JOSEPHAT MWINGIRA: JINSI NILIVYOTOKEWA NA BWANA YESU: AKIWA MBINGUNI MWINGIRA ANATOLEWA VIGAMBA MACHONI NA AWEZE KUONA ROHONI.(4)

Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira




 Leo tunaendelea na sehemu ya mwisho  ya ushuhuda wa mtumishi wa MUNGU Josephat Mwingira, mbeba maono wa huduma ya Efatha yenye makanisa zaidi ya 200 hadi sasa. Kama hukusoma sehemu ya pili ambapo Malaika alikuja kumchukua Duniani na kumpeleka mbinguni FUNGUA HAPA

baada ya kutoka kuzimu, BWANA YESU alimuonyesha mambo mbalimbali ambaye tumeyaona katika sehemu ya 2 na ya 3 hapa sasa ni hitimisho na hapa kuna mambo makubwa zaidi ambayo BWANA YESU alimuonyesha Mwingira.
karibu.
                               Naelezwa siri ya mwanadamu


Baada ya kutoka sehemu ya mamalaka, BWANA YESU alinipa siri ya mwanadamu. Alinieleza kuwa, mwanadamu kama mwanadamu, ndiye mwenye uhalali juu ya dunia, na siyo shetani. MUNGU ndiye aliyempa huu uhalali. Kwa hiyo MUNGU hawezi kumiliki dunia kwa maana anajua kwamba amempetia mwanadamu, japo MUNGU andye muweza wa yote. Hivyo, mwenye uhalali wa kutumia vya duniani na dunia yenyewe ni mwandamu. Mwenye faida na dunia ni mwanadamu.

Tukiwa hapo, ndipo akanieleza juu ya KUSUDI la kuniita mimi kwamba shetani hawezi kuitumia dunia kuharibu watu na vitu vilivyomo, mpaka ampate mtu wa kumtumia. Sipofanya hivyo atakuwa amevunja sheria ya Uumbaji   ambayo inasimamiwa na MUNGU mwenyewe, MUNGU kama MUNGU anaitwa MUNGU MKUU kwa sababu YEYE ndiye Mkuu wa yote na vyote vyenye asili ya Ki-Ungu – kama Malaika na wanadamu- ambao waliumbwa ili wishi milele, lakini kwa sababu ya ‘kosa’, haitakuwa hivyo tena. Hata kwa MUNGU pia, utaratibu anaotumia, ni huo uo. Hawezi kuwa na uhuru wa kufanya kila kitu duniani cha kumpinga au kumpiga shetani, mpaka ampate mtu atakayesimama kwa ajili yake. Isaya (Isay 6:8) anasema alisikia sauti ya BWANA ikisema. “Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Ndipo BWANA YESU, pia, akaniambia “Ninataka wewe, Josephat, uende ukafanye kazi hiyo”. Nikashangaaa sana. Nikapokea UTUME kutoka kwa BWANA YESU”.

BWANA YESU,akasema,”Uhai wa mwanadamu ni wa muhimu sana kwa upande wa MUNGU duniani. Yaani, uhai wa mtu duniani, ni muhumu sana kwa MUNGU kuliko mtu huyo kufa. Uhai wa mwanadamu unamfanya MUNGU aweze kufanya kazi kubwa zaidi na kupata tukuzo zaidi duniani. Ndiyo maana, katika kitabu cha Kutoka (Kut 15:26), MUNGU anaagiza na kuahidi kuwa, “Utaisikiliza kwa bidii sauti ya BWANA, MUNGU wako, na kufanya yaioelekea mbele zake; mimi sitatia juu yako maradhi yoyote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa mimi ndimi BWANA nikuponyae”. MUNGU, hata siku moja, hafurahii mtu akifa kabla ya wakati wake au kabla ya kutimiza kusudi alilomwambia. 


                                       Majukumu niliyopewa.


Tulipotoka pale, akanionyesha eneo linguine ambalo ni ‘Makao Matakatifu’. Baadaye, tulipomaliza kuzinguka, akaniambia, “Sasa nataka urudi duniani”, maana alikuwa amekwesha nionyesha mambo mengi, pamoja nay ale yatakayofuata baada ya ‘karamu ya Mwana kondoo’. Kitu cha muhimu alichoniambia ni kwamba, alitaka mimi nirusi duniani nikajiandae kwa ajili ya kazi ambayo ilikuwa mbele yangu. Na majukumu yenyewe niliyopewa ni kama ifuatavyo:-


                                        Huduma nilizopewa
 

Akanieleza juu ya tofauti ya Huduma zile tano, zilizomo katika Kitabu cha Efeso (Efes 4:11) na katika Kitabu cha Wakorintho (1Kor 12:28). Akanieleza, na tofauti zake, na uhusiano wake, na mazingira ya utendaji kazi wake. Akaniambia, “Utawaweka watu kazini kama nitakavyokuagiza”. 


