Makundi ya kikatoliki yanayopigania haki za wapenzi wa jinsia moja
yameelezea ghadhabu yao kutokana na hatua ya maaskofu wa kanisa hilo ya
kukataa mapendekezo ya kutangaza msimamo kuhusu mashoga, wasagaji pamoja
na watu waliotalakiana na wanaoana.
Wakati wa kumalizika kwa mkutano wa maaskofu wa kanisa katoliki, Vatican
ilishindwa kupata theluthi mbili ya kura za maskofu wa kuunga mkono
maoni yao kuhusu masuala hayo.
Kundi la kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja nchini Marekani la New
Ways Ministry limesema kuwa hatua ya maskofu hao kuamua kujadili suala
hilo ni matumaini ya siku za usoni.
Masuala hayo yanatarajiwa kuzungumziwa tena baada ya mwaka mmoja.
CHANZO: BBC SWAHILI
Comments