BWANA YESU
asifiwe.
Karibu tena
siku ya leo tujifunze ujumbe usemao ‘’sababu za sisi kujifunza neno la MUNGU.’’
Mathayo 7:24-25
‘’Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
‘’
Si rahisi
kujifunza kitu kama huna umuhimu nacho.
Sio rahisi
kutenga muda wako kwa ajili ya kujifunza jambo Fulani kama huna umuhimu na
jambo hilo.
Sio rahisi
kulipa gharama iwe ni pesa yako au muda wako ili tu kujifunza kitu Fulani, kama
kitu hicho hakina umuhimu kwako.
Kama jambo
ni la muhimu kwetu lazima tu tutenge muda wa kujifunza jambo hilo.
Mwaka 1994
nikiwa na miaka miaka 8 nilianza
kufundishwa kilimo, masomo haya ya kulima hayakuihitaji hiari yangu bali
ilikuwa ni lazima, Walezi wangu walikua na lengo zuri tu kwamba kama
nikifanikiwa kuwa mkulima mzuri basi ningeishi maisha mazuri kijijini kwetu
Isambara, kilimo ni uti wa mgongo wa kijiji kile, Mwaka 1 baadae yaani mwaka
1995 nilianza darasa la kwanza, shuleni ilikuwa ni mbali sana zaidi ya kilomita
9 na wakati huu bado nilikuwa naendelea na kujua kulima, Kila siku nilitakiwa kuwahi kurudi nyumbani kutokea shuleni ili tu kuendelea na kilimo, Kama nitachelewa kufika basi nijue
lazima tu nikute matuta 5 hadi 8 ya kulima ambayo lazima niyamalize ndipo
niende nyumbani, kilimo hakikuwa na mchezo, hivyo ilikuwa ni wajibu wangu
kuwahi nyumbani nikitokea shuleni ili kumalizia viporo vya matuta. Walimu wangu
wa nyumbani walitimiza wajibu wao wa kuhakikisha nakua mkulima bora ili
nisiwasumbue baadae. Walinisaidia sana maana miaka 2 baadae nikiwa darasa la 3
nililima majaruba mawili ya mbunga na kutoa magunia 3 ya mchele na hivyo kupelekea mimi na kaka yangu kuwa
wanafunzi wa kwanza kutoka kitongoji chetu kununua baiskeli ili tuwe tunawahi
shuleni ambako ni mbali sana na walimu ni wakali kupita kawaida. Kujifunza
kulima kule kulinisaidia na kunifanya
niwe mkulima mzuri. Darasa lile la
kilimo hata kama lina magumu yake lakini lilinisaidia sana, Vile vile kujifunza
neno la MUNGU ni darasa jema na lenye manufaa kwa roho yako na uzima wako. Luka
11:28 ‘’ Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.
‘’
Nimesema
huwezi kutoa muda wako kujifunza kitu ambacho hakina manufaa kwako, lakini kama kina manufaa basi utajifunza kwa
gharama zozote. Kilimo nilijifunza kwa
gharama kubwa lakini kilinisaidia sana hivyo hivyo napenda kukuambia kwamba
hakuna kitu muhimu kujifunza kama neno la MUNGU maana .
-Ahadi ya
MUNGU kwako utaikuta ndani ya neno.
-Baraka zako
utazikuta ndani ya neno la MUNGU.
-Ushindi
wako utaukuta ndani ya Neno.
-Ulinzi wako
unatokana na ahadi ya MUNGU kwako, ambayo iko ndani ya neno.
Neno la
MUNGU( Biblia) ni muhimu sana katika maisha yako. MUNGU kila siku anaandaa
watumishi wake kwa ajili tu ya neno likufikie, yaani hakuna ambako hutapata
mafundisho ya neno la MUNGU, Kama uko chumbani kwako ukifungulia tu Wapo FM au
Redio yeyote ya dini lazima utakutana na mahubiri, Semina ndio zipo kila
sehemu, Nyimbo za dini ziko kila sehemu hadi kwenye simu yako hapo ulipo,
Mikutano ya injili ipo kila mahali, Kanisani ndio kabisaaaaa mahubiri kila
siku. Ni MUNGU anazungumza na wewe, hata mitandaoni wapo watumishi wengi sana
ambao MUNGU amewaagiza kulipeleka neno lake huko. Yaani kama kuna mtu ataenda
jehanamu, basi ataenda kwa kupenda kwake mwenyewe ila kama maonyo na neno la
MUNGU lazima tu alilipata.
