KUFUNGULIWA KUTOKA NDOA NA MAPEPO AU JINI MAHABA.

                                                                                               “Nami nimeona lililo na uchungu kupita mauti yaani,Mwanamke ambaye moyo wake ni mtego na tanzi na mikono yake ni kama vifungo; Yeye ampendezaye mungu atamponyoka,bali mwenye dhambi atanaswa na yeye“(Mhubiri 7:26)

Mpendwa mapepo dume na mapepo jike yapo na ni halisi.pepo mahaba dume kwa kiingereza linaitwa incubus. Pepo jike linaitwa sacubus. pepo dume linauwezo wa kulala na mwanamke kadhalika na pepo jike lina uwezo wa kulala na mwanaume katika ndoto. Mapepo mahaba yanatoka baharini au kwenye mito au kwenye maziwa.(wote niwatendakazi wa shetani asili yao kuzimu)kuna wanaume ambao wameoa katika hali halisi na pia wameoa katika ulimwengu wa roho.hivyo kunauwezekano wamtu kuwa na mwanamke katika halihalisi na kuwa na kuwa mwanamke katika ulimwengu wa roho. Solomoni anasema “Nami nimeona lililo na uchungu kupita mauti,yaani mwanamke ambaye moyo wake ni mtego na tanzi,na mikono yake nikama vifungo; yeye ampendezaye mungu atamponyoka,bali mwenye dhambi atanasw na yeye” (Mhubiri 7:26).
Andiko hili linatuonyesha picha ya utendaji kazi wa mapepo mahaba.Na haya mapepo yapo katika jinsia zote.kwahiyo ukipenda dhambi utanaswa na ukichagua kumpendeza mungu utaponyoka.uamuzi ni wako kunaswa au kuponyoka (nimeshakupa maarifa). Mungu akusaidie uponyoke ndiyo sababu nimeleta kwako samo hili iliujue dalili za mapepo mahaba na ufunguliwe kutoka katika kifungo cha ndoa za mapepo mahaba. Pepo mahaba ni pepo awezaye kumtawala mwanaume au mwanamke katika ulimwengu wa roho, pepo huyu mchafu ana madhara mengi sana mfano kuzuia kushika mimba au kuharibu mimba,au kuzuia kuoa au kuolewa (kuvunjika uchumba/ndoa) pepo mahaba hujidhihirisha katika ndoto,kwani mtu aliyenaswa na pepo mahaba huota ndoto akifanya ngono.
UTAJUAJE KAMA UNA VIFUNGO VYA KIPEPO MAHABA/JINI MAHABA?
Unaweza ukawa umeoa au hujaoa / umeolewa au hujaolewa katika hali halisi.
UNAJUAJE KWAMBA UNAHITAJI HUDUMA YA KUFUNGULIWA KUTOKA VIFUNGO VYA MAPEPO MAHABA?
Ilikujibu swali hili ngoja tuone dalili za mapepo mahaba katika maisha ya watu mbalimbali.Kwa ufahamu huu utajua kwamba unahitaji huduma ya kufunguliwa.
DALILI ZA MAPEPO MAHABA
1.Kuchoka katika ndoa – Kabla ya kuoa au kuolewa kila mtu alikuwa na shauku ya kufurahia ndoa.lakini baada ya muda mfupi wanandoa wamechokana na ndoa imekosa ladha.Wakati mwingine mwnandoa mmoja anamchoka mwenzi wake.Kama ungepewa nafasi ya kuamua kwaupya huenda usingekubali kuolewa na mwanaume huyo au kuoa mwanamke huyo. Mpendwa msomaji kama unajisikia kuchoka ndoa hiyoni dalili ya kuwepo kwa mapepo ya mahaba tafuta msaada wa huduma ya kufunguliwa
2.Kufanya tendo la ndoa au mapenzi kwenye ndoto na mtu unayemfahamu au usiyemfahamu.
3.Kuchukia kuoa au kuolewa (unajuta kama usingeolewa au usinge oa)
4.Kufanya maamuzi yasiyo sahihi wakati wa kuoa au kuolewa. Kuolewa au kuoa  mtu asiye sahihi.
5.Kuachwa na mume au mke.Kila mwanamume akikuoa baada ya muda mfupi anakuacha.Ujue unamapepo mahaba yanayofukuza wanaume katika maisha yako.Unakuta mwanamke mzuri amesoma na ana (uwezo) kazinzuri lakini anaachwa na wanaume au anatelekezwa na wachumba hapo unahitaji huduma ya fufunguliwa.
6.Kuchukia mahusiano ya kindoa na mumeo au mkeo.Wakati usiku unatembelewa na mapepomahaba.
7.Kunyonyesha watoto kwenye ndoto wakati huna mume wala mchumba /au umeolewa na huna mtoto kabisa! Ni dalili ya kifungo cha pepo mahaba.
8.Kuogesha watoto kwenye ndoto wakati hujaolewa ni dalili mapepo mahaba.
9.Kuota una familia kwenye ndoto wakati hujaolewa / au kuoa na wala huna mchumba.
10.Kuota unafanya shopping na mwanaume au mwanamke wakati hunahata mchumba.
11.Kumchukia mwenzi wako kiasi cha kutamani afe ili uoe au uolewe na mtu mwingine.
12.Kuota wanawake au wanaume wako uchi,au wewe mwenyewe kujiota ukouchi.
13.Wanandoa kuota mwanaume au mwanamke yuko katikati yenu au pembenimwa kitanda chenu wakati mmelala.
14.Mwanaume kukosa nguvu na kushindwa katika tendo la ndoa.