                                      huduma ya kuhamishia


Akaniambia, “Nimekupa Huduma ndani yako ya kuhamishia. “Pia, wakati huohuo, alinifanyia vitu kadhaa. Aliyashika macho yangu, akatoa vigamba bigamba na kusema, “Kuanzia sasa, utaona mambo ya Ki-Ungu. Mambo yaliyo katika ulimwengu wa roho. “Akanishika mikono na kuambatanisha na mikono yake. Alipotoa mikono yake, nikaiangalia mikono yangu nikaona damu. Akasema, “Nimeitakasa mikono yako, ili kila utakalolifanya, likafanikiwe, na kila utakayemwekea mikono, akafunguliwe,” kasha kwenye macho akaweka malaika, mmoja asimame upande huu na mwingine upande huu – walinde macho yangu usiku na mchana, ili kuweza kuonanjia ya kwenda na kitu cha kufanya kwa ajili ya BWANA, na kwa ajili watu wake wanaokuja kwa ajili ya kumjua BWANA . kasha akayagusa masikio yangu na kusema, “Kuanzia sasa, utaisikia sauti yangu kwa usahihi. “Kwenye kinywa, akanifanyia kitu cha ajabu sana! Akaweka kidole chake kinywani mwangu, akanigusa na kusema, “Kuanzia sasa Neno limetakaswa kinywani mwako”.

Halafu akanishika miguu yangu katika sehemu ya magoti na akasema, “Umetiwa nguvu miguuni na hata kwenye kiuno” akaongeza kusema, “Utafanya kazi ambayo wengie hawajawahi kufanya”. Baadaye akasema, “Kuanzia sasa, nimeweka mamlaka juu yako, na nguvu na uwezo.” Akaniambia maneno mengi ya kunitamkia kwamba amenipa Huduma ya kuhamishia ya ‘Kitume’ na ‘Kinabii’. Akasema, “Katika utume wako, mwangalie sana Paulo alivyopita kimamlaka, itafanana na hilo. Katika Unabii, angalia Isaya alivyotabiri. Utatabiri mbambo yajayo, mambo ambayo hayajawahi kuwepo bado, wala hayajawahi kutokea, wala hakuna aluewahi kuyatamka katika kizazi chako na katika jamii yako, na yote yatatimia”. Akaniambia, “Uteweza kuwahudumia Mitume, Manabii na wenye huduma zingine zote, kuwaweka kwenye nafasi zao”. Katika hilo, akaniambia, “Nimmekupa upako wa kuhamishia ili wengine nao waweze kupokea”. Akasema, “Ni wachache sana ninaowapa upako hii, kwa kuwa siyo wengi wana uwezo wa kutumia”. Akaongeza kusema, lakini utakwenda kufanya kitu ambacho wengine hawajawahi kufanya”. Akaendelea kusema, “Utakwenda kuweka nidhamu ya Ki-roho, ambayo italifanya kanisa langu likue kwa kasi na kumshinda shetani. Nidhamu ya Ki-roho ni pamoja na utendaji na utekelezaji”. Akaanza kunifafanulia kazi ya zile Huduma nitakazokwenda kuzifanya. 



                                   Huduma za uponyaji



Katika Huduma ya uponyaji, akanifundisha namna ya magonjwa yanavyokamata watu, na kutesa, na kadhalika. Akasema, “Kila ugonjwa una chanzo , yaani, una asili yake”. Kwa hiyo, akawa ananieleza asili ya kila ugonjwa. Nikauliza, “Sasa, mbambo gani yanasababisha ugojwa gani?” YEYE akasema, “Vitu vingi”. Ndipo akanieleza ya kuwa, “MUNGU hafurahii wagojwa. Hufurahia watu wakiwa na afya njema. Maana ndiyo aliyowapa. Bali, kwa sababu ya uovu uliopo duniani, shetai amesambaza magojwa , lakini MUNGU ni mponya


 MUNGU wa mbinguni akubariki sana na asante sana kwa kusoma blog bora ya Maisha ya ushindi  na jiandae pia kwa shuhuda mbalimbali ambazo watumishi wa MUNGU watashuhudia mahali hapa pia kama na wewe una ushuhuda wa kweli ambao MUNGU wa mbinguni amekutendea muujiza fulani, karibu kwa kushuhudia hapa maana kushuhudia ni kumwaibisha shetani , nitafute kwa namba hii 0714252292 au kwa email tumia mabula1986@gmail.com.
Efatha mwenge.

Comments