AMOS OMELA AFUNGA NDOA

Utukufu apewe BWANA
Hayawi hayawi mwisho yamekuwa.
Watumishi wa MUNGU Amos Omela Fumbuka na Lucy Daniel Wamefunga ndoa katika kanisa la Kawe Pentecostal Church(KPC) Kawe.
Ndoa hiyo aliifungisha Askofu wa jimbo la Dar es salaam kanisa  P A G(T) Thomas Dige.
Askofu Dige aliwasifu maharusi kwa uaminifu wao kwa MUNGU na kuwataka vijana wengine kuiga mfano huo. Kiongozi wa ibada hiyo alikuwa ni Mchungaji Kiongozi wa KPC Mchungaji Elly Boto ambapo kabla ya kumkaribisha askofu Dige alisema kuwa vijana hao wamekamilisha taratibu zote ambazo zinatakiwa na hata Darasa la ndoa wamejifunza na kufanya vyema sana na wanahitaji pongezi.

“Apataye mke (mume) apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA “-Mithali 18:22.
Waefeso 5:33 “Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.” 
Upendo ni nguzo ya Pili na pia ni moja ya tunda la Roho katika ndoa. Hapa naomba nieleze hii ndoa inayoongelewa ni ya Kikristo hivyo upendo huu hauwezi kuutenga na upendo wa Kristo kwa ujumla,
Zifuatazo ni baadhi tu ya picha za tukio hilo.
pia kumbuka Amos ndiye aliyetoa ushuhuda huu wa ajabu na MUNGU alimtetea na sasa amempa baraka mpya kama hukusoma ushuhuda huo FUNGUA HAPA
Lucy akiwa tayari kuingia kanisani.

ALICHOKIUNGANISHA MUNGU, MWANADAMU ASIKITENGANISHE.

Amos akiingia agano la ndoa takatifu na Lucy

Ni kama Lucy anasema hivi  ''Nimekuchagua Amos ili uwe wangu wa maisha''

Lucy akisaini cheti cha ndoa.

Kwa YESU ni raha sana

Baada ya kufunga ndoa, hapa wakiwa na ndugu na  marafiki nje ya kanisa.

Mambo mazuri sana

Hakika wamependeza sana.

Nakurudisha nyuma kidogo '' Hapa ni kipindi Amos na msimamizi wake wakiingia kanisani kanisa zima walitoka nje ili kumsindikiza.''

Amos anasema kwamba ''WEWE LUCY NDIO MKE WANGU'' Na Lucy naye anasema ''AMOS WEWE NDIO MME WANGU''

Waebrania 13:4 “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.”

Wakijiandaa kwenda beach kupiga picha



Tunafurahi na wanaofurahi.

Ukumbini

Keki

BWANA YESU awafunike, awape watoto na awape familia njema. mbarikiwe sana tena sana watumishi wa MUNGU.

Comments