Na Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima. Ufufuo na Uzima,Tanganyika parkers Kawe |
I.
Utangulizi
Waefeso 6:13 Kwa
sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu,
na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
Mtume Paulo anazungumza na kanisa la waefeso hii sura iko kama sura ya
kijeshi vile anaelezea silaha za kuvaa wakati wa uovu. Kuna siku ya uovu ambayo
huwa inakuja kwenye maisha ya mtu na mtume Paulo amesisitiza tuvae silaha zote
kwaajili ya siku ya uovu na siku hii inaitwa siku ya ubaya kwenye “Zaburi27:5 Mradi
atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, Atanisitiri katika sitara ya hema
yake, Na kuniinua juu ya mwamba”. Kuna siku ya ubaya inakuja ambayo wewe
hujui ni lini inakuja inaitwa ni siku ya mabaya na huwezi kujua ni lini inakuja.
“Mhuburi7: 14 Siku ya
kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda
sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote
litakalofuata baada yake.”
Unapaswa kuelewa siku hii
ipo ndio maana mtume Paulo amesema tuvae silaha zote kwaajili ya siku ya uovu.
Imeitwa siku ya uovu au siku ya ubaya au siku ya mabaya
“Mithali 16: 4 Bwana amefanya kila kitu kwa kusudi lake;
Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya. “
Maisha yana siku ambayo imekuwa imepangwa kwa namna fulani lakini watu
wengi hawajui siku hiyo inakuwa imepangwa.
“Yefania1: 15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa
na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya
mawingu na giza kuu, “
Maisha yalianzia rohoni kabla hayajaja mwilini na unapo mwona mtu
ameshinda mwilini alishinda kwanza rohoni, mabaya matatizo dhiki tabu magonjwa
na mabaya mengine yanakuwa yamepangwa kuanzia rohoni kambla hayajatokea mwilini,
kawaida kuna ulimwengu wa rohoni na ulimwengu wa mwilini na mambo mengi
yameanzia rohoni mfano Yesu alikuwepo rohoni na akaja mwilini lakini alikuwa
Mungu neno rohoni “hapo mwanzo kulikuweko….” Kwahiyo Yesu kabla hajamwaga damu
alikuwepo rohoni kwanza. Ukimwona mtu amepata ajali; ajali hiyo imeanzia rohoni
kwanza ukimwona mtu amefukuzwa kazi; alifukuzwa rohoni kwanza na uwezo wako wa
kushinda mwilini huanzia rohoni kwanza na kushindwa kwako mwilini huanzia
rohoni kwanza, ukimwona mtu ameshindwa kitu mwilini jua alishindwa rohoni
kwanza “Ufunuo9: 15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa
wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue
theluthi ya wanadamu.” hawa
malaika wameandaliwa kwa wakati Fulani saa, siku, mwezi na mwaka wameandaliwa
kwenye siku ambayo imepangwa Mungu ni mungu wa wakati na majira wakati wa
kupanda nawa wakati wa kuvuna, wakati wa kupanga mawe na wakati wa kutupa mawe,
wakati wa kuua na wakati wa kuhuisha. Wewe unaweza kudhani ni bahati mbaya,
hapana ni siku imepangwa kuanzia rohoni kwaajili ya saa siku mwezi na mwaka fulani
na wala sio bahati mbaya.
II. SOMO
Mungu ana majira ana wakati ana mwezi ana saa na ukisoma hapo unaona
malaika wamefungwa kwaajili ya saa na siku Fulani. Ajali inaanzia rohoni baadae
inakuja mwilini ukiliona taifa limeanza kumtegemea mganga wa kienyeji ujue
limefika mahali fulani rohoni, ukiona kanisa limekuwa jua limefikia mahali Fulani
rohoni kawahiyo siku ya uovu ni siku iliyoandaliwa tokea rohoni.
“Matendo ya mitume 13: 6 Walipokwisha
kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa
uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;
7 mtu huyu
alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita
Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.
8 Lakini
Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka
kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.
9 Lakini
Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,
10 akasema,
Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi
kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?
11 Basi,
angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda.
Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa
kumshika mkono na kumwongoza. “
Hapa mtume Paulo ametoka amekwenda kuhubiri ulaya mji wa pafo amekwenda
kuhubiri pale amealikwa na mkuu wa mkoa na alipofika pale mkuu wa mkoa alikuwa
ana akili nyingi na msomi lakini akasema aende na msaidizi wake bar yesu ambaye
ni mchawi, sasa mtume Paulo akaanza kumfundisha injili ya Yesu na mkuu wa
mkoa akawa amsikiliza kwa makini lakini
kwenye ulimwengu wa rohoni yule bar yesu(mchawi) akaanza kumtupi vitu ili
aiache ile Imani iliyokuwa inamwingia. Biblia inasema akaanza kumpa moyo wa
kuiacha ile Imani aanze kuahirisha kumsikiliza mtume Paulo lakini mkuu wa mkoa
anafikiri ni akili zake kumbe alikuwa anarushiwa vitu vya kuiacha ile Imani.
Sasa Paulo akamwona huyu bwana akaondoa macho wa yule liwali na kumwangalia
anayemletea upinzani (bar yesu) akamwambia uwe kipofu wa muda akamwambia ewe
mwana wa uovu huachi kuzipotosha njia za Bwana na uwe kipofu kwa muda na biblia
inasema viganda vikaingia kwenye yule bar yesu na yule liwali alipoona mabo
yale aliyaamini mafundisho ya Bwana.
Kwahiyo wachawi ni wa rohoni wanatenda mambo yao usiku na hawaonekani
unakuta mtu anakuja anakuwangia usiku na ukiamka unaanza kujisikia uchovu au
humpendi mkeo au hali yeyote ile mbaya na hujui kama umefanyiwa hiyo hali
ikutokee kuanzia rohoni. Neno la Bwana linaitwa upanga wa roho maana yake
linaweza kukata mabaya yeyote yale yanayopandwa rohoni na wachawi siku ile ya
uovu. Kwa kawaida wachawi wakitaka kuua mtu wanapanga siku tarehe na saa ya
kumuua mtu. Siku ya uovu ni siku ambayo imepangwa mtu atendewe uovu/ubaya mfano;
siku ya kufa mgonjwa unashangaa watu wanashauri mtu mgonjwa asafirishwe hadi
hospitali fulani au apelekwe kwa mganga fulani kumbe ni sehemu ya kufanyika
tukio lake la uovu katika siku ya uovu na unakuta anaenda kufia huko. Kabla laana
haija mpata mtu imepangwa rohoni, kabla ajali haija mpata mtu imepangwa rohoni
kwenye ulimwengu wa rohoni kuna matukio yanapangwa kabisa kabla hayajatokea
mwilini iwe ni ajali, kufilisika,kufukuzwa kazi,kuachika, kufeli mitihani au
mabaya yeyote yale yanapangwa rohoni kwanza kabla hayaja tokea mwilini. Mungu
ni roho lakini ana miguu biblia inasema ameweka miguu yake duniani na shetani
ni roho lakini anaweza kuandika na kusajili majina kwaajili ya siku ya uovu na
wewe uliyeokolewa na Bwana Yesu hatusomeka majina yako au biashara yako haitasomeka
katika ulimwengu wa rohoni, ndoa yako haita someka na usiposomeka rohoni, mwilini
hakuna baya litakalo kupata “Nailifuta jina langu kwenye madhabahu yeyote
iliyotaja jina langu, iliyo andaa ajali kwaajili yangu kwa jina la Yesu”.
“2Thesalonike2:3 Mtu
awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule
ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;“
Hapa alizuiwa rohoni na shetani na shetani anaweza kushindana na mtu
rohoni na watu wengi wanajua kwamba shetani hawezi kuingia mwilini sababu kuna
roho mtakatifu ni kweli na jua shetani anatumia njia mbili kwanza anaweza
kushindana na wewe akiwa njie ya mwili “Zakaria3:1-
1 Kisha
akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na
Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.
2 Bwana
akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua
Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni?
3 Basi,
Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika.
4 Naye
huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi
zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami
nitakuvika mavazi ya thamani nyingi.“
Pia anaweza kukumiliki rohoni ukitaka kwenda kanisani kichwa kinauma,
ukija kanisani unataka kuondoka ndiomana Yesu allipokuwa akiondoka aliwaambia
mkizubaa shetani atawapepeta kama ngano; japo alisema ametupa mamlaka ya
kukanyaga nyoka na n’ge lakini shetani hachoki na anatumia njia hizo na sio
lazima shetani awe ndani anaweza kuwa nje kwa sababu huja kaa vizuri mfano
ukienda kuomba kazi hupati japo vigezo unavyo na umeokoka maanake ni kuna
mamlaka imejipanga rohoni kukufuatilia kila utendalo na uendako ili kukuzuia.
