KUVUNJA MADHABAHU

  • SEMINA NDANI YA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA,MOSHI.
     
    . By: Mchungaji Mwandamizi Mwangasa

    SOMO: KUVUNJA MADHABAHU

    Madhabahu ni nini?

    Madhabahu ni daraja toka duniani kwenda mbinguni.

    Kuna aina mbili za madhabahu

    1. Madhabahu ya Mungu wa Mbinguni

    2. Madhabahu ya shetani(sehemu inayowaunganisha wachawi na shetani)
    Amu 6;25-28.
    25 “Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Mtwae ng'ombe wa baba yako, yaani ng'ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo;
    26 ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata.
    27 Ndipo Gideoni akatwaa watu kumi miongoni mwa watumishi wake, akafanya kama Bwana alivyomwambia; lakini ikawa kwa sababu aliwaogopa watu wa nyumba ya baba yake, na watu wa mji, hakuweza kuyatenda hayo wakati wa mchana, basi aliyatenda usiku.
    28 Hata watu wa mji walipoondoka asubuhi na mapema, tazama, madhabahu ya Baali imebomolewa, na ile Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na yule ng'ombe wa pili ametolewa sadaka juu ya ile madhabahu iliyojengwa”.

    Gideoni aliagizwa na Mungu akaibomoe madhabahu ya mungu Baali maana kwa wakati ule walikuwa wanamwabudu mungu Baali na kumtolea kafara kama vile ya damu.Kwa kufanya hivyo walikuwa wanapata nguvu kinyume na nguvu za Mungu wa Mbinguni.

    Roho inayomtawala mchawi na kumfanya aende kwenye madhabahu ya shetani ni wivu.Kazi yao katika ulimwengu wa roho ni kujadili jinsi ya kutenda ili kufikia kusudi la kumfunga mtu.Mfano mtoto anapelekwa kwenye makaburi na kufanyiwa zindiko kwa mizimu ya mikoo,na kwa kufanya hivyo matokeo yake ni kuandaa matatizo kama magonjwa yatakayoutesa ukoo mzima mfano ukoo Fulani mabinti wote huwa hawaolewi,tambua ya kuwa kuna madhabahu ilyojengwa kulinda ukoo na laana hiyo lakini tambua leo iko madhabahu ya Yesu kristo inayovunja madhabahu ya kishetani.
    Wachawi huwa wanapeleka mashitaka yao kwa shetani lakini leo wewe na mimi tupeleke mashitaka yetu kwa Yesu Kristo ili aivunje madhabahu ya kishetani inayotesa maisha yetu.

    Tambua ya kuwa kila kinachotokea mwilini kimeanzia rohoni.Tambua ya kuwa chanzo cha tatizo ni madhabahu iliyowekwa kwa kila tatizo hivyo anza kubomoa chanzo cha tatizo ambacho ni madhabahu mana Bila kubomoa madhabahu wafu hawawezi kufufuka,magonjwa hayawezi kupona na leo tumezikamata nguzo mbili ambazo ni mauti na kuzimu na ni lazima zibomolewe.
    Tambua ya kuwa wewe ni jeshi la Bwana linakwenda kubatilisha kila mpango wa giza maana yeye ni Bwana wa mbwana na ni mfalme wa wafalme.Ukiamua kusimama kwa uaminifu mbele za Bwana hata mashetani na wachawi wafanyeje hawataweza maana imeandikwa katika Zaburi 34:7 “Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa”.
    Usisubiri mapepo na mapepo na mashetani wakuvamie,anza kuwavamia leo kwa Jina la Yesu,simama kama mwanajeshi wa Bwana anza kukataa aibu,kupuuzwa,magonjwa kwa Jina la Yesu maana vita ya rohoni lazima uamue kuokoka maana wachawi hawamwogopi mtu yeyote ambaye hajaokoka na nuwa Mwanajeshi wa Bwana.

Comments