa  aanze uhusiano naye kwa njia ya maombi na kwa  njia hii ya kuomba uhusiano wetu  na Mungu unaanzishwa na kutunzwa.
 
Ni lazima tunyenyekee na kutii na kuonyesha heshima mbele za Mungu wetu kwa kumshukuru na kumtukuza kwa ajili ya uweza wake na nguvu zake.
Yoh: 15:14 "Ninyi mmekuwa rafiki zangu mkitenda niwaamuruyo." Mungu anatuheshimu sana, tunapoyatenda yale aliyotuagiza. Anatuthamini kiasi cha kutufanya sisi kuwa marafiki zake, hivyo tunaweza kushirikiana naye na kuongea naye wakati wowote. Yeye kama rafiki yetu anapenda sisi tuwe na furaha, amani na maisha ya ushindi. Mungu anapenda sisi tuwe karibu naye kila wakati. Yak 4:8 "Mkaribieni Mungu naye atawakaribia ninyi.".MUNGU awabariki sana na tusonge mbele na wokovu maana MUNGU wetu anajibu maombi. na katika maombi yako siku zote tumia mamlaka ya jina la YESU KRISTO kuharibu hila zote za shetani maishani mwako.

Comments