Leo Jumanne Septemba 08, 2015 Askofu Gwajima anaongea na waandishi wa
habari akitoa maelezo juu ya alichokisema Dk. Slaa wakati anaongea na
waandishi wa habari pia kutoa maelezo ya uhusikaji wake kwenye tukio
husika.
Askofu Gwajima:
Mshenga ndio huwa anatumwa na mposaji, kwa hio siri zote za
mposaji anazo mshenga lakini alikosea tu kwamba, mimi kusaidia kumleta
mzee Lowassa CHADEMA ni kazi ya Mungu kwa sababu Biblia inasema heri
wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu. Kwa hio, kwa desturi
wanasiasa huwa hawaelewani mpaka wapate mtu wa kuwaleta pamoja kwa
sababu wanasiasa wanageukana muda wowote.
Kwa sababu hio mimi nilisimama pale sio kwa sababu ni bora kuliko
wengine lakini kwa sababu nilikuwa mtu sahihi kwa wakati ule kuwaleta
pamoja hawa wanasiasa wawili na wengine ili kusudi tukomboe taifa letu
kama ilivyokuwa kiu ya Dk. Slaa. Kwa hio nikawakutanisha pamoja,
nilianza na Dk. Slaa mwenyewe mpaka ikafika sasa Slaa mwenyewe akaniita
twende tukamwone mwenyekiti, tukaonana na mwenyekiti kukawa na
mazungumzo ya muda mrefu baadae wakakubaliana vizuri.
Mpaka tarehe 26/07/2015 siku ambayo mheshimiwa Edward Lowassa alikuwa
anaingia CHADEMA, kulikuwa na mkutano uliofanyika pale bahari beach
hotel, kwa hio usiku ule Mheshimiwa Lowassa alikuwa anakuja kuingia
CHADEMA kwa maana ya kuonana na kamati kuu ya CHADEMA. Na kwa sababu
mimi namediate niko katikati, ni vizuri niwepo ili nihakikishe
mheshimiwa Edward Lowassa ameingia CHADEMA kwa usahihi, hajaonewa na
hajamuonea Dk. Slaa.
Tulikwenda mpaka kamati kuu ya CHADEMA, nataka niongee kwenye platform
ya mtumishi wa Mungu kwa sababu wanasiasa wanaweza kudanganya lakini
mimi nilikwenda mpaka nikawaomba watu wa CHADEMA, mimi si mmoja ya
kamati kuu ya CHADEMA, nawaomba mniruhusu niingie kamati kuu ili
nihakikishe mheshimiwa Edward Lowassa amefika salama.
Na hili jambo ni la kawaida, mtu anaweza kusema ulikuwa mchungaji
ulifanyaje hivyo! Siku zote wanaogombea Urais, siasa, vyeo, nafasi,
power, ukurugenzi wanaanzia kwa waganga wa kienyeji, wanazindikwa,
wanachanjwa chale. Ni jambo zuri kama mtu ameanzia kwenye nyumba za
ibada. Na mtu hatakiwi aone jambo hili ni baya, ni zuri kuliko yote
badala ya kuanzia kwa waganga wa kienyeji, ameanzia kwenye nyumba ya
ibada.
Usiku ule mheshimiwa Lowassa, sasa akaingia kwenye kamati kuu na mimi
nilikuwemo ndani ya kamati kuu kuhakikisha amefika salama na alipokelewa
pale nje na Dr Slaa na Prof Baregu na mwenyekiti wa chama na watu
wengine. Mzee Lowassa akaongea, wote wakasimama kwa pamoja wakapiga
makofi, wakamkubali, wakampokea. Mkutano ukamalizika usiku kama saa sita
hivi, basi nikafurahi mimi nimeimaliza kazi ya kuwa mpatanishi kwa watu
ambao kwa nature ya kawaida wasingeelewana.
(Gwajima anaonyesha meseji aliyotumiwa na Dr. Slaa kuhusu kustaafu kwake siasa)
Gwajima: Kama Dr. Slaa anakuja aje atoke hapa akane aone mambo ya
mshenga yalivyo, watu wanashangaa Slaa anaweza kufanya haya! Si yeye ni
mama. Slaa alikuwa padri, sasa uzoefu wa ndoa hana, bora sisi wachungaji
tunaoa.
Nilimpa maneno ya matumaini, nitamtafuta mkewe niongee nae, nilimtafuta
mkewe rose garden. Nilianza mimi kumbembeleza amruhusu baba aendelee na
hayo maelezo nimeyarekodi na mimi ni mtu wa kurekodi. Alisema
ameshawaambia watu yeye atakuwa first lady, siku iliyofata tarehe 28,
nilimuita yule mama Kibo complex.
Tukakaa ndani ya gari yake, nilikuwa mimi na mtu mwingine, niliendelea
kurekodi tena. Ilikuwa ni siku Lowassa anapokea kadi bahari beach,
nawaonyesha hio sio kwa mumuone Slaa mbaya. Saa nane mchana akasema
nimekubali Slaa arudi aingie kazini kwa sharti mkutano wa kumpokea
Lowassa ufutwe. Nikamwambia hilo halitatokea milele.
