Jibu:    Ukiwa
 mtoto wa Mungu, atakujulisha kuwa huyu ndiye, Mungu ana njia maelfu za 
kufunua yale Tusiyoyajua. Kinachotakiwa ni kukubali kuwa watoto wake ili
 tuisikie sauti yake, kama Baba anavyoongea na Mwanae ndivyo Mungu 
anavyojifunua kwa watoto wake.
Angalia
 mfano wa Mcha Mungu alivyompatia Isaka Mke aliyechaguliwa na Bwana, 
aliweka vigezo ambavyo Mungu alimuongoza Binti kuvitimiza, Isaka 
akajitwalia Mke wa kuchaguliwa na Bwana.
Mwanzo 24:13-14 [Kwa faida yako soma kisa kizima : Mwanzo 24:1-67]
“Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, basin a iwe hivi; Yule msichana nitakayemwambia, tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili Bwana wangu”. Nina mifano Mingi ya namna hii.
Vijana
 Mungu anawapenda na wakati wote anawawazia MEMA kwa siku zijazo, 
mnayoyaona ni furaha sasa hivi ni mashimo marefu ya siku za usoni katika
 maisha ya familia. Kubali Yesu atawale maisha yenu ili mpate kuishi 
maisha ya furaha na AMANI.MUNGU akubariki sana na nakutakia maandalizi mema ya Christmas na mwaka mpya.
“Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, basin a iwe hivi; Yule msichana nitakayemwambia, tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili Bwana wangu”. Nina mifano Mingi ya namna hii.
NB: Jambo
 la kusikitisha, ndoa nyingi leo ni ndoano zilizotegwa na yule Adui 
ambaye ndiye mwanzilishi, hebu jiulize ni Mungu yupi anayehamasisha 
NGONO kabla ya Ndoa? Na siku hizi vijana wengi wanadai ku “test” kwanza 
ndipo wafunge Ndoa. Kwa hiyo wengi leo wamekuwa Mboga za kuonjwa na 
mwishowe kuishia kuachwa, lakini hata wakioana kwa mtindo huo wasipotubu
 na Mungu kuwasamehe, Ndoa haiwezi kuwa Salama, kwani anayeisimamia ni 
ADUI bila kujali sala za wachungaji. Amri inasema USIZINI. Anayeendelea 
na Dhambi Maombi yake ni Dhihaka kwa Mungu. Waebrania 6:4-6.







Comments