BWANA YESU asifiwe. namshukuru MUNGU kwa
 uzima aliotupa hadi hii leo Dec 25 tunasherekea ukumbusho wa kuja kwa 
ukombozi duniani maana hakuna uzima popote ila ni kwa YESU KRISTO 
{Yohana 14:6}. Ndio maana dunia nzima ni shangwe na furaha kwa tukio 
ambalo limetokea miaka 2012 iliyopita ambapo siku YESU anazaliwa malaika
 ambao ni jeshi la mbinguni walishangilia na kumsifu sana MUNGU{Luka 
2:8-14} na siku hiyo hiyo YESU mwanaume wa ajabu anazaliwa watu wenye 
heshima na watawala walimsujudia {Mathayo 2:11} hao walijua kuwa 
aliyezaliwa ni MFALME wa wafalme na BWANA wa mabwana. Pia YESU alizaliwa
 kwenye hori la ng'ombe ashilio la kwamba wanyama wapumzike maana hakuna
 tena sadaka ya kuteketezwa kama ilivyokuwa zamani  maana YESU ni 
dhabihu idumuyo milele ili watu wasamehe dhambi zao na kuurithi uzima wa
 milele bure kupitia yeye {Waebrania 9:12-15}.na tunasherekea christmas 
kwa kumwabudu MUNGU na kuonyesha upendo kwa wengine na kuhakisha kwamba 
 YESU anatenda jambo jipya mioyoni mwetu ili tuzidi kuishi katika neema 
yake maana kwa ajili yake na kwa neema yake alituhamisha kutoka kwa 
shetani na sasa tuko huru mbali na kuonewa na wachawi na hata nguvu 
zozote za giza. HIZI HAPA NI BAADHI TU YA SALAMA ZA KUTAKIANA HERI YA 
CHRISTMAS NA MWAKA MPYA KUTOKA KWA WATUMISHI WA MUNGU PAMOJA NA MARAFIKI
 NA WASOMAJI WA BLOG HII.
![]()  | 
| DIANA NATASHA MUHANGO | 





Comments