DHAMBI YATUPASA TUISHINDE

RAPHAEL MBOGO
Mathayo 11:7-19.
Mwanadamu kwake ni rahisi kuona na kusikia mambo yahusuyo wokovu LAKINI Mwanadamu kwake ni vigumu kuamua na kuacha mabaya na kutenda mema.
Rumi 7:15-16.
lile baya nisilolipenda ndilo nilifanyalo .kwanini? Kwa sababu bado wanadamu tuna tabia ya kuziendekeza dhambi ndiyo maana inakuwa vigumu kuiacha.
DHAMBI ikoje,na Uovu ukoje?
pengine hili linaweza kuwa swali lako.Dhambi ni roho mbaya inayokaa moyoni,ambayo ikikomaa inazaa matunda ambayo ndiyo maovu.
Uovu-This is the outcome of a sin.
uovu ni matendo ambayo yametokana na dhambi.
Kaini alionywa na Mungu akamwambia,"Dhambi iko mlangoni mwako lakini unapaswa uishinde"Mwanzo 4:7..Kaini akaiacha ile dhambi.Dhambi huwez kuizuia sababu inakuja kwa mfumo wa mawazo nayo mawazo yatakaa moyöni.unao uwezo wa kuikataa ndiyomaana Kaini aliambiwa alipaswa aishinde dhambi.Matokeo yake akamwua ndunguye Habili.huo ndio uovu sasa. ndugu nakuomba soma pia Zab.25:8-9 Tumwombe Bwana atupe macho ya rohöni, pia 2kor 4:3-4..Mungu awatangulie. by Raphael Mbogo

Comments