SISI HATUMO MIONGONI MWAO WANAOPOTEA MAANA TUNAYE YESU KRISTO.

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
 
BWANA YESU atukuzwe ndugu zangu.
Karibu tujifunze ujumbe special kabisa wa neno la MUNGU.

Waebrania 10:39 '' Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu. ''

Wanaopotea ni wale wanaomkataa BWANA YESU kama Mwokozi wao.
Wanaopotea ni wale wanaokataa Wokovu wa KRISTO.
Wanaopotea ni wale ambao hawaishi maisha matakatifu ya wokovu.
Wanaopotea ni watenda dhambi wasiotaka kutubu.
Wanaopotea ni wazinzi na waasherati ambao hawana mpango wa kutubia uovu wao huo na kuuacha.
Sisi tuliookoka hatumo miongoni mwao wanaopotea maana tunamtii KRISTO na Neno lake.
 
Luka 19:10 ''Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea. ''

BWANA YESU alikuja kuokoa kile kilichopotea ambacho ni mwanadamu, lakini mwanadamu huyo akimkataa BWANA YESU ataendelea kupotea na mwisho wa waliopotea ni ziwa la moto.

Injili ya KRISTO inawahitaji wanadamu wote.
Injili ya KRISTO inaweza kuwaokoa wanadamu wote ila tu wanadamu hao wanatakiwa kuufuata uzima kwa kumpokea BWANA YESU kama BWANA na Mwokozi wao.

2 Kor 4:3-6 '' Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; ambao ndani yao mungu wa dunia hii(shetani) amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake KRISTO aliye sura yake MUNGU. Kwa maana hatujihubiri wenyewe, bali KRISTO YESU ya kuwa ni BWANA; na sisi wenyewe kuwa tu watumishi wenu kwa ajili ya YESU. Kwa kuwa MUNGU, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa MUNGU katika uso wa YESU KRISTO.''

Kama injili ni ngeni basi ni ngeni tu kwa hao wanaopotea.
Kama toba ni jambo gumu basi ni gumu tu kwa hao wanaopotea.
Kama kuacha dhambi ni haiwezekani basi haiwezekani tu kwa hao wanaopotea wasio na haja ya kutubu.
Ndugu, usikubali kupotea bali okoka na anza upya na BWANA YESU mwenye uzima wako wa milele.
Kama ulikuwa umepotea basi nakuomba geuka leo kwa kumpokea BWANA YESU nayeokoa.
Sisi tuliookoka hatumo miongoni mwao wanaopotea maana tunamtii KRISTO na Neno lake.

1 Kor 1:18 '' Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya MUNGU.''

Waliopotea ni wale wanaokataa kazi ya Mwokozi YESU pale msalabani.
Wanaopotea ni wachawi na waganga wanaotumainia kazi zao feki wakiwa hawana haja ya kutubu na kuacha dhambi.
Wanaopotea ni wale wanaopingana na Neno la MUNGU yaani Biblia.
Sisi sio miongoni mwao wanaopotea maana tunaye KRISTO YESU Mwokozi wetu..
Waliopotea ni wale walio na juhudi katika maovu na mambo ya kidunia, wakiwa hawataki wokovu wa BWANA YESU.
Sisi sio miongoni mwao wanaopotea maana sisi tunaishi maisha matakatifu katika BWANA YESU.
Wanapotea ni wale wasio mtii MUNGU.
Wanapotea ni wale Wasio na wokovu wa KRISTO.
Wanapotea ni wale Wachawi na waongo.
Wanapotea ni wale wanaoenda kwa waganga wa kienyeji.
Wanapotea ni wale wanaoabudu sanamu.
Wanapotea ni wale wanaosujudia mawe na miti.
Wanapotea ni wale waasherati wasio na haja ya kutubu.
Wanapotea ni wale wezi na majambazi.
Wanapotea ni wale watoa rushwa na wapokea rushwa wasio tubu.
Wanapotea ni wale mafisadi na walaghai.
Wanapotea ni wale Wasaliti wa ndoa zao.
Wanapotea ni wale Wasengenyaji na wachonganishi.
Wanapotea ni wale waongo na mashoga.
Wanapotea ni wale walawiti na wafiraji na wafirwaji.
Wanaopotea ni wale wanaooa mke zaidi ya mmoja.
wanaopotea ni watenda dhambi wasio na haja ya kuja kwa YESU kuokoka na kutubu ili wasamehewe.
Sisi sio miongoni mwao wanaopotea maana sisi tunaishi maisha matakatifu katika BWANA YESU.
Sisi sio miongoni mwao wanaopotea maana KRISTO ndiye mwokozi wa maisha yetu.

BWANA YESU alikuja kuokoa kile kilichopotea ambacho ni mwanadamu, lakini mwanadamu huyo akimkataa BWANA YESU ataendelea kupotea na mwisho wa waliopotea ni ziwa la moto.
Ndugu, usikubali kuwa miongoni mwao wanaopotea.
BWANA YESU anatamani aseme siku ile ya mwisho kwamba ''Karibu mtumwa mwema na Mwaminifu''
Ndugu, usikubali kushawishiwa na mwanadamu wa aina yeyote kwamba eti umwache YESU.
Kumuacha BWANA YESU ni kuuacha uzima.
Sisi tuliookoka hatumo miongoni mwao wanaopotea maana tunamtii KRISTO na Neno lake.
Zaburi 1:6 ''Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.''

Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichaka chako cha kuficha uovu wako , nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.

Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.

Comments