BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze.
Mhubiri
12:14 ‘’Kwa maana MUNGU ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.
‘’
Kila kazi,
kila neno la siri vitaletwa hukumuni.
Kila mtu ana
kazi yake, kila mtu anapenda kuwa na kazi yake , Kila mtu ana matarajio ya kuwa
na kazi yake.
Kazi hapa
inamaanisha yote tunayoyatenda ikiwemo na kazi zetu za kuajiriwa zitaletwa
hukumuni.
-
Huwa
najiuliza hivi Daktari unayetoa mimba kisa tu umesomea, Je MUNGU
anakuchukuliaje?
-
Askari
unaye kula rushwa, je MUNGU anakuchukuliaje?
-
Wakili
unayetetea uongo ambao ni dhahiri, Je MUNGU anakuchukuliaje?
-
Hakimu
unayepotosha hukumu ili tu kuwapendezesha watu Fulani, Je MUNGU
anakuchukuliaje?
-
Wewe
unayetumia kazi yako ili tu kuwanyanyasa wengine, je MUNGU wa mbinguni
anakuchukuliaje?
-
Mganga
wa kienyeji ndio kabisa umembeba shetani kuanzia mwilini mwako hadi kwenye
hirizi unazotumia, Je MUNGU aliye hai anakuchukuliaje?
Neno la
MUNGU linasema kila kazi italetwa hukumuni.
Wengi
wamepelekwa motoni na kazi zao walizokua wanazifanya wakiwa duniani.
Kazi nyingi
ni njema lakini zikiingiliwa na shetani
zinakuwa mbaya sana.
Badala ya
kutenda haki , wengi hutenda uovu kupitia kazi zao. MUNGU atusaidie.
Kazi nyingi
hata neno la MUNGU linazikubali mfano Luka aliyeandika kitabu cha Luka
mtakatifu na matendo ya mitume alikuwa Daktari lakini hakutoa mimba na tena
kazi yake ilikuwa njema kwa MUNGU.
-Watu wa TRA
ni muhimu sana kwa taifa lakini neno la MUNGU linasema juu yao kwamba ‘’
Msitoze kitu zaidi ya mlivyoamriwa-Luka 3:12’’
-Wanajeshi,
Polisi, mgambo na askari magereza ni muhimu sana katika taifa letu lakini neno
la MUNGU linasema juu yao kwamba ‘’ Msimdhulumu mtu, Msimshitaki mtu kwa uongo,
tena mtoshewe na mishahara yenu- Luka 3:13’’
Ndugu yangu
-usikubali
kazi yako ikutenge na MUNGU wako.
-Usikubali
kazi yako ikutenge na uzima wa milele.
-Usikubali
kazi yako ikutenge na mbingu.
-Usikubali
kazi yako ikutenge na uwepo wa MUNGU maishani mwako.
Kina Daudi
walikuwa wafalme lakini walimpendeza MUNGU, Kina Yusufu walikuwa mawaziri wakuu
lakini walimpedeza MUNGU, Kazi yako ndugu isikutenge na MUNGU wako.
Nemesema
kila mtu ana kazi yake, haijarishi ni kazi nzuri au ni kazi mbaya. Wengine kazi
zao ni uzinzi, wengine kazi zao ni kujiuza, wengine kazi zao ni ulevi , wengine
kazi zao ni uongo. Hizo zote ni kazi na zitaletwa hukumuni.
Hakuna asiye
na kazi, yawezekana wewe hujaajiriwa serikalini lakini kazi yako ikawa ni
umbeya na uchonganishi.
Kila kazi
italetwa kwenye mizani ya MUNGU ili kuhukumu.
Usikubali
kazi yako ikawa machukizo kwa MUNGU.
Baada ya
kuongelea kazi sana tugeukie Neno la siri.
Nen la siri
nalo litaletwa hukumini.
Haijarishi
neno hilo ni jema au baya.
BWANA YESU
anasema katika Mathayo 12:36 kwamba
‘’Basi , nawaambia, kila neno la siri watakalolinena wanadamu, Watatoa hesabu
ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki na kwa
maneno yako utahukumiwa.’’
Nachopenda
ujue pia ni kwamba kila neno liwe zuri au baya huanzia moyoni na baada ya hapo
ni kitendo.
Mawazo yako
yote kwa MUNGU yanafahamika. Ndugu hata kile ambacho ni siri ya moyo wako tu,
hujawahi kumwambia mtu lakini napenda utambue kwamba kwa MUNGU kinafahamika.
Ndugu zangu
tuchunge sana maneno ya vinywa vyetu, tusicheke na watu kwa nje tu huku mioyoni
mwetu tunawachukia , na mioyoni mwetu tunatamani wafe kabisa.
Kazi yako
itahukumiwa na pia maneno ya kinywa chako yatahukumiwa. Ndugu zangu tuwaze mema
na tutende mema. Tuwabariki watu na usithubutu kuwalaani watu kwa kinywa chako.
Ila Kama
kuna jambo la siri baya ambalo unalo, na uovu huo umeshindwa kabisa kuacha
nakushauri usifanye siri, waone watumishi wa MUNGU waaminifu na watakuombea
utapona juu ya hilo.
Kusikitika
tu kwamba uongo imekuwa sehemu ya maisha yako na umeshindwa kuacha,
haitakusaidia, ni heri kwenda kanisani na kumwona mchungaji ili akuombee.
Kinywa chako
kisikutenge na MUNGU wako.
Tumia kinywa
chako kwa mazuri, maana kinywa chako kinaweza kusababisha uzima au mauti.
Hata kuokoka
tunaokoka baaya ya kumkiri BWANA YESU kwa vinywa vyetu na kuanza kuukulia
wokozi katika mafundisho kanisani.
Warumi 10:9-11
‘’ Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa
chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua
katika wafu, utaokoka.
Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.
‘’
Njia nzuri
ya kukitumia kinywa chako ni katika;
1. Kuwaongoza watu kutenda mema.
2. Kuwafundisha watoto wetu kumjua MUNGU na wajue MUNGU anataka nini kwao.
3.
Kuwafariji wengine katika upendo wa KRISTO
4. Kuwashirikisha wengine wokovu wetu.
5. Kuwaombea wengine ili MUNGU
awasaidie.
6. Kukemea dhambi na kuonya watenda mabaya.
7. Kumshukuru MUNGU kwa maombi.
Tumia kinywa chako kwa hayo na MUNGU
akubariki sana.
Comments