Kutoka 20:12{Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.}
Agizo
la kuheshimu wazazi ni kati ya Amri kumi za Mungu, tatizo la watoto na
vijana kutowatii wazazi linaendela kuwa sugu kila kunapokucha, si ajabu
kusikia mtoto anaporomosha matusi ya Nguoni kwa baba au mama yake, mgeni
akifika nyumbani utasikia mama anasema “nyie watoto mpishe mgeni akae” au “Amkia mgeni”, hiyo inaashiria nini? kwenye Mabasi utakuta Mama mja mzito amesimama huku watoto wa shule wamekaa, ni mara ngapi tunaona watoto wanafyonya watu wazima?. Wazazi wamepewa wajibu wa kuwa mawakili wa Mungu hapa duniani, hivyo ni lazima watoto watii na kuheshimu ushauri wa wazazi.
Angalia
Mifano ifuatayo ya Vijana waliokaidi Ushauri wa wazazi wao na matokeo
yake, kumbuka wazazi sio wale tu waliokuzaa ni watu wote wanaokuzidi
Umri na wenye mamlaka juu yako.
1. Kijana
mmoja alikodi vijana wa kihuni kuja kumpiga baba yake, kwa sababu
anamkataza kwenda Disko, mzee alivamiwa na kupigwa hadi mauti, hadi leo
yule kijana ni kichaa, anayekula kwenye majalala ya taka.
2. Binti
mmoja alikuwa akionywa kuwa ni hatari kukaa faragha (kukaa na mwanaume
katika chumba mkiwa wawili, au sehemu ya Giza), hata angekuwa mchumba
wako, mtazini tuu. Binti alimuona mama yake amepitwa na wakati, akaamua
kwenda kwa rafiki yake wa kiume, bila kutarajia alijikuta amezini, na
hapohapo goli likafungwa, bahati mbaya alipomuambia kijana juu ya mimba
yake, alimruka futi mia, mwisho wa yote yule dada akaamua kujiua kwa
Sumu ya panya.
Kijana! kama umeamua kutozini, usijidanganye kuwa utashinda zinaa katika mazingira ya kukaa wawili chumbani. Uliona
wapi wembe usinate kwenye Simaku vikiwa karibu? Au Ukalie jiko la Mkaa
usiungue? Mapenzi ni moto mara moja, au umeme “transformer”. Kuna sehemu ambayo ukifika akili inapotea, kwa lugha ya kigeni inaitwa (Point of no Return),
usijidanganye, wengi wamejikuta wana ukimwi, waja wazito, wameharibiwa
usichana wao bila matarajio, kuishi au kuolewa na mtu asiyemtarajia n.k.
kwa sababu ya kutozingatia ushauri huu.
3. Kufungiwa nira na wasioamini, soma, 2Korintho 6:14-15.
Hili ni tatizo sugu katika kizazi chetu, wala msije mkaiga jambo hili,
Binti mmoja mkristo aliyekuwa amekaidi ushauri na kuamua kuolewa na
Kijana wa Imani tofauti, alikutwa amefariki kwa kuwekewa sumu kwenye
chakula, na mke mwenza ambaye hakutaka mume wake amuoe, ila kutokana na
Imani ya mumewe kuoa wake wengi ilikuwa ruksa, hivyo akaoa na ndipo
ugonvi ukaanza. Tunashuhudia matatizo mengi, ikiwa ni pamoja na kuzuiwa
kuabudu kwenye imani yako, watoto kukosa misingi ya Imani, Ndoa haiwi
mwili mmoja tena kwa misingi ya Biblia, kwa sababu ya Imani, mwisho ni
kujitenga na Mungu.
Mungu akikataza jambo, anamaanisha hivyo, usifanye, ukikaidi Mungu anasema, hata Maombi au sala yako ni CHUKIZO kwake “Yeye agauzaye sikio lake asiisikie sheria, Hata sala yake ni chukizo” Mithali 28:9.
Unaweza kusema mbona naomba na ananiskia? Kumbuka hata mwizi anaomba
anapoenda kuiba na anarudi salama, unafikiri nani anayejibu maombi? Na
mwisho wake ni upi?

Comments