UFUFUO NI USHINDI

Na Mchungaji Bryson Lema, Ufufuo na uzima Morogoro.
Utangulizi: Ukristo haufananishwi na dini zingine zozote. Hii ni kwa sababu, mwanzilishi wa imani hii  zaidi ya miaka 2,000 iliyopita alikufa na baada ya siku 3 akafufuka, na kaburi lake liko  wazi hadi leo hii. Alfajiri ya siku kama ya leo, Yesu Krsito aliishinda mauti, akainuka tena. Hata sasa, tatizo  ulilo  nalo si kitu  tena,  kwa sababu aliyeko ndani yako  ameinuka  tena kwa nguvu.

UFUNUO 5:5…[Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba.]…. Hii siyo saa ya kulia tena, bali ni ya ushindi. Yule Yesu Krsito waliyetaka kumzimisha, huwa haondoki moja kwa moja, bali  anapoondoka huweka ‘appointment’ ya kurudi tena. Yesu tunayemtuaminia sisi huwa hakai makaburini kama waanzilishi wa dini zingine ambao wapo  makaburini hadi leo hii.
KUTOKA 22:23..[ Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao,]… Wao walikaa ili wewe uteseke/ au uangamie/ au upotee, lakini Yesu Krsito aliiweka saa kama hii ili kuitikisa malango ya giza. Yesu Krsito alikuja ili watu wawe na uzima, tena wawe nao tele. Kumbe basi, Yesu Kristo alikuwa akinipitisha katika mafunzo ya kupokea ushindi wangu. Kwa kufufuka kwake, Yesu Kristo leo amenitangazia ushindi.
YEREMIA 31:16-17…[Bwana asema hivi,  Zuia sauti yako, usilie, na macho yako yasitoke machozi;  Maana kazi yako itapata thawabu,  nao watakuja tena toka nchi ya adui; Ndivyo asemavyo Bwana. 17 Tena liko tumaini kwa siku zako za mwisho, asema Bwana; na watoto wako watarejea hata mpaka wao wenyewe.]… Yesu Kristo amesimama ili kuwaangusha waliokupinga na kukalia njia yako. Wao wamejipanga ili maisha yako yawe ya huzuni, lakini Yesu Krsito asubuhi  na mapema leo,  ameinuka tena na kutoka kwenye lile shimo walilomchimbia. Yesu anapofufuka, hatoki hivyo hivyo, bali hutoka huko na ‘funguo’ za kukutoa wewe kwenye lile tatizo  lako. Yesu Kristo anazo funguo za maisha yangu na kazi yangu. Wao walijipanga kinyume nami lakini  yeye alipofufuka alikuja na funguo akijua kuwa lile tatizo lako lina mahali lilipofungiwa, na atazitumia hizi funguo kulifungua.
Yesu Krsito huonekana kwenye  kilio.  Usitarajie kumuona Yesu Krsito  katika vicheko vyako. Wana wa Israeli walipokaa Misri kwa miaka 430,hatimaye Yesu Kristo alishuka baada ya kukisikia kilio chao ili kuwatoa katika hali ya vilio. Yesu Ksrito amesema atayafuta machozi yako. Kwa  sababu hiyo,  hata mipango yangu iliyokuwa inaelekea kwenye mauti,imefufuka tena.
Yesu Kristo baada ya kufufuka alipewa  JINA lipitalo majina yote. Kwa sababu Yesu yu hai, huzuni yangu imekwisha. Hawezi  mtu kuuzuia Ukristo usienee hapa duniani. Hawezi mtu kuzuia Ufufuo na Uzima  kuenea duniani,kwa sababu aliyetupa hii kazi ni Yesu Kristo  mwenyewe. Hayupo wa kunizuia, kwa sababu aliyeigwa Bahari ya Shamu yu ndani yangu,  aliyemwangusha Mfalme wa Bashani yu ndani yangu, aliyewatoa wana waIsraeli  Misri kwa mkono wenye ngubu yu ndani yangu, aliewalisha wana wa Israeli mana jangawani yu ndani yangu.
ZABURI 23:4…[ 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.]… Usikate tama kamwe  kwa sababu yote unayoyaona katika maisha yako siyo mauti, bali  ni uvuli wa mauti tu.
ZABURI 23:5…[Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.]… Unapoona madui zako  wamekuzunguka, jua kuwa katikati pana mafanikio yako.  Usiuzuie upanga wako kuwaangamiza,  kwa sababu umwonapo adui ujue kuna ushindi wako. Adui hakai  kwenye  nyumba za manyasi au udongo.n umwonapo mlinzi ujue ndani ya hili jumba pana mali na vitu vya thamani. Kwenye  nyumba Za nyasi hapaka walinzi. Hapo hapo penye ulizni mkali, pana kitu unapaswa kuking’ang’ania. Kama hamna kitu, kwani nini kunuzuia?  Hata wewe uwaonapo watu wakizuia,  ujue kuna kitu. Goliath aliinuka kipindi cha Daudi na siyo cha Sulemani kwa sababu Daudi ndiye saizi yake. Sauli aliinuka wakati wa Daudi,   hakuinuka wakati  wa Sulemani kwa sababu Sulemani asingemweza. Ahabu anamtaka mtu jeuri kama Eliya. Kila adui na mbambe wake. Hata wapiganaji masumbwi, hupimwa ili wapambanishwe kwa uzito sawa. Ukiona adui ameinuka huyo ni saizi yako.
Daudi aliinuliwa kwa ajili ya Wafilisti. Sauli kuona vile akampa kazi ya kumpatia Wafilisti 50,  naye Daudi aksema hiyo si taabu, nitakuletea. Kila jaribu ulionalo maishani mwako ujue lina mlango wa kutokea. Imeandikwa, ‘mimi ni silaha ya Bwana  ya vita’, na ndiyo  maana Mungu amekuweka kwenye hili tatizo ulilo  nalo, na kwamba utumike sawasawa kumuangamiza huyo adui wako.
                          © Information Ministry (Ufufuo Na Uzima - Morogoro)

Mtaa wa Nguvu Kazi, (Minara Mitatu), Mkundi-Morogoro.

 /or

Contact our Senior Pastor:

 Dr. Godson Issa Zacharia

 (Ufufuo Na Uzima – Morogoro)

Cellphone: (+255) 757 550878 / +255 719798778

Comments