“Siku ya uovu iliyo pangwa kwa ajili yangu ninaifuta kwa jina la Yesu,
ninaifuta siku ya ubaya iliyoandaliwa kwaajili yangu ninaifuta kwa jina la
Yesu”
Kuna mashetani maalum kwaajili ya kila siku ya uovu wameandaliwa na
hutumika kwaajili ya mambo fulani yanayotaka kutokea kwaajili ya siku ya
uharibifu na mashetani ni malaika(walioasi) na sifa mojawapo ya malaika
wanaweza kujubadilisha maumbo yao wakawa binadamu au upepo Yuda1:6 ufunuo12:7
Mungu alimwambia shetani kwa habari ya ayubu akamruhusu amguse lakini asiguse
roho yake na unaona upepo ulivuma pande zote katika nyumba ile kumbe ni shetani,
malaika walijibadilisha wakavaa maumbo ya kibinadamu na kwenda kumtembelea Ibrahimu
wakala wakaondoka na tunaposema tukio la siku ya uovu ni kama tukio la kupata
ajali ambayo mtu (malaika mwovu) anasababisha ni kwamba yule mtu wa siku ya
uovu anaweza kuwa ni shetani amevaa umbo la mwili na tayari tukio lilishapangwa
tokea ulimwengu wa mwilini. Na mashetani hawa walishafika eneo la tukio tayari
kwaajili ya siku hiyo “katika jina la Yesu naifuta tarehe ya ubaya na uovu
kwaajili ya familia yangu tarehe ya uovu tarehe ya ubaya juu yangu ninaifuta
kwa jina la Yesu”
Kuna baadhi ya mambo yamepangwa kwenye maisha yako na wewe unasema ni
bahati mbaya kumbe yamepangwa na biblia inasema nitakuokoa na mtego wa mwindaji
shetani anaitwa ni mwindaji. Na anakuwinda na kama hujaokoka na huna Yesu
anakupata kwa urahisi ni lazima siku ya uovu ikupate na huwezi kuiepuka “katika
jina la Yesu ninaiharibu siku ya ubaya siku ya uovu iliyopangwa kwenye maisha
yangu naiharibu kwa jina la Yesu siku ya ajali, siku ya kifo naiharibu kwa jina
la Yesu na kila aliye ipanga namrudishia yeye kwa jina la Yesu”
Katika kitabu cha Mathayo mamajusi waliiona nyota ya Yesu hata kabla
hajazaliwa na walikuwa ni wachawi na ile nyota ikawaashiria kwamba kunamtu
Fulani amezaliwa mahali Fulani ni mfalme ndio maana alisema yuko wapi
aliyezaliwa huyu mfalme wa wayahudi na inatupa ufahamu kwamba shetani na wachawi
wanaweza kuona maisha yako miaka ijayo na wakaanza kushindana na wewe leo.
Kwenye ulimwengu wa rohoni kuna kiashiria cha mafanikio ya mtu ya baadae kabla
mtu hajafanikiwa na wachawi wanaona utakuwa mtu gani baadae na wewe unashangaa
unachukiwa bila sababu ni kwasababu wanafahamu utakuwa nani baadae ndio maana
watu wote wanaotumiwa na Mungu leo walipita kwenye matatizo kwanza kabla Mungu
hajawatumia mfano: Musa alitakiwa auwawe lakini kwenye ulimwengu waroho shetani
alikuwa anajua kwamba kuna mtu anakuja ambaye atawaokoa wana wa Israeli baadaye
na hata wewe leo hii ndio maana wanafanya vita mbele yako wanajua utakuwa nani
siku zijazo haitoshi Yesu alipozaliwa herode alitoa amri wauwawe watoto wakiume
lakini alikuwa analengwa Yesu “huta kufa bali utaishi ili uyasimulie
matendo makuu ya Bwana” “japo ninapatwa
na matatizo mengi sitakufa mpaka nimetimiza kusudi la Bwana” wameona utakuwa nani baadae wametuma watu
wanaoonekana ni binadamu lakini ni mashetani wametumwa kukuzuia usifikie kusudi
lako wametumwa, mashetani majini, wachawi wanataka kukuzuia usiwe kama
ulivyokusudiwa na Bwana lakini Biblia inasema hakuna atakaye zua vile
ulivyopangiwa na Bwana. Wataangukia pua wanaofanya vita na wewe wachawi na wote
wanaofanya watakuinamia “kwa jina la Yesu nitakuwa kama vile Mungu alivyo panga
niwe katika jina la Yesu, siku ya ubaya iliyoandaliwa juu yangu naishinda kwa
jina la Yesu ile siku ya mabaya ninaifuta kwa jina la Yesu” mabaya hayatakupata
wewe wala tauni haitakariba hemani mwako kwa jina la Yesu.
