KUWA MTENDAJI WA NENO NA SIO MSIKIAJI TU WA NENO



WATU WAKIWA KATIKA SEMINA YA NENO LA MUNGU VIWANJA VYA JANGWANI
Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu: "Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji, Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia. Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, "Mwenye masikio na asikie! {Luka 8:4-8} ndugu zangu mbegu zinazozungumzwa hapa ni neno la MUNGU na linapandwa moyoni mwako ili liote na kuzaa mema yanayompendeza MUNGU. hivyo ndugu hakikisha unakuwa udongo mzuri na usikubali kupokea na neno harafu hulifanyi
kazi bali unakuwa msikiaji tu wa neno la MUNGU lakini huwezi kuishi sawasawa na neno linavyotaka na kitu hiki ni machukizo hapa BWANA YESU alikuwa akiwafundisha watu wengi ambapo alitaka wawe watendaji wa neno na sio wasikiaji tu na hata leo anatutaka mimi na wewe tuwe watendaji wa neno hebu angalia ufafanuzi wa BWANA YESU kwako na kwangu kuhusu tunavyolisikia neno ambalo MUNGU anapanga mioyoni mwetu kupitia matumishi wake "Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu. Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.'' {Luka 8:11-15}. kumbe neno tulilofundishwa na tunalofundishwa tuwe tunalifanyia kazi ila liwe ni neno la kutoka Biblia sio mtu akufundishe neno lake huku akikuambia ni neno la MUNGU ndio maana tunaambiwa zipimeni kila roho je zinatokana na MUNGU au ni mwanadamu tu kwa matakwa yake au ni shetani? . ubarikiwe sana na nakutakia siku njema ilia kumbuka kuwa mtendaji wa neno na sio msikiaji wa neno.
YESU KRISTO ANATUPENDA NA NDIO MAANA AMETUCHAGUA ILI TUURITHI UZIMA WA MILELE KUPITIA YEYE
YESU KRISTO NI MUNGU PAMOJA NASI
YESU KRISTO ANATUPENDA NA NDIO MAANA AMETUCHAGUA ILI TUURITHI UZIMA WA MILELE KUPITIA YEYE

Comments