Askofu Dr Josephat Gwajima. |
Polisi hao waliokuwa na silaha walifika nyumbani kwa askofu huyo
maeneo ya Salasala jijini Dar wakiwa kwenye magari zaidi ya manne ambapo
walipiga kambi katika eneo hilo kwa saa sita huku njia hiyo ikiwa
imefungwa kwa saa kadhaa kabla ya waandishi wa habari na baadhi ya
waumini wa askofu huyo kuruhusiwa kupita.
Hata hivyo baada ya polisi hao kuzungumza na mawakili wa Gwajima na
viongozi kadhaa wa kanisa hilo, waliamua kuondoka huku wakitoa amri
kiongozi huyo afikie kituo kikuu cha polisi kwa ajili ya mahojiano
zaidi ambapo alifika na baadaye kufikishwa katika Mahakama ya Kisutu
ambapo taarifa za kina kuhusu kilichojiri huko zikiwa bado
hazijapatikana.
Askari wakiwa nyumbani kwa Gwajima.
Makamanda wa polisi wakiwa tayari kwa lolote.
Gari lililombeba Gwajima likitoka ndani ya nyumba yake kuelekea kituo kikuu cha polisi kwa ajili ya mahojiano.
Mawakili wa Gwajima wakisalimiana na mmoja wa maofisa wa polisi mara baada ya kufika eneo la tukio.
Mawakili wa Gwajima wakisalimiana na mmoja wa maofisa wa polisi mara baada ya kufika eneo la tukio.
Waandishi wa habari wakiwa eneo la tukio.
Waumini wa Gwajima wakiwa wamezunguka nyumba wa askofu wao.
Kundi la wafuasi wa Gwajima wakifika nyumbani kwake mara baada ya polisi kuondoka eneo la tukio.
Baadhi ya watu waliokuwemo ndani ya nyumba ya Gwajima wakichungulia dirishani.
Baadhi ya waumini wa Gwajima wakifuatilia kwa makini hali iliyokuwapo.
Baadhi ya waumini wakiwa mbele ya nyumba ya Gwajima.
Gari la polisi likiondoka eneo la tukio.
Hapa wakishangilia ushindi baada ya polisi kuondoka eneo la tukio.
Comments