Jibu: Ukiwa
mtoto wa Mungu, atakujulisha kuwa huyu ndiye, Mungu ana njia maelfu za
kufunua yale Tusiyoyajua. Kinachotakiwa ni kukubali kuwa watoto wake ili
tuisikie sauti yake, kama Baba anavyoongea na Mwanae ndivyo Mungu
anavyojifunua kwa watoto wake.
Angalia
mfano wa Mcha Mungu alivyompatia Isaka Mke aliyechaguliwa na Bwana,
aliweka vigezo ambavyo Mungu alimuongoza Binti kuvitimiza, Isaka
akajitwalia Mke wa kuchaguliwa na Bwana.
Mwanzo 24:13-14 [Kwa faida yako soma kisa kizima : Mwanzo 24:1-67]
“Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, basin a iwe hivi; Yule msichana nitakayemwambia, tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili Bwana wangu”. Nina mifano Mingi ya namna hii.
Vijana
Mungu anawapenda na wakati wote anawawazia MEMA kwa siku zijazo,
mnayoyaona ni furaha sasa hivi ni mashimo marefu ya siku za usoni katika
maisha ya familia. Kubali Yesu atawale maisha yenu ili mpate kuishi
maisha ya furaha na AMANI.MUNGU akubariki sana na nakutakia maandalizi mema ya Christmas na mwaka mpya.
“Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, basin a iwe hivi; Yule msichana nitakayemwambia, tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili Bwana wangu”. Nina mifano Mingi ya namna hii.
NB: Jambo
la kusikitisha, ndoa nyingi leo ni ndoano zilizotegwa na yule Adui
ambaye ndiye mwanzilishi, hebu jiulize ni Mungu yupi anayehamasisha
NGONO kabla ya Ndoa? Na siku hizi vijana wengi wanadai ku “test” kwanza
ndipo wafunge Ndoa. Kwa hiyo wengi leo wamekuwa Mboga za kuonjwa na
mwishowe kuishia kuachwa, lakini hata wakioana kwa mtindo huo wasipotubu
na Mungu kuwasamehe, Ndoa haiwezi kuwa Salama, kwani anayeisimamia ni
ADUI bila kujali sala za wachungaji. Amri inasema USIZINI. Anayeendelea
na Dhambi Maombi yake ni Dhihaka kwa Mungu. Waebrania 6:4-6.
Comments