Mashetani duniani wako wa aina nne tu
1.
Majoka walioanguka toka mbinguni “Ufunuo12: 7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika
zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika
zake;” wanauwezo wa kuvaa
maumbo yeyote yale lakini ni nyoka mashetani
2.
Majini, wanaoendana na mila za kiarabu lakini
wanatenda mapenzi ya kishetani
3.
Mizimu wanaoendana na familia kuleta magonjwa ya
kurithi, wanaweza kuelekezwa kwenye familia wakaelezwa familia hii isizae au
isifanikiwe au izae inje ya ndoa mfano Ibrahimu na isaka na mtoto wake
walipatwa na urithi wa kupatwa na shida ya kuza hii inatufundisha kuna mambo
yanatokea kwenye ukoo ambayo ni ya kujirudia rudia, na kuna koo nyingine hata
ukisoma namna gani hawawezi kupata kazi na shida zinaanzidi kumbe tatizo ni
mizimu.
4.
Miungu ni mashetani yanayo abudiwa; mabudha na
wengine kibao
“Hawa wote wanaitwa mapepo”
nashindana na mashetani wanaoongoza familia yangu kwa jina la Yesu mashetani wa
talaka, aibu, umaskini, kukataliwa walioandaliwa kwaajili ya siku ya uovu/mabaya
nashindana nao kwa jina la Yesu.
Kwahiyo haya mashetani yanakuwa
yameshatumwa karibu na wewe walishafika ili waharibu ndoa yako,kazi yako,
bihashara yako na maisha yako. “kwaajina la Yesu ninaharibu siku ya ubaya
iliyotengwa na wakala wa shetani kwaajili yangu, aliyeiandaa ajali, kuharibu mahusiano yangu
ninaamuru impate Yeye aliye iandaa kwa
jina la Yesu, kifo kimpate yeye aliyekiandaa kwa jina la Yesu,” ninafanya vita
na kila aliye elekezwa kwangu kwaajili ya siku ya ubaya aliyetumwa siku yeyote
ninashindana naye leo kwa jina la Yesu.
Kila silaha itakayo fanyika juu
yangu haitafanikiwa kwa jina la Yesu kwa jina la Yesu”kwa damu ya mwanakondoo
nina jitakasa kwaajili ya vita vya Bwana kuanzia leo saa yeyote niliyopangiwa
tukio kwenye ulimwengu wa roho ninaifuta kwa jina la Yesu, siku ya uovu
iliyopangwa kwajili ya taifa langu ninaifuta kwa jina la Yesu.
III.
MAOMBI.
Baba Mungu ninaomba unipe nguvu
kwaajili ya vita ya kuteketeza siku ya uovu juu yangu kwa jina la Yesu. Ninaharibu
mabaya yote yaliopangwa siku ya uovu kwa jina la Yesu, ninateketeza mashetani
yote yaliopangwa kwaajili ya siku ya uovu kwa damu ya mwanakondoo, ninatengua
kila mauti iliyopangwa juu ya familia yangu kwa jina la Yesu, ee mkuu wa bahari
ninakukamata katika jina la Yesu na mawakala wako wote ninakushambaratisha kwa
damu ya mwanakondo, katika jina la Yesu ninatengua matukio yaliopangwa juu
yangu kwaajili ya siku ya uovu ninayasambaratisha kwa jina la Yesu kwa damu ya
Yesu imeandikwa mabaya hayatanipata mimi wala tauni haita ingia hemani mwangu
ninaharibu mabaya yaliopangwa kwenye bihashara yangu kwa damu ya mwana kondoo,
ninaharibu na kuteketeza mashetani yote yalioandaliwa kwaajili yangu katika
siku ya uovu kwa jina la Yesu, ninatengua kila ajali iliyoandaliwa na makuhani
wa kishetani juu yangu na familia yangu kwa jina la Yesu, kwa mamlaka ya jina
la Yesu ninafuta kila saa na mwaka wa siku ya uovu na mabaya juu yangu na
familia na kwa jina la Yesu.
AMEN.
Comments