BWANA YESU
asifiwe.
Karibu
tujifunze.
Wateule wa
MUNGU tuko safarini hapa duniani, hatujafika bado kule tuendako. Tuendako ni
mbinguni ambako yako makao yetu aliyotuandalia BWANA YESU. Nampenda sana BWANA
YESU maana alisema ‘’ -Yohana 14:2-3,
Nyumbani mwa BABA yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana
naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja
tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.’’
-BWANA YESU
kwenye maandiko hayo anaongea na wale waliompokea.
-Waliompokea
YESU wana kibali cha kuishi mbinguni.
-Hawahitaji
visa card maana Visa card yao ni kumpokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wao.
-Hawa ndio
waabuduo halisi, waabuduo halisi tayari makao yao ya milele yako mbinguni
yameshaandaliwa na BWANA YESU.
-Biblia
inawashauri wateule hawa kuendelea tu kumwabudu MUNGU BABA katika roho na
kweli, wasiyumbishe na dunia, wasiogope wanavyoviona kwa mwili bali wavae nira
ya BWANA YESU siku zote.
JE UNATAKA
KUMWABUDU MUNGU KATIKA KWELI YAKE?
Yohana 4:24
‘’ MUNGU ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
‘’
Kama unataka
kumwabudu MUNGU katika kweli yake yote hakikisha unafanya yafuatayo.
-Waabuduo
halisi humwabudu MUNGU katika Roho na kweli.
-Humwabudu
MUNGU katika utakatifu.
-Humwabudu
MUNGU katika ukweli.
-Humwabudu
MUNGU katika KRISTO YESU pekee.
-Humwabudu
MUNGU peke yake.
-Humwabudu
MUNGU BABA siku zote za maisha yao.
-Humwabudu
MUNGU bila dhambi.
Je unataka
kumwabudu MUNGU BABA katika ukweli wake?
1.
Okoka.
Yohana 1:12-13 ‘’ Bali wote waliompokea(YESU) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake;
waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU.
‘’
BWANA YESU alikuja kukutafuta wewe ndugu ili tu akuokoe Luka 19:10 ‘’ Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea. ‘’
BWANA YESU alikuja kukutafuta wewe ndugu ili tu akuokoe Luka 19:10 ‘’ Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea. ‘’
2.
Liishi
neno la MUNGU. Zaburi 119:105 ’’ Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
‘’
Ni baraka kubwa kulisikia neno la MUNGU na kulishika Luka 11:28 ‘’heri walisikiao neno la MUNGU na kulishika. ‘’
Ni baraka kubwa kulisikia neno la MUNGU na kulishika Luka 11:28 ‘’heri walisikiao neno la MUNGU na kulishika. ‘’
3. KRISTO
aishi ndani yako siku zote na wewe kaa ndani ya KRISTO siku zote.Warumi 8:10-11 ‘’ Na KRISTO akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki. Lakini, ikiwa ROHO yake yeye
aliyemfufua YESU katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua KRISTO YESU katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa,
kwa ROHO wake anayekaa ndani yenu.
‘’
Mabadiliko hutokea baada tu ya kumpokea BWANA YESU, Hukumu zote za nyuma zinafutwa 2 Kor 5:17 ‘’Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. ‘’
Mabadiliko hutokea baada tu ya kumpokea BWANA YESU, Hukumu zote za nyuma zinafutwa 2 Kor 5:17 ‘’Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. ‘’
4.
Uwe
mwanamaombi siku zote. Yohana 14:13-15 ‘’ Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili BABA atukuzwe ndani ya Mwana.
Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.
Mkinipenda, mtazishika amri zangu.
‘’
Ndugu maombi humkimbiza shetani, maombi huwadhuru wachawi, kwa maombi utakuwa huru siku zote na utapona kila ugonjwa na kila udhaifu Yakobo 5:16 ‘’Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. ‘’ ,
Maombi ni maisha. 1 Thesalonike 5:16 ‘’ ombeni bila kukoma;‘’
Ndugu maombi humkimbiza shetani, maombi huwadhuru wachawi, kwa maombi utakuwa huru siku zote na utapona kila ugonjwa na kila udhaifu Yakobo 5:16 ‘’Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. ‘’ ,
Maombi ni maisha. 1 Thesalonike 5:16 ‘’ ombeni bila kukoma;‘’
5.
Ongozwa
na ROHO MTAKATIFU.Warumi 8:9‘’ Lakini ikiwa ROHO wa MUNGU anakaa
ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu
awaye yote asipokuwa na ROHO wa KRISTO, huyo si wake.
‘’,
6.
Usifanye
dhambi.1 Yohana 2:1-2 ’’Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na
kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa BABA, YESU KRISTO mwenye
haki,
naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.
‘’,
dhambi ni mbaya sana na dhambi huleta mauti na dhambi ni mama wa jehanamu maana dhambi huzaa jehanamu 1 Yohana 3:8 ‘’ atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. ‘’
dhambi ni mbaya sana na dhambi huleta mauti na dhambi ni mama wa jehanamu maana dhambi huzaa jehanamu 1 Yohana 3:8 ‘’ atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. ‘’
7.
Uwe
na imani thabiti. Waebrania 11:6 ‘’Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye
MUNGU lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale
wamtafutao.
‘’
Waliookolewa wana imani thabiti na walio na imani thabiti wako ndani ya KRISTO , Wamezaliwa upya kwa ROHO 2 Kor 5:7 ‘’Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. ‘’
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Waliookolewa wana imani thabiti na walio na imani thabiti wako ndani ya KRISTO , Wamezaliwa upya kwa ROHO 2 Kor 5:7 ‘’Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. ‘’
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
Comments