BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu.
Leo nina
ujumbe wa ajabu sana ambao MUNGU amenipa ili nikuletee. Ujumbe unahusu MAJITU.
Watu wengi
wanatamani kufika mahali fulani kimaisha lakini
kuna vitu ni vikwazo vya kuwakwamisha, hivyo vikwazo ndio JITU
ninalozungumzia leo.
1 Samweli
17:31-46 ‘’Na maneno hayo aliyosema Daudi yaliposikiwa, watu wakamweleza Sauli; naye akatuma mtu kwenda kumwita.
Daudi akamwambia Sauli, Asizimie moyo mtu ye yote kwa ajili ya huyu; mimi mtumishi wako nitakwenda kupigana na Mfilisti huyu.
Sauli akamwambia Daudi,
Huwezi wewe kumwendea Mfilisti huyu upigane naye; maana wewe u kijana
tu; na huyu ni mtu wa vita tangu ujana wake.
Daudi akamwambia Sauli,
Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na alipokuwa akija
simba, au dubu, akamkamata mwana-kondoo wa lile kundi,
mimi hutoka nikamfuata, nikampiga, nikampokonya kinywani mwake; na akinirukia, humshika ndevu zake, nikampiga, nikamwua.
Mtumishi wako alimwua simba
na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa
sababu amewatukana majeshi ya MUNGU aliye hai.
Daudi akasema, BWANA
aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono
wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na BWANA atakuwa
pamoja nawe.
Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii.
Naye Daudi akajifunga upanga
juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi
akamwambia Sauli, Siwezi kwenda na vitu hivi, maana sikuvijaribu. Basi
Daudi akavivua.
Akaichukua fimbo yake
mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji,
akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake,
na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
Huyo Mfilisti naye akamsogelea Daudi na kumkaribia; na mtu yule aliyemchukulia ngao yake akamtangulia.
Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri.
Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.
Ndipo Daudi akamwambia yule
Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi
ninakujia wewe kwa jina la BWANA wa majeshi, MUNGU wa majeshi ya Israeli
uliowatukana.
Siku hii ya leo BWANA
atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako,
nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi
ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko MUNGU katika
Israeli.
‘’.
-Umepanga
kwenda mkoa Fulani ili ukaanze ajira yako ambayo umetafutiwa huko lakini nauli
ikawa kikwazo, nauli hiyo ndio Jitu linalokukwamisha.
-Watu wengi
wamezuiliwa na majitu katika maisha yao.
Wana wa
Israeli walikuwa na nguvu sana ila tu wakisikia jina Goliathi wanaogopa maana
Goliathi lilikuwa ni jitu ambalo hawakuwahi kulishinda.
-Mfalme
Sauli aliliogopa jitu Goliathi.
-Kaka zake
Daudi waliliogopa hili jitu.
-Waisraeli
waliliogopa hili jitu lakini Daudi kijana mdogo
aliijua siri ya kuliondoa hili jitu.
-Wewe ndugu
yangu najua una majitu mengi tu maishani mwako je unajua siri ya kuyaondoa?
Kuna watu
majitu yao ni madeni, yaani umeshindwa kuyaondoa majitu madeni katika maisha
yako.
Jitu ukiliogopa
litakusumbua sana, ona jinsi ambavyo Goliathi aliwadharau Wanajeshi wa Israeli
hadi mfalme wao Sauli. Walikuwa wanaweza kusema chocgote walichotaka kusema
lakini akitokea tu jitu Goliathi wote wanakimbia mbio. Jitu huyu alitisha na
kuwasumbua sana wana wa Israeli kama ambavyo wewe leo unavyosumbuliwa na
majitu. Majitu yako leo yanaweza kuwa kiburi, yaani kila ukiomba hupokei kwa
sababu una kiburi na kila siku wewe ni mtu wa kwanza kuwatukana watumishi wa
MUNGU. Kumbuka kwamba kwa MUNGU kila jambo litatolewa hesabu yake, na
yawezekana kabisa hesabu yako imeanza kutolewa ndio maana hupokei hadi pale
ambapo utaliondoa jitu kiburi na kuacha kuwatukana watumishi wa MUNGU.
Je unataka
kuyaondoa majitu yote katika maisha yako?
1 Yohana
3:8b inasema ‘’ Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.
‘’.
BWANA YESU
alikuja ili tu kila kazi yote ya shetani
iondoke kwa wanadamu na katika kazi zake shetani, majitu ni sehemu muhimu ya
kazi hizo za shetani na kwa kutumia majitu hayo, shetani huwatesa sana watu wa
MUNGU.
Je unataka
kuyaondoa majitu maishani mwako?
