SIFA 7 ZA KIJANA AMBAYE YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKE.


Peter Michael Mabula Kwenye huduma: Hapa nikiwa na wateule wa BWANA YESU huko Chalinze Mkoa wa Pwani.
BWANA YESU asifiwe ndugu.

Karibu tujifunze ujumbe huu wa tutuimarisha katika safari yetu ya kwenda mbinguni.
Nilipookoka kulikuwa na changamoto ambazo zilikuwa zinanikabili, kwanza sikujua kuomba kabisa, nilichokuwa nafanya ni kwamba, wakati wa maombi ya wote nilikuwa namuiga mchungaji anavyoomba, yaani kila neno analotamka na mimi nalitamka kwa sauti ya chini. Nilitamani sana kujua kuomba kwa muda mrefu na kwa kweli hata mwezi haukufika nikawa najua kuomba hata nusu saa bila kukoma.

Ndio nilikuwa nimezaliwa kiroho kama Biblia inavyosema katika Yohana 1:12-13( Bali wote waliompokea(YESU) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU. ).

Baada ya kuzaliwa mara ya pili na kuwa mtoto wa MUNGU nilitakiwa kukua kiroho kwa kuzingatia mafundisho kanisani. Namshukuru MUNGU nilifaulu kwa hilo la kuhudhuria mafundisho,  Siku kadhaa baadae ROHO MTAKATIFU alisema nami kwa njia ya andiko, nikasikia sauti ikisema ‘’Mtu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo kwa MUNGU’’ Nikatambua kwamba natakiwa kufunga, kweli kesho yake nikaanza kufunga na kuomba.

Zilikua ni hatua za kuukuliwa Wokovu.

Kama kimwili kuna kukua kuanzia mtoto mchanga, mtoto, kijana, mtu mzima na mzee, hata kiroho ni hivyo hivyo ila kwa sasa sijui kama nimefikia umri gani kiroho ila nauhakika sio mtoto mchanga wala mtoto kiroho.

Nimekueleza mambo hayo kunihusu mimi huku nikiamini kabisa kwamba hata wewe uliyeokoka kuna mapito uliyopitia katika kuukulia wokovu. Maombolezo 3:27 ''Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake.''

Nira inayozungumzwa hapa ni kumpokea BWANA YESU na kujifunga nira yake ambayo ni laini, Ni vema sana kuokoka ukiwa kijana , sio kuwa na mawazo ya kuokoka ukiwa mzee huku huna uhakika hata asilimia 1 kama utafika uzeeni.

Ndugu ulifanya vyema sana kumpokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako. Baada ya kuwa ni mzima kiroho yaani wewe huwezi kupeperusha na upepo wa kumwacha KRISTO mwenye uzima wako wa milele, Huwezi kuyumbishwa na mafundisho potofu au mafundisha manyonge.

Unaenenda kwa roho wala hauzitazamii tamaa  za mwili.

Kwa kuzingatia hayo yote juu, unafanya vyema sana lakini hapa kuna mambo 7 ya kuzingatia na ya muhimu sana kwako ili tu tumpendeze MUNGU wetu na kuenenda vizuri katika Wokovu wako ambao ni wa thamani sana.

Nazungumzia SIFA 7 ZA KIJANA ALIYEOKOKA.

Vijana ndilo kundi ambalo linawindwa sana na shetani na wachawi kwa sababu umri huo ndio umri wa kuchagua maisha ya kuishi, shetani anajaribu kwa kila mbinu ili tu kijana achague kumtumikia shetani na sio MUNGU aliye hai. Vijana tunatakiwa tuwe Macho sana na tusikubali kuamua kuishi maisha yaliyo nje na KRISTO YESU.

Biblia katika 1 Yohana 2:14 Inasema ‘’ Vijana tuna NGUVU, Neno la MUNGU liko ndani yetu na TUMEMSHINDA shetani.

Vijana wakiamua kumshinda shetani , hakika wanamshinda maana wana nguvu, hata wakisema watembee kilomita 20 kwenda kwenye maombi wanaweza maana wana nguvu.

Vijana waliookoka wanatakiwa Neno la MUNGU liwe ndani yao ili wasiyumbishe na dhambi na kila cha shetani.

Tumemshinda shetani na tukiamua kumshinda tutamshinda siku zote, jambo la kufanya ni kuhudhuria mafundisho kanisani , kuwa mwana maombi, kukisoma na kulitafakari neno kila mara, Kumtii MUNGU, na kufanya kazi ya MUNGU.
SIFA 7 ZA KILA KIJANA ALIYEOKOKA.
KILA KIJANA ALIYEOKOKA LAZIMA AWE NA.
                                    1.  UTII.

Kutii ni kitendo cha kuyapokea maagizo na kuyatekeleza. 1 Petro 5:5-7 ‘’ Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu MUNGU huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa MUNGU ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. ‘’

Luka 2:52 ‘’Naye YESU akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza MUNGU na wanadamu. ‘’
BWANA YESU ni mfano hai kwetu maana alipozaliwa na Mariamu aliendelea kukua kiumri lakini akimpendeza MUNGU na wanadamu pia, na hata sisi katika maisha yetu vijana tunatakiwa tumpendeza MUNGU na wanadamu pia.
  1 Samwel 2:26 ‘’ Na yule mtoto, Samweli, akazidi kukua akapata kibali kwa BWANA, na kwa watu pia. ‘’

2.  KUWA MTU WA KUTAFAKARI NENO LA MUNGU.

Yohana 8:31 ‘’Basi YESU akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. ‘’
-Kukaa kwenye neno  ni kujifunza neno na kulitafakari neno .
 Mithali 1:7 ''Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.''

 -Lazima vijana tuwe karibu na mambo ya MUNGU.

                         3.LAZIMA UWE VIELELEZO.

1        1 Timotheo 4:12 ‘’ Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi. ‘’ 

                                   4.LAZIMA UWE NA HEKIMA.

Mhubiri 4:13 ‘’ Heri kijana maskini mwenye hekima Kuliko mfalme mzee mpumbavu. ‘’ 

5. UKUMBUKE HUKUMU.

              Vijana wengi kwa sababu ya uhuru wa maamuzi hujikuta wakifanya dhambi, kumbe kuna hukumu. Mhubiri 11:9-10 ‘’ Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote MUNGU atakuleta hukumuni. Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako; kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia. ‘’


                       6.KUMKUMBUKA MUNGU.

     Mhubiri 12 :1 ‘’ Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. ‘’

                      7.KUFANYA KAZI KWA BIDII NA KUWEKA MALENGO MAZURI.

Mithali 13:16(Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa; Bali mpumbavu hueneza upumbavu. ) 

Neno la mwisho kwa leo kwa vijana ni hili.


1 Thesalonike 4:1-12 (Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika BWANA YESU; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza MUNGU, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana. Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa BWANA YESU.  Maana haya ndiyo mapenzi ya MUNGU, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;  si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua MUNGU.  Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosa katika jambo hili; kwa sababu BWANA ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.  Maana MUNGU hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.  Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali MUNGU, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
  Katika habari ya upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na MUNGU  kupendana.
 Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini twawasihi, ndugu, mzidi sana. Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;
 ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote. )

Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                     MUNGU akubariki sana .
                      Ni mimi ndugu yako
                       Peter M Mabula
                 Maisha ya Ushindi Ministry.
                           0714252292 

                     mabula1986@gmail.com
                 MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

Comments