15.Mwanamke kupata maumivu makali sana wakati wa hedhi (maumivu makali ya tumbo)
16.Matatizo ya mfululizo ya magojwa ya kike mfano ya tumbo la uzazi,kuziba mirija ya uzazi.
17Kuotaunabakwa ndotoni.Kuharibu mimba baada ya kuota unafanya tendo la ndoa.
18.Kujutia kuoa / kuolewa bila sababu ya msingi
19.Kukosa hamu / moyo wa kuambatana na mwezi wako.Hujisikii tena kuongea na mwenzi wako wa ndoa unapenda kucheka na wanawake / wanaume wengine kuliko mwenzi wako hizi nidalili za kifungo cha pepo mahaba tafuta msaada wa kufunguliwa haraka upone!.
20.KIla wakati kuwaza kwamba ndoa itavunjika unapotazama miaka miaka mitano ,kumi huoni kudumu kwa ndoa yako hata hapo ulipo unaonakama muujiza.
21.Kukosa utoshelevu w moyo kat ika ndoa uliyonayo.
22.kama ni msichana huoni kijana yeyote aliye wahi kukusemesha kwamba atakuoa ujue maranyingine hata wachawi wanaweza wakawa wamekufunga.
24.Kupewa ahadi za kuolewa bila kutimiwza / kama hakuna anayemaanisha unahitaji huduma ya kufunguliwa.
25.Kuachwa baada ya wanaume kuujua mwili wako au kuchukiwa baada ya mwanaume kulala na wewe.
26.Kucheza na nyoka ndotoni wala hung’ati hili sijambojema ni hatari.
27.kubakwa mara kwa mara katika halihalisi.
28Kumpamimba msichana mwingine halafu unaoa mwanamke mwingine.
29.Mchumba kufariki kabla ya ndoa (kufaghafla mipango ya harusi imeandaliwa)
30.Kuachiswa kazi au biashara kufa mara baada ya kuoa au kuolewa.
31.Kupata ajalimba ya baada tu ya kuoa au kuolewa.
32.Mwenzi wako hakubaliani nawewe katika jambololote mnalopanga (anakuwa mpinzani tu!)
33.Kila mwenzi anaye kuoa au unaye muoa anakufa
34.Kuwa na uamuzi wa kutoolewa au kuoa kwa kuogopa matatizo ya ndoa (hofu ya ndoa).
35.Mwenzi kutokukujali wakatiunaumwa unajihudumia mwenyewe hadi unapona nayeye yupo hata ulalamike maumivu anaendelea na shughulizake bila kujali.
36.kupigwa mara kwa mara bila huruma na mume wako.
37.kutishiwa kufukuzwa mara kwa mara na mumewako.
38.Kupotelewa na pete ya ndoa au cheti cha ndoa ktk mazingira ya kutatanisha.
39.Kupewa pete za mapenzi na waganga wa kienyeji au wanajimu.Vua hiyo pete katika jina la yesu ni antena / agano la kuvutia mapepo katika maisha yako.
40Kujuta kuolewa au kuoa mwenzi huyo.
41.Kupanga kwamba niki rudi nyumbani tu nitapokeana na mwenzi wangu kwa furaha ghafla unawasili unaingiwa na chuki moyoni juu yake.
42.Kuchelewa kurudi nyumbani bila sababu ya msingi (Baada ya ndoa mwenzi wako anabadili tabia ghafla).
Sura yako kuonekana mzee kuliko umri wako.
43.Kutokwa damu sana au kwa muda mrefu wakati wa hedhi kukiambatana na maumivu makali (maranyingine siku zinzkuwa za mvurugiko mvurugiko).
44.Unakuwa na roho ya liwalo na liwe hujali ndoa yako hata ukishauriwa hushauriki.
45.Kutokupata mimba katika ndoa yako hata vipimo vya kidaktari vikionyesha huna tatizo au kuharibika mimba mara kwa mara.
46.kutengana kwa wana ndoa hata ingawa mnakaa nyumba mmoja (mzungu wa nne) kila mtu ana chumba chake.
47.Tumbo lako kuonekana unamimba hata watu wana kuona hivyo wakati hauna.
48.Matiti kutoa maziwa wakati huna mimba wala mtoto.
49.Kujisikia mjeuri,hasira,ukaidi kutokuelewana ktk ndoa.
50.Kuonywa na mtu ktk ndoto kwamba hutaolewa.
51.udhihirisho wa wazi wa mapepo mahaba wakati wa usiku.
52.kukumbuka mahusiano ya mapenzi na rafiki zako wa zamani wakati una mkeo / mumeo kitandani.
53.Kujichua au kujiridhisha mwenyewe bila mwenzi usiku au bafuni.
Mpendwa msomaji hizi ni dalili kadhaa ktk nyingi kama unaona hapo ikosehemu inakugusa tafuta mahala penye huduma ya kufunguliwa upone, haya mapepo machafu yana leta hata kukufanya uwe unaishiwa kila mara hata ungekuwa na pesa ya kutosha wewe mda mchache huna kitu, amani katika ndoa ni ndogo sana ni hekaheka tu!na kama kuoa au kuolewa kuna zuiwa na haya niliyo kupa mbinu jinasue ktk jina la Yesu !
Njia kubwa ni umpe Yesu maisha yako. Na usiogope hata wewe ambaye ulisha mpa Yesu maisha yako kama una dalili hizi nenda kafunguliwe sio dhambi kufunguliwa uweze kuoa / kuolewa. Na uliyeko katika ndoa ikiwa na mambo ya jinsi hii hauko salama hata kidogo kafunguliwe uweze kufurahia ndoa yako katika Jina la Yesu.
Frederick D Marandu

Comments