Mathayo 19:4-6{Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe}
Nikawaida
kusikia; heri nisingeolewa au nisingeoa, na wengine hata kama hawasemi
kwa maneno lakini mioyoni wanajuta kwanini waliingia kwenye Ndoa,
wanatamani kutoka lakini hawawezi. Kitu cha kushangaza ni hiki; wakati
wengine wanatamani kutoka katika ndoa, wengi wanatamani kuingia ili na
wao wajionee. Na wengine bila aibu wanawaambia vijana "Ndoa ni ngumu
mtaiweza?". Kimsingi NDOA sio NGUMU ila wanadamu wanaingia katika NDOA
bila kuwa na Elimu ya NDOA.
Leo
hebu tuanze kuangalia kuwa, Je! ni mpango wa Mungu Ndoa ziwe na hali ya
kukatisha tamaa namna hiyo? kama sivyo, matatizo yanatoka wapi? make
utaona vijana wakati wa uchumba walikuwa wanabembelezana zaidi ya Mtoto
na Mama, wananyweshana juice huku mmoja amempakata mwenzie, akiwa
anamwangalia usoni kwa tabasamu lisilo na mfano, utafikiri wako peponi.
Unashangaa baada ya kuoana na kuishi takribani mwaka mmoja, na wengine
hata miezi mitatu haipiti, MAMBO YANAANZA KUBADILIKA TARATIBU LAKINI KWA
UHAKIKA.
Majibu
ya mikato unaanza kuyasikia, makelele na kununiana vinaