ILIKUWA NI SIKU NJEMA KWA JANETH KIFARU NA YOTHAM.

Mchungaji akisema kitu kabla ya tukio la kutangwazwa uchumba.
Tarehe 6 July 2014 katika kanisa la Ebeneza lililopo Mbagala, kituo kimoja baada ya mtongani ukitokea mjini  kulifanyika tukio kubwa sana na la muhimu sana katika maisha ya Janeth Kifaru na Yotham Kashimba, baada ya Yotham Kumvisha pete ya uchumba mchumba wake Janeth. 
 Tukio hilo ambalo liliibua shangwe  na vigelegele kanisani maana hakuna aliyejua tukio hilo zaidi ya wahusika na Mchungaji.

Maombezi.
Akiongea maneno machache baada ya zoezi la kuvishana pete kumalizika , Mchungaji Medadi Issa ambaye ni mchungaji kiongozi wa Ebeneza Church Mbagala alisema hiyo ni hatua nzuri sana kwa vijana hawa wa YESU na kuwataka vijana wengine kukaa katika maombi siku zote maana ahadi za MUNGU ni ndio na kweli.

Hizi hapa baadhi ya picha za tukio hilo.
 
HII NI KUMBUKUMBU NZURI KATIKA MAISHA YA YOTHAM NA JANETH



Janeth Kifaru.

Comments