JINSI KWELI YA MUNGU INAVYOMBADILISHA MTU.





BWANA YESU asifiwe.
Karibu tujifunze kweli ambayo huwaweka watu huru kutoka kwenye utumwa wa mambo mabaya.
Yohana 8:31-31  ‘’ Basi YESU akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. ‘’.
-Huwezi kuwekwa huru pasipo kweli.
-Neno la MUNGU ndio kweli.
-Neno la MUNGU huweka huru.
-Neno la MUNGU ndio kweli inayodumu milele.
-Alichokisema MUNGU ndicho neno lake.
-Neno la MUNGU ni hakika na amina.
Neno la MUNGU linayajua mawazo ya kila mwanadamu.
-Hakuna jambo ambalo linaweza kujificha mbele ya Neno la MUNGU.
Siku moja BWANA YESU na wanafunzi wake walikuwa wanatembea kutoka mji mmoja kwenda mji mwingine. Njiani YESU akaulaani mti na kuendelea na safari, walipomaliza huduma huko wakarudi, wanafunzi wake walipofika pale kwenye ule mti wakakuta ule mti uliolaaniwa umekauka kweli, ikabidi wamuulize BWANA YESU kuhusu jambo hilo. BWANA akajibu, akawaambia ‘’Mwaminini MUNGU’’ . Neno hilo la BWANA YESU sio dogo ni kubwa sana,  sio watu wote wanamwamini MUNGU, wengi wanamwamini kwa midomo yao tu lakini ikitokea jaribu kidogo tu uaminifu wao hutauona. Lakini mtu ambaye kweli imemweka huru , huyo lazima awe na imani timilifu kwa MUNGU maana kweli ya MUNGU imemweka huru.
Ndugu yangu tamani sana neno la MUNGU siku zote, tamani neno ambalo halijaghoshiwa wala kuwekewa matakwa ya binadamu ndani yake.
Watu hutenda dhambi kwa sababau kweli haimo ndani yao, kweli ni BWANA YESU.
Yohana 3:31’’Yeye ajaye kutoka juu, huyo yu juu ya yote. Yeye aliye wa dunia, asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani. Yeye ajaye kutoka mbinguni yu juu ya yote. ‘’.
-Aliyekuja kutoka juu ni BWANA YESU.
Biblia pia kuna sehemu inasema ‘’ Amebarikiwa ajaye kwa jina la BWANA’’. YESU yuko juu ya yote, ukimpata yeye umepata vyote, yeye ni kweli ya milele, yeye ni Neno la MUNGU, yeye alifanyika mwili ili atukomboe, atuokoe na atuweke huru. Neno lake hutuweka huru, jina lake hutuweka huru, Damu yake ni ulinzi kwetu. Ni faida kuu kuwa na BWANA YESU.
Ndugu yangu utakuwa huru kama tu neno la MUNGU utalipa nafasi maishani mwako.
Wala usikubali kuwa msikiaji tu wa neno la MUNGU bali uwe mtendaji wa neno.
Neno la MUNGU ni kweli ambayo inaweza kumbadilisha mtu kutoka kwenye ukahaba na kuwa mchungaji, kutoka Ujambazi na kwa Mhubiri, kutoka mchawi na kuwa Askofu, kutoka mnajimu na kuwa Mwanamaombi, kutoka kuimba nyimbo za shetani na kuimba nyimbo za injili.
Tuliruhusu tu neno la MUNGU lifanye kazi yake maishani mwetu. Kubali ndugu kubadilishwa na Neno la MUNGU.
Yohana 17:17 ‘’Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. ‘’
-Neno la MUNGU ndio kweli, sio kukimbilia miujiza tu huku neno hulitaki, bali taka neno la MUNGU na miujiza kwako itakuja.
-Miujiza haimfikishi mtu mbinguni  bali ukilitii neno la MUNGU siku zote za maisha yako, utafika mbinguni.
- Ukilikataa neno la MUNGU unakataa uzima.
-ukilikataa neno la MUNGU unakaribisha matatizo.
Yohana 1:12 ‘’ ‘’
-Ndugu zangu tumepewa uwezo wa kushinda dhambi.
- Tumepewa uwezo wa kufanyka watoto wa MUNGU.
Mtoto wa MUNGU ni Yule aliyempa BWANA YESU maisha yake.
Zaburi 125:1 ‘’Bali wote waliompokea(YESU)  aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; ‘’.
KWANINI TUNAJIFUNZA NENO LA MUNGU?
            1. Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu Neno la MUNGU huleta tabia ya uungu ndani yetu.
           2. Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu MUNGU huliangalia neno lake ili alitimize kwetu.
           3. Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu neno la MUNGU ndio mpango wa MUNGU katika maisha yetu.
           4.  Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu Neno la MUNGU ndio kweli inayodumu milele.
          5. Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu, kwa neno hilo tutapata uzima wa milele.
         6. Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu adui yetu ibilisi anaogopa neno la kweli la MUNGU kama sisi wateule tukilitumia ipasavyo.
        7. Tunajifunza neno la MUNGU kwa sababu neno hilo ni sauti ya MUNGU ya kutuongoza katika maisha yetu yote.

Ni heri kulitendea kazi neno la MUNGU.
Ni heri kuliishi neno la MUNGU.
Isaya 55:11 ‘’ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma. ‘’
 Neno la MUNGU lina mamlaka kuu.
 Neno la MUNGU ndio katiba ya watakatifu.
 Neno la MUNGU ndio chakula cha uzima war oho zetu.
Tunalihitaji neno la MUNGU siku zote za maisha yetu.

Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                     MUNGU akubariki sana .
                      Ni mimi ndugu yako
                       Peter M Mabula
                 Maisha ya Ushindi Ministry.
                           0714252292 
                     mabula1986@gmail.com
                 MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
 MUNGU Akubariki.

Comments