Na Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima. Ufufuo na Uzima,Tanganyika parkers Kawe |
SOMO: UKOO TATA
MANENO YA MSINGI: Mwanzo 50:24, 1 Nyakati 4:9
Baraka au laana ya ukoo inatokana sana na
shina la ukoo. Ulivyo ukoo wa mtu,ndivyo alivyo mtu kama hana Mungu. Kuna koo
ambazo ni tata sana, hata zikitoa mambo, na mambo hayo nayo huwa ni tata. Mara nyingi vyanzo vingi vya matatizo aliyo
nayo mtu yana uhusiano wa karibu na ukoo alipotokea mtu huyo.
Mwanzo 50:24 “Yusufu akawaambia nduguze, Mimi ninakufa, lakini Mungu atawajia
ninyi bila shaka, atawapandisha toka nchi hii, mpaka nchi aliyowaapia Ibrahimu,
na Isaka, na Yakobo alivyowabariki”. Tunaona jinsi ambavyo Unaweza
kukuta ukoo Fulani kuanzia wa kwanza hadi wa mwisho watoto wote ni tata. Hivyo
kabla hujaoa wala kuolewa chunguza ukoo kama ni tata au sio tata. Watu wengine
wakishafika mjini wanaanza kujisifu na wanasahau kama huko walikotoka mfano shangazi hana hata viatu na bibi anapuliza
kiko cha ugolo hadi sasa!
Kutokana na neon hili unaweza
kuona Yakobo alikuwa na watoto 12, na kabila 12 zilitokana na watoto wale.
Hivyo kila tabia ya mtu inatokana na msingi wa
ukoo wake. Hivyo yatupasa tuchimbe na tung’oe msingi ya koo tata.
Kumbuka niliwahi kufundisha habari ya majeshi ya wafu, nikasema sio vizuri
kabisa kuendekeza na kuwatolea sadaka.
Kitabu cha kwanaza cha maneno matakatifu
kinaanza na majina ya ukoo. Mfano katika kitabu cha 1Nyakati 1. Kutokana na
majina ya koo hizi, inatufindisha kuwa kila majina ya koo yalitengeneza majina
ya sehemu hizo leo. Kila mtu ajue chochote utendacho leo unatengeneza ukoo
wenye baraka au laana ya kizazi kijacho. Usifikirie kuwa unaposoma sana ndio
kushinda katika maisha, lakini elimu inakupa tu mwanga wa kukuangazia utafute
jinsi ya kujikwamua katika maisha yako, ukitumia kipawa alichokupa Mungu.
Unaweza kuona baadhi ya koo
mabinti hawezi kuolewa, au kusoma mpaka chuo kikuu, au wanakufa katika umri
mdogo. Kwa namna hii unaweza kuona kuwa matatizo hayo ndio chanzo na msingi wa
ukoo huo. Hivyo rudia maneno haya “
katika jina la Yesu nayavunja mambo yote mabaya katika ukoo wangu “ Ukoo wa
mtu unatabili maisha ya mtu anayoishi leo. Unaweza kukuta kila kinachotokea
mfano kifo katika ukoo ni cha namna ileile. Mfano kule Bukoba unaweza kukuta
nyumba ya Profesa Fulani , lakini maisha ya familia yake sio sawa na kiwango
cha elimu walionayo. Jambo hilo limetokana na msingi wa ukoo wake. Sema maneno
haya “ Kwa jina la yesu navunja
mahusiano ya taabu yangu na familia yangu katika jina la Yesu”
Leo uhame hapo ulipo kwenye ukoo
wa laana na mikosi uingie kwenye ukoo wa kushinda kaita jina la Yesu. 1 Nyakati 4:9 “Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze; na mamaye akamwita
jina lake Yabesi, akisema, Ni kwa sababu nalimzaa kwa huzuni.”
Huyu mtu alizaliwa kwa huzuni na
akaitwa jina lake ni huzuni, lakini baada hapo alimtafuta Mungu akaishia kuwa
wa furaha na kuheshimiwa na ndugu zake. Walawi
25:47 “Tena kama mgeni au mtu akaaye
nawe akitajirika, na nduguyo amekuwa maskini karibu naye, akajiuza kwa huyo
mgeni, au kwa huyo akaaye kwako, au kwa ukoo wa jamaa ya huyo mgeni”
Na wewe ukiamua kumtii na kumtumikia Mungu
ataona hata utakao wazaa hawataanzia wewe ulikoanzia bali ulikoishia wewe.
Hivyo mtii Mungu na kumuheshimu Mungu utaheshimika na watu wote na viongozi wa
nchi hii watokane na wewe katika jina la Yesu. Kama ukoo wako ni ukoo wa
kushindwa utabaki kuwa wa kushindwa mpaka uhame katika jina la Yesu. Leo nahama
kutoka katika ukoo wa laana, mkosi, kushindwa, kukataliwa, kuachwa, magonjwa,
vifo vya mara kwa mara.
Zamani
mtu alikuwa anaweza kujiuza kutoka kwenye familia ya umaskini na kuingia katika
familia ya kitajiri na anakuwa mali ya familia au ukoo huo na sisi tumeamua
kujiuza kwenye familia ya mwana kondoo.