Huu ni upendo
mkuu sana wa MUNGU kwetu.
Nimetoa
mfano na maelezo ili tu uone umuhimu wa kujifunza neno la MUNGU na faida zake.
Na sasa
nakuletea kiini kabisa cha somo letu yaani SABABU AMBAZO ZINATUFANYA SISI
WATEULE WA KRISTO KUJIFUNZA NENO LA MUNGU SIKU ZOTE.
Ziko sababu
nyingi sana za kujifunza neno la MUNGU lakini muda huu nakuletea sababu 3 kuu za
wewe na mimi kujifunza neno la MUNGU kila mara.
SABABU 11 ZA
KUJIFUNZA NENO LA MUNGU KILA MARA.
1.KWELI YA INJILI YA YESU.
2 Timotheo 2:1-2 ‘’Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika KRISTO YESU.
Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.
‘’
-Tunajifunza neno ili tukawafundishe na wengine maana hii ndio kweli ya injili.
Matendo
19:9-10 ‘’Lakini wengine walikaidi, wakakataa kuamini, wakiitukana ile Njia mbele
ya mkutano; basi, akaondoka akawaacha, akawatenga wanafunzi, akahojiana
na watu kila siku katika darasa ya mtu mmoja, jina lake Tirano.
Mambo haya yakaendelea kwa muda wa miaka miwili, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la BWANA, Wayahudi kwa Wayunani.
‘’
-Huwezi ukanyamaza ikiwa BWANA amekupa agizo, MUNGU anataka watu wajifunze neno hivyo huwapamzigo watumishi wake ili tu neno litufikie na tujifunze.
Matendo 20:20 ‘’ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba,
‘’
-Mitume walipewa mzigo na MUNGU wa kufundisha neno la MUNGU.
-Na hata leo MUNGU anainua maelfu ya watumishi ili tu neno lake litufikie.
-MUNGU anataka tujifunze neno lake.
2. MITUME
WALIAMLIWA NA BWANA YESU.
Mathayo 28:19-20
‘’ Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la BABA, na MWANA, na ROHO MTAKATIFU;
na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
‘’
Marko 16:15-16 ‘’Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa
‘’
3.TUTAKUWA
NA MSINGI IMARA KWA AJILI YA IMANI YETU.
2 Timotheo 3:16-17 ‘’ Kila andiko, lenye pumzi ya MUNGU,
lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa
kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
ili mtu wa MUNGU awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
‘’
4. YESU KRISTO ATAKUWA NA SISI.
Marko16:20 ‘’
Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, BWANA akitenda kazi pamoja nao,
na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.]
‘’
5.TUNAKUWA TUNASHIRIKI PENDO LA
MUNGU.
Yohana 14:21-24 ‘’Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye
anipendaye atapendwa na BABA yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha
kwake.
Yuda (siye Iskariote), akamwambia, BWANA, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?
YESU akajibu, akamwambia,
Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na BABA yangu atampenda; nasi
tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake BABA aliyenipeleka.
6. TUNAKUWA NA UHURU WA KIROHO.
Yohana 8:31-32 ‘’ Basi YESU akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
‘’, Warumi 8:1 ‘’Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika KRISTO YESU.
‘’.
7. ILI TUWE NA HOFU YA MUNGU AMBAYO
ITATUFANYA TUSITENDE DHAMBI.
Zaburi 36:1 ‘’Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake, Hakuna hofu ya MUNGU mbele ya macho yake.
‘’
8. NENO LA MUNGU HUTUONGOZA KUTENDA MEMA.
Zaburi
119:105 ‘’ Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
‘’
-Likituongoza hili neno la MUNGU tunalojifunza, tutamaliza safari salama.
9. NENO NI CHAKULA CHA KULETA AFYA
KATIKA ROHO ZETU.
Mathayo 4:4 ‘’
Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha MUNGU.
‘’
10. KWA SABABU NENO LA MUNGU HALITAPITA KAMWE.
Mathayo 24:35
‘’ Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
‘’
Waebrania
4:12 ‘’ Maana Neno la MUNGU li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko
upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na
roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua
mawazo na makusudi ya moyo.
‘’
11. NENO LA MUNGU HUTUPA UJASIRI
KATIKA YOTE,
Matendo 4:31
‘’ Hata walipokwisha kumwomba Mungu,
mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu,
wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
‘’
Comments