KUVUNJA MAAGANO

Kama ulishawahi kuwa na mahusiano na mtu yeyote, na ukafanya naye tendo la ndoa, alafu baadae ukavunja yale mahusiano hukumuoa au kuolewa naye, ujue uliingia naye kwenye agano, unawezakuta mtu ana maagano ya ndoa na watu kumi au zaidi anatembea nayo na Mungu anayafahamu. Haijalishi uliingia kwenye maagano na watu wangapi, kama ni kumi, watano, mmoja wataje mbele za Mungu na uvunje yale maagano uliyopatana nao, mmoja baada ya mwingine. Sasa shida hapa inakuwa kwamba usipofanya hivyo, lile agano na machozi ya uchungu ya yule uliyemuacha yatakuandama popote, utajikuta hata sehemu nyingine mambo yako hayaendi vizuri kumbe kilichokufunga ni maagano.Au kama ulishawahi kutoa mimba, au kumshawishi mtu atoe mimba na akatoa, ujue pia uliingia kwenye agano, unahitaji kuomba na kutubu mbele za Mungu, tena kwa kumtajia Mungu, kama ni mimba kumi sema, kama ni tano sema, kama ni moja sema, alafu vunja hilo agano na kutubu kwa damu ya Yesu. Upo hapo????

Comments