2 Wakorintho 8:9
Inatwambia kumbe yesu alifanyika
kuwa maskini ili tuwe matajiri. Na yesu ametukubali kwa umaskini wetu sisi
tupate kuwa matajiri kwa njia ya imani. Na kwa namna hiyo tunapata kibali na
kuweza kuendelea mbele. Ndo maana unaweza kuona unaweza kuwa na sifa nzuri za
kupata visa, tenda, kazi lakini usipate. Hili kwa sababu ukoo wako umeandikiwa
muwe wa kukosa. “Leo natangaza kwa jina la yesu lazima uhame katika jina la yesu.”Unaweza kukuta
familia zinatawaliwa na nguvu za giza? Kabla hatujamjua yesu, wazazi wetu walikuwa
wanatumia ulinzi wa kimila. Kuna familia nyingine wewe kabla kuja mjini kuna
kitu ulipewa uje nacho kama ulinzi kwako dhidi ya watu wabaya. Anaweza kuletwa
na baba wa familia au bibi au babu wa ukoo, akiwa na nia njema ya kuwawekea
ulinzi, lakini kumbe ndo chanzo cha nyinyi kuanza kulindwa na mashetani.
Wakati mwingine mambo hayo
yanatengenezwa kama karatasi yenye maandishi ya kutoka kulia kwenda kushoto Fundo
hili linaitwa talasim. Kimsingi kupitia zindiko hili familia inaanza kulindwa
na masheteni. Kwa mfano pia unaweza kukuta mtua ana namba ya waziri mkuu,
mkurugenzi au mtu mkubwa.Lakini pamoja na kuwajua watu hao haikukusaidia kwa
kuwa kuna utata wa kishetani unaolinda familia yenu. Unahitaji kuhama ukoo huo
wa utata. “kwa jina la yesu nakataa kabisa kung’ang’ania ukoo tata”
Wakati mwingine unaanza kujiuliza mbona nimejitahidi kusoma sana lakini
bado mambo
2 Timetheo1:3
“Leo navunja kila laana, balaa namatatizo yaliopandwa ndani ya ukoo
wangu katika jina la Yesu”
Maombolezo 3:30-32
Isaya 53:4
Tumeumba kwa neno hivyo unapaswa kutamka kwa kinywa chako. Na utambue imeandikwa wewe
u rungu langu na silaha za bwana za vita. Mtu yeyote kuanzia sasa naamuru achiwe
katika jina la Yesu. Unaweza kujiuliza maswali ya kwamba mbona kaka zangu wananafuu? Tambua kuwa balaa iliyo
ndani ya famila au ndani ya ukoo inaweza kijidhihirisha kupitia mtu mmoja.
Imeandikwa pi kuwa amelaaniwa mtu Yule amwagaye damu ya mtu asiye na hatia.
Inaweza kutokea ajali inatokea anakufa mtu mmoja au unazaa mtoto anaulemavu wa
ngozi. Lakini kwanini usijiulize kwanini itokee kwako? Kimsingi lazima ujue kuwa kunakitu kinapelekea
au kimepengwa kikupate kama ilivyofanyika katika ulimwengu waroho.
Mfano katika taifa la Marekani
kila raisi aliyekuwa anaingia madarakani alikuwa anauwawa mpaka walipoamua
kuingia ikulu na kuomba na kuvunja laana hiyo na haikutokea tena. Unaweza
kukuta kunatabia Fulani inatawala kabila Fulani, lakini hakuna kabila bora
kuliko nyingine sema tu inategemea kiwango cha kutawaliwa na mashetani hao.
Jiulize pia wakati naomba kwa nini watu wanalipuka mapepo? Hii ni kwasababu mtu
anayelipuka mapepo kimsingi ameshikiliwa na mashetani wasimamizi wa laani maana
wamewekwa kusimamia laana hiyo na kuhakikisha unaangamia na kupotea kabisa.
Lakini kwa wanao mwamini Yesu pia kuna damu ya mwanakondoo imewekwa
ilikusimamia na kuvunja laana ya ukoo huo au inayokufatilia wewe.
Watu wa hospitalini huwa wanasema
tutaweza kuicontrol pressure yako au kisukari lakini sisi tumepewa mamlaka ya
kung’oa kubomoa na kuharibu. “Lakini leo
sema nakataa kusimamiwa na mashetani wa balaa, laana na mikosi na toroka na kuhama
kutoka maeneo ya kishetani katika jina la Yesu.” Kuna namna mbili shetani
anazoweza kutumia kukushambulia.
1.
Anaweza kuwa nje
2.
Anaweza kuwa ndani yako
Zakari3:1
Kuna mtu analalamika anadegree 2,
au 3, lakini hapati kazi.
Pamoja na kushindwa lakini
unaweza kuanza tena, kushinda tena, kutengeneza tena. Tumejifunza kuomba
wenyewe kwa mamlaka ya jina la Yesu.
Unatakiwa ujue kuwa hatumuombi Mungu atende bali twatumia mamlaka ya
Yesu iliyoko ndani mwetu. Hivyo unatakiwa ujue kuomba mwenyewe. Kila mtu anayo mamlaka shida tu huwezi kutumia usichokijua. Uwezo wako wa kuvunja, kushambulia na kuharibu
katika ulimwngu wa roho, ndo uwezo wako wa kushinda katika ulimwengu wa mwili.
Utakuwa kama bwana anavyotaka uwe, wala hautakuwa kama watu wanasema nini juu
yako. Mungu anajua kesho yako kabla haujaiona, na kesho ya maisha yako iko
mikononi mwako. Wanakuita aliyeshindwa lakini mbinguni wanakujua kama shujaa.
Tanzania mpya inakuja, na wewe
unayonafasi ya kustawi katika nchi mpya ijayo katika jina la Yesu. Mungu
anawatafuta waliodharauliwa na watu, na anakufanya kuwa wa heshima na anaanza
kukufanya hatua kwa hatua.” Nina
kataa balaa zilizopangwa kuharibu kesho yangu, naiona kesho yangu inang’aa katika jina la Yesu.”
Amen
Comments