Mathayo
11:28 inasema ‘’Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
‘’
BWANA YESU
leo anatutaka tuyapeleke kwake majitu
yote yanayotusumbua ili atupumzishe.
Kaka na Dada
nakuomba kimbilia kwa YESU kwenye uzima. Majitu yatakuachia na utakuwa huru
tena huru kweli kweli.
Bartimayo upofu
ndio ulikuwa jitu lake lakini aliijua siri ya kuliondoa jitu hilo la upofu na
ndio maana bada ya kukimbilia kwa YESU uzima uliingia kwake.
Ndugu
kimbilia kwa YESU leo na majitu yote yataondoka kwako.
Kipindi cha
nyuma mimi nilikuwa mhudhuriaji mzuri sana wa ibada kanisani, sikujua kuokoka
ni nini na sikutaka kuokoka, nilijua kuokoka ni kuhama dhehebu langu zuri na sikuona faida kabisa ya kuokoka,
niliendelea kusali lakini bila uwepo wa MUNGU wala hofu ya MUNGU hata kidogo,
ilikuwa ni jambo la kawaida sana kwenda kanisani ni nikitoka tu kanisani naanza
kutenda dhambi hata nyumbani sijafika, siku nyingine nilikua nawahi kutoka
kanisani ili tu nikafanya machukizo mbele za MUNGU, dhambi ilikua jitu baya sana
kwangu, nilitamani kuacha lakini sikuweza, na licha ya dhambi kuwa jitu kwangu,
jitu jingine kwangu lilikuwa ni uzingizi yaani kila nikiingia tu kanisani
usingizi unanisumbua hadi ibada inaisha, nilidhani ni jambo dogo kumbe hili
jambo lilikuwa ni jitu kubwa sana, yaani adui alihakikisha kila jumapili sipati
neno la MUNGU. Licha ya hayo majitu mawili, kulikuwa na jitu jingine kubwa sana
ambalo ni kusinzia kila nikianza kusoma Biblia, yaani kila nikianza kusoma
Biblia hata kabla sijamaliza mistari miwili lazima nisinzie, hali hii ilinitesa
sana na kuniumiza sana maana nilitamani sana kuisoma Biblia na kuielewa lakini
jitu usingizi alinishinda, ndipo baadae kabisa nikiwa Zanzibar niliisikia sauti
ya MUNGU ikiniambia niende kanisani maana nisipoenda kuna kifo mbele yangu,
niliogopa sana lakini sauti hiyo ilizidi na kuzidi na kupelekea kwenda
kanisani, na wakati huu MUNGU aliniongoza kutafuta kanisa kwa masaa 4 maana
kila kanisa nikienda ndani yangu naambia kwamba ‘’ Sio hapo nilipokuagiza uende’’ hadi kwa
baadae nikajikuta nakutana na mchungaji wangu wa Zanzibar ambaye MUNGU
alimuandaa anisubiri stand, tukaenda naye kanisani na siku hiyo nikaokoka. Na
tangu nimeokoka mwaka 2008 sijawahi kusinzia kanisani, sijawahi kusinzia kwa
sababu ya kusoma Biblia na dhambi zile zilizokuwa zinanisumbua zamani kwa sasa
haziniwezi tena. Tangu siku nimeokoka , majitu hayo BWANA YESU ameyaondoa
maishani mwangu.
Ndugu yangu
tambua neno hili ya kwamba ukitaka majitu yakukimbie basi mpe BWANA YESU maisha
yako na liishi neno la MUNGU.
-Majitu mengi
yanayokubabili maishani mwako ni kwa sababu hujajua tu jinsi ya kuyaondoa.
Siri ya
kuyaondoa ni kumkabidhi YESU majitu hayo na yeye atayaamuru yarudi kuzimu na
kukuacha wewe ukiwa huru.
Ni kweli
kabisa Goliathi alikuwa ni jitu linalotisha sana kwa waisraeli lakini Daudi
kijana mdogo alijua jinsi ya kuliondoa majitu kama haya. Ndio maana Daudi
akakumbuka jinsi ambavyo MUNGU alimshindia kwenye majitu makubwa kama simba na
dubu. Nampenda Daudi kwa maneno haya aliyoliambia jitu Goliathi ‘’BWANA leo atakuua mikononi mwangu, na Dunia
nzima itajua kwamba yuko MUNGU katika Israeli.’’
Hata wewe
leo yaambia hayo majitu kwamba ‘’ Ewe jitu ugonjwa leo utajua kwamba yuko MUNGU
kwangu, na kwa sababu MUNGU yuko upande wangu basi leo majitu yatatoka yote.’’
Kwa jina la
YESU KRISTO majitu yote yatoke kwangu.
Kwa jina la
YESU umeshinda.
Comments