BWANA YESU
atukuzwe ndugu zangu.
Karibu
tujifunze Neno la MUNGU.
Je shoka
lijisifu juu yake anayelitumia?
Je Msumeno
ujitukuze juu ya anayeutumia?
Isaya 10:15
‘’ Je! Shoka lijisifu juu yake alitumiaye? Je! Msumeno ujitukuze juu yake
auvutaye? Ingekuwa kana kwamba bakora ingewatikisa waiinuao, au fimbo
ingemwinua yeye ambaye si mti. ‘’
-Shoka ni
silaha ambayo hutumiwa na wanadamu kukata miti au vitu mbalimbali, Mwanadamu ndiye mwenye mamlaka yote kuhusu
shoka, annaweza kulitumia shoka hilo au anaweza asilitimue.
Biblia
inatuita wateule wa MUNGU kwamba sisi ni silaha za vita vya MUNGU.
Yeremia
51:20-23 ‘’ Wewe u rungu
langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe
nitaharibu falme; na kwa wewe nitamvunja-vunja farasi, na yeye ampandaye; na
kwa wewe nitalivunja-vunja gari la vita, na yeye achukuliwaye ndani yake; na
kwa wewe nitawavunja-vunja mwanamume na mwanamke; na kwa wewe nitawavunja-vunja
mzee na mtoto; na kwa wewe nitawavunja-vunja kijana mwanamume na kijana
mwanamke; na
kwa wewe nitamvunja-vunja mchungaji na kundi lake; na kwa wewe nitamvunja-vunja
mkulima na jozi yake ya ng'ombe; na kwa wewe nitawavunja-vunja maliwali na
maakida. ‘’
-MUNGU aliwatumia waisraeli kama silaha za vita
vyake.
-Silaha ni
kama shoka ambayo inatumiwa na mtumiaji, shoka haitakiwi kujisifu au kuchukua
utukufu wa kutumika kwake bali heshima yote hupata aliyeitumia.
MUNGU
aliwatumia Waisraeli kama silaha za kuangamiza Yeriko iliyokuwa imejaa waabudu
miungu, kazi ya Waisraeli ilikuwa tu kupiga kelele na kupitia kelele hizo MUNGU
alitenda makuu na maadui za MUNGU waliangamia.
Hata wewe
ndugu unaweza leo kutumika kama silaha ya MUNGU kupitia maombi yako ya kuharibu
kila kazi ya wachawi iliyoinuka katika jamii yako. Lakini hautakiwi kujisifu
baada ya baada ya ushindi bali mpe MUNGU heshima maana ndiye aliyekushindia.
Isaya 45:9
‘’Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je!
Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono?’’
Kanisa
linapoomba kwa ajili ya amani ya nchi na MUNGU akailinda nchi sio kazi ya
kanisa kujisifu bali ni nafasi ya kanisa kumtukuza MUNGU kwa matendo yake makuu
kwa kuilinda nchi.
Mfalme Ahabu
baada ya kumwasi MUNGU, MUNGU alimtumia Nabii Eliya kama silaha za vita vyake,
kazi ya Eliya ilikuwa kutumia Mamlaka ya KRISTO iliyokuwa ndani yake kuamua na
kutomba na hakika BWANA aliwaadhibu
Israeli wote hadi mfalme wao Ahabu. Eliya hakujiinua na wala hakujisifu bali
alimtukuza MUNGU.
Je shoka
lijisifu juu yake alitumiaye?
Kama
mtumishi wa MUNGU wewe hakika umekuwa chombo na
silaha za BWANA. BWANA YESU anaweza hata akakupeleka kwa njia ya maono
kwenye kikao cha wachawi na ukaisikia mikakati yao yote, ukawaeleza kanisa na
kanisa likaomba hata mipango yote ya
wachawi yote ikafa. Ni jukumu lako uliyeona maono kumtukuza BWANA na pia ni
jukumu la kanisa kumtukuza MUNGU na sio kutumia nafasi hiyo kujisifu na
kujitangaza kama kanisa badala ya kmtangaza KRISTO YESU anayeokoa. Kanisa ni
silaha lakini BWANA ndiye anayeitumia silaha hiyo hivyo silaha haiwezi kujisifu
wala kujiinua juu yake anayeitumia.
Je msumeno ujitukuze juu yake anayeutumia?
Leo
Watumishi wengi wamefanyika silaha za
BWANA za vita na MUNGU amewashindia, MUNGU amelishindia kanisa,MUNGU
amelishindia taifa,, MUNGU amepigana mwenyewe kupitia waombaji. Je
waombaji au watumishi wa MUNGU kwanini
kujiinua?
Wakolosai
1:16-17 ‘’ Kwa kuwa katika yeye(KRISTO) vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni
na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya
enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na
kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana
katika yeye. ‘’
-Kuna watu
zamani walikuwa watumishi wa KRISTO lakini kwa baadae wamegeuka na kujiona na
wao ni sawa na KRISTO. KRISTO ni MUNGU na ndiye aliyewaumba watumishi hao
lakini ajabu watumishi hao wamejiinua na kumsahau muumba wao. Hawahitaji tena
kumtii BWANA wala kumwabudu.
Wakolosai
3:9-11 ‘’ na kuwaangaza
watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote
ilisitirika katika MUNGU aliyeviumba vitu vyote; ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya
MUNGU iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa
roho; kwa
kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika KRISTO YESU BWANA wetu.
‘’
Ndugu zangu,
je aliyeumba ajiinue juu yake aliyemuumba?
Warumi
9:20-22 ‘’ La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye MUNGU? Je! Kitu
kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi? Au mfinyanzi je!
Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha
heshima, na kimoja kiwe hakina heshima? Ni nini basi, ikiwa MUNGU kwa kutaka
kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi,
alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa
uharibifu; ‘’
Leo
makristo wa uongo wengi wanaanzisha
makanisa na dini na kujipa sifa ya KRISTO na kujipa heshima ya KRISTO wakati
wao ni wanadamu tu wa kawaida na wote wanahitaji neema ya KRISTO YESU BWANA
wetu, hawa wote wako kimyume na BWANA YESU na wanapotosha wengi.
Ndugu zangu,
jambo la kukumbuka ni hili, BWANA YESU siku moja atarudi na kuhukumu, BWANA
atamlipa kila mwanadamu sawasawa na matendo yake.
Isaya 29:16
‘’ Ninyi mnapindua mambo; Je! Mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu
kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu; au kitu
kilichoumbwa kimnene yeye aliyekiumba, Yeye hana ufahamu? ‘’
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku
nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio
kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na
utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi
kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko
KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments