SIMBA WALILIZUNGUKA KANISA LETU TUKIWA NDANI KWENYE MAOMBI


Naitwa Agnes Philipo naishi Buyu, Zanzibar nina miaka 13 napenda kushuhudia tukio moja ambalo lilitokea tarehe 15 April 2012 tukiwa kwenye maombi ya usiku kanisani kwetu PAG  Chukwani, Zanzibar tulianza maombi kama kawaida saa 3 usiku na tukiwa tunaomba kama kawaida watu wakinena kwa lugha na wengine wakiomba tu kawaida niliona simba mmoja nje ya kanisa na baada ya muda mfupi waliongezeka na kuwa wengi.Niliogopa sana na kumwambia mchungaji kwamba kuna simba kwa nje, Mchungaji akasema kwamba maeneo hayo ya zanzibar hakuna simba hivyo simba hao ni sio simba wa kawaida ila nguvu za giza na kama MUNGU akikuonyesha kitu basi hata jibu lake analo ila tu anakutaka wewe utumie mamlaka ya YESU KRISTO ndani yako kuharibu na kuteketeza nguvu zote za giza, Tukaanza kuomba wanamaombi wote kwa juhudi na na tukiwa tunaomba wale simba waligeuka na kuwa kama majitu ambayo siyafahamu yakiwa na vichwa 3 kila moja. Niliogopa zaidi na kuwaambia wenzangu ambao wao hawakuona ila mmoja wao tu ndie alikua anaona kama mimi hivyo watu wawili tu kati ya kundi la watu 22 tuliokuwa tunaona mambo hayo na tulipozidi kuomba zaidi wale majitu walirudi na kuwa simba huku wakilia kama watu na muda ambapo maombi ya mamlaka yalipozidi walianza kuungua mmoja mmoja na  wakaanza kukimbia na wakati huohuo wakianza kukimbia nilijikuta natamka kwamba ''NAWAFUNGA KWA JINA LA YESU KRISTO'' na kweli hapohapo wakawa kama wameshikwa na kitu. tukaanza kuomba huku wakipiga kelele na baada kama ya dakika 5 walianza kuteketea kabisa hadi wakafa na kubaki majivu.Siku hiyo ndipo niliona nguvu ya maombi maana kwa jinsi wanamaombi walivyokuwa wanataja jina la YESU ndipo moto ulivyoongezeka sana na tangu siku hiyo nikiomba kitu huwa natumia sana kutaja jina la YESU maana siku hiyo niliona nguvu kubwa kupitia jina hilo.MUNGU awabariki sana hakika kwa YESU KRISTO ni raha sana ukiomba kwa imani na mamlaka.
AGNES PHILIPO

Comments