Watu wengi sana wametumwa kuongea na yule mama, akiwemo mzee Ndesamburo
ambae alishindwa kumpata yule mama, kumbe yule mama anaongea kwa karibu
sana na mchungaji Max hivyo akampeleka Ndesa.
Mchungaji Max: Ilifika mahali chama kiliacha majukumu yote kumpata yule
mama kuongea na Ndesamburo, yule mama alisema CHADEMA wanacheza mpaka
waongee nami, alisema CHADEMA ni waongo na wanafiki, kwanini watufanya
mpaka tumekosa urais. Mpaka juzi nilikuwa nawasiliane nae lakini
maongezi yake kwa ujumla anasema kwanini wameachwa kugombea Urais, kwa
jinsi alivyokuwa anaongea nikajua hata Dokta hawezi kuchomoka.
Slaa alisema Josephine amemfungia Serena, ukweli mimi naufahamu, ishu ipo kwa mkewe, Dr tumeshampoteza.
Gwajima: Siku moja nilikuwa Korea, Slaa alisema mkewe amedondoka
amezimia, nikaomba kwenye simu mkewe akaanza kupiga kelele, nilimwambia
Dr. Slaa sijawahi kuona mambo haya. Nilikuwa namsindikiza mke wangu
kwenda London, cha kushangaza nikamkuta mke wa Dr Slaa airpot amekuja
kusindikiza, umeambiwa na nani! Akasema nimejisikia tu! Baada ya check
in, kurudi mke wa Dr. Slaa alidondoka chini, mashetani yalikuwa
yanamrudia.
Siku nyingine Slaa alinipigia simu mkewe amedondoka, haya ni mashetani,
Slaa anaongozwa na mwanamke wa aina hii. Ikulu pangekalika? Slaa si
yeye, kuna tatizo limetokea.
Slaa Serena alisema kwenye mkutano wa CHADEMA watu waliletwa na malori
na mabasi, mlioenda mjiulize ni kweli? Mtu anaesema uongo wa mchana,
anasema Gwajima anasema maaskofu wa katoliki wamepewa hela. Kanisa
katoliki ndio kanisa credible sana duniani.
Kwanini Slaa amesema! Kwanza kuwaondolea credibility, maaskofu hawa
wamemsomesha, leo maaskofu 30 anawasingizia. Kwa mtu unaemuamini Slaa
unaweza kusema anasema kweli lakini nimekuonyesha mazingira kwanini!
Anatukana maaskofu wa protestant na katoliki, nani aliemtuma! Slaa
aliulizwa unalindwa na usalama wa taifa? Alisema kweli, watu wa usalama
wanambeba kwenda Serena, Azam na Star Tv kutukana maaskofu. Maaskofu
hawaruhusiwi kujihusisha na siasa lakini ni wapiga kura, Je, atakupa
kura! Je waumini wao watakupa kura! Strategy hii imeshindikana wafikirie
nyingine. Bahati mbaya hii ilikuwa silaha yao ya mwisho.
Mababa askofu wa kanisa katoliki hawakupewa rushwa wala mimi sijapewa
rushwa, anasema nilikuwa nazunguka kwenye ndege na Lowassa. Mimi nina
ndege yangu na siombi kibali kuzungumza mtu.
Usalama wa taifa sio wa CCM, mnatafasiriwa nyie ndio mnatukana maaskofu,
usalama wa taifa mnamuharibia Magufuli, mwacheni aendelee kampeni zake
kwa amani.
Siku nitakayorudi kumjibu Slaa akinisemesha, nitasema Slaa alivyokutana
na watu wa usalama wa taifa Afrika kusini. Usalama mtapomuongoza tena
huyo mtu wenu wenu atukane maaskofu, nitawalipua na bomu na macho yenu
hamtafungua tena
Uadalifu wa Slaa
Gwajima: Alisema baba askofu lazima mtubu, najiuliza yeye ni msafi
kuliko sisi? Slaa aliacha wito ambalo ni tatizo tayari, zaidi ya kuacha
wito ukaoa! Nikija tena nitaleta watoto aliowazaa na uhusiano wa yeye
kutoka. Ukaa na mke na watoto ukatelekeza, haitoshi ukaenda kuoa mke wa
mtu mwingine. Kamili akaweka zuio mahakamani.
Slaa alisema Ridhwani nauza madawa ya kulevya, leo Slaa ndio anao
aliowasema, anaemuongoza Slaa akome na akome kabisa. Watu wa usalama
kazi yenu ni kulinda nchi iwe na amani na sio kuichafua.
Kinachosumbua ni wakati na majira, Miaka 500 kabla ya kristo kulikuwa na mtu
aliehubiri ubudha, akaijaza asia Ubudha kwa sababu yalikuwa majira yake.
Baada ya hapo, karne ya kwanza alitokea YESU KRISTO na kukutana na
upinzani wa ajabu, ukifika wakati wakasema wamemkamata.
Kweli ukiizika ina tabia ya kufufuka na ukiizika haiwezi kufa tena,
akaja kutokea Mtume Muhammad japo alipata upinzani mkubwa leo Uislam
umeenea sana. Nami niseme mfate majira, msishindane nayo. Tanzania ni
kubwa kuliko watanzania.
Comments