BWANA YESU KRISTO
asifiwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze ujumbe wa MUNGU unaoleta mabadiliko, kufunguliwa na uponyaji.
Leo
tunajifunza kuhusu taji ambazo tutapewa wateule wa MUNGU tukifika mbinguni.
Ufunuo 3:11 { Naja
upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. }
BWANA YESU
kwenye hilo andiko anasema ‘’Shika sana ulichonacho asije mtu akaitwaa taji
yako’’
1 Kor 9:25 ''Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali SISI TUIPOKEE TAJI ISIYOHARIBIKA.''
1 Kor 9:25 ''Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali SISI TUIPOKEE TAJI ISIYOHARIBIKA.''
Taji
atakayotoa BWANA YESU ni muhimu sana.
Kuna taji nyingi ambazo watapewa watakatifu baada ya kushinda ya dunia.
Mathayo 13:43 ''Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa BABA yao. Mwenye masikio, na asikie.''
Mathayo 13:43 ''Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa BABA yao. Mwenye masikio, na asikie.''
Kuna
-Taji ya
uzima(Yakobo 1:12)
-Taji ya
haki(2 Timotheo 4:7-8)
-Taji ya
utukufu(1 Petro 5:4)
-Taji
isiyoharibika( 1Kor 9:25)
-Taji ya
mfia imani.(Ufunuo 2:10)
Taji hizi
saba watapewa watakatifu wa MUNGU, Kila mtu sawasawa na sifa ya taji yake ila
taji ya uzima tutapewa wote tutakaoingia uzimani yaani wote waliokombolewa kwa
Damu ya YESU KRISTO na kufanyika watoto wa MUNGU kwa yeye tena wameliishi neno
la MUNGU.
-Taji ya
uzima ni ya wote wateule wa KRISTO watakaovumilia mpaka mwisho.
-Kuna watu
watapata taji zaidi ya moja kulingana na kile walichokifanya duniani.
-Kwa sehemu
ndogo sana naomba nizungumzie Taji ya utukufu.
Taji ya
utukufu watapewa wateule wa BWANA YESU ambao waliwaongoza wengine katika kutenda mema, Daniel 12:3 ''Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.''
Taji ya utukufu ni muhimu sana, na Biblia inaendelea kusema.
1 Petro 5:4 ‘’ Na Mchungaji mkuu(YESU) atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka. ‘’
Taji ya utukufu ni muhimu sana, na Biblia inaendelea kusema.
1 Petro 5:4 ‘’ Na Mchungaji mkuu(YESU) atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka. ‘’
Ndugu yangu,
hapa unaweza ukajiona kabisa kwamba unastahili taji gani na kama ukivumilia
hadi mwisho wa maisha yako BWANA YESU atakupa taji Zako au yako unayostahili.
Taji ya utukufu wataipata wale ambao walikuwa wanawaongoza wengine katika kutenda mema.
Leo
nazungumzia TAJI YA MFIA IMANI.
Hii ni taji
ngumu kidogo maana kunahitajika uvumilivu na kujaa ROHO MTAKATIFU. Ufunuo 2:10-11 ‘’Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo
Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki
siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima. Yeye aliye na sikio,
na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye
hatapatikana na madhara ya mauti ya pili.’’
Sifa muhimu
ili kuipta taji hii ni ‘’UWE MWAMINIFU KWA YESU HATA KUFA’’
Taji hii
wataipata wale ambao licha ya mateso waliyoyapata kwa sababu ya KRISTO lakini
walivumilia hadi mwisho. Kuna mambo yanaweza kuruhusiwa kabisa maishani mwako
lakini BWANA leo anakutaka uvumilie mpaka mwisho. Mitume na manabii
walivumilia. Kuna ambao kwa kujitoa kwako na kuvumilia kwao ndio maana leo
injili umetufikia mimi na wewe, haikuwa kirahisi hivyo. Kuna ambao waliwekwa
kwenye mapipa ya mafuta yanayowaka moto mkali lakini bado walisema ‘’YESU ni BWANA’’. Kuna
watumishi walikatwa mikono na kukata na mapanga na bado walibaki katika BWANA
YESU. Hakika walifanya kazi inayohitaji TAJI YA MFIA DINI. Ndugu yangu, swali
kwako ni hili, je utavumilia na kumkiri YESU KRISTO kama BWANA na MWOKOZI wa
maisha yako hata kama ni katika kipindi kigumu?
-Je utasema
YESU ni BWANA na Mwokozi wako hata kama ukoo wako watakufukuza na kutaka kukuua
kwa sababu tu umeamua kuokoka?
-Je utasema
‘’Kufa ni faida na kuishi ni KRISTO’’ Hata kama unataka kunyongwa kwasababu ya
kumtumikia BWANA YESU?
Stephano
alivumilia hadi mwisho, alikuwa mwaminifu hata kufa. Biblia inasema hivi juu ya
yaliyomtokea Stephano na bado akavumilia hadi mwisho. Matendo 7:54-60 ‘’ Basi
waliposikia maneno haya, wakachomwa mioyo, wakamsagia meno. Lakini yeye akijaa
ROHO MTAKATIFU, akakaza macho yake, akitazama mbinguni, akauona utukufu wa
MUNGU, na YESU akisimama upande wa mkono wa kuume wa MUNGU. Akasema, Tazama! Naona mbingu
zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa MUNGU. Wakapiga
kelele kwa sauti kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja, wakamtoa nje ya mji,
wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni pa kijana mmoja
aliyeitwa Sauli. Wakampiga
kwa mawe Stefano, naye akiomba, akisema, BWANA YESU , pokea roho yangu. Akapiga magoti,
akalia kwa sauti kuu, BWANA, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya
akalala. Na Sauli alikuwa akiona vema kwa kuuawa kwake. ‘’
Ndugu zangu,
mtumishi huyu alivumilia hadi mwisho.
-Yawezekana
wewe hata hupitii jaribu gumu kama hili lakini umekubali kabisa kumkana BWANA
YESU na kuirudia dunia.
-Yawezekana
umesemwa tu kidogo na watu walioshiba makande na umelia sana na kurudi nyuma,
wewe wala hujapitia jaribu kama la Stefano lakini kwanini kurudi nyuma?
-yawezekana
muumini mwenzako kakukwaza kidogo lakini hadi umeacha wokovu, ndugu hivi
unaijua jehanamu au unaisikia tu? Ndugu je uzima wa milele umeuchukia kwa
sababu tu ya kusemwa kidogo na wanadamu wanaomwakilisha shetani?
Ndugu yangu,
haijalishi kuna nini.
Haijalishi
nani kasema nini.
Haijalishi
dunia inasema nini.
Tusikubali
kumwacha BWANA YESU maana hakuna uzima kwingine kokote nje na BWANA YESU(Matendo
4:12).
Ndugu zangu,
taji ya mfia dini haipatikana kwa kupigana na mtu yeyote na wala haipatikani
kwa kuitetea dini yeyote ile, ila itapatikana kwa kuvumilia mateso yote kwa ajili ya KRISTO. Vita vyetu sisi sio juu ya damu na nyama
Waefeso 6:12 ‘’ Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali
ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo
wabaya katika ulimwengu wa roho. ‘’.
Na hata ninaposema neno Dini simaanishi dini tunazozifahamu bali naamisha Dini yaani njia ya kumwelekea MUNGU(Ayubu 4:6) Na njia ni moja tu ya kweli yaani YESU KRISTO(Yohana 14:6,YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi. ).
Na hata ninaposema neno Dini simaanishi dini tunazozifahamu bali naamisha Dini yaani njia ya kumwelekea MUNGU(Ayubu 4:6) Na njia ni moja tu ya kweli yaani YESU KRISTO(Yohana 14:6,YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi. ).
Wanaojitoa
mhanga hawawezi kupata taji kutoka kwa MUNGU aliye hai.
Wanaotetea
dini zao wala hawahusiani na MUNGU aliye hai. Wateule wa KRISTO ni watu wa
rohoni na hawatafuti taji kimwili.
BWANA anatutaka
tuvumilie kwa yote ambayo tutapitia, tuwe waaminifu mpaka kufa kwetu. Pia kama
tutapitiamagumu Fulani maishani mwetu ambayo ni hila tu za shetani tunalo jina la YESU
KRISTO la kutupa ushindi, lakini kama kuna jambo ambalo litaruhusiwa kwetu kama
lilivyoruhusiwa kwa Stefano basi tuvumilie.
Ufunuo 6:9 ‘’
Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao
waliochinjwa kwa ajili ya neno la MUNGU, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa
nao. ‘’
-Ndugu yangu
vumilia yote unayopitia.
-Kuna mengine
yanakupata kwa sababu yako mwenyewe maana ulijisahau kuomba.
-Mengine
yanakupata kwa sababu ya kutoitii sauti ya MUNGU.
-Wala
usiseme unajaribiwa na MUNGU bali omba kupitia jina la YESU KRISTO aliye hai,
ila pale kunapohitaji uvumilivu uwe mwaminifu hata kufa na BWANA atakupa taji
ya mfia dini.
Vumilia
ndugu na ongeza sana maombi.
Dada mmoja
alipoamua kuokoka ndugu zake walitaka kumuua, walimtisha sana na kumfukuza,
alikuja kanisani na tukajitolea kumhifadhi kwa muda. Alivumia na sasa ni mke wa
mtumishi mmoja kule Zanzibar, kwa sasa maisha ni mazuri na mama yake ndio kwa
sasa wanamuona wa muhimu kuliko watoto wengine.
Ndugu
vumilia yote na MUNGU yu pamoja na wewe.
MUNGU akubariki sana .
Kwa sasa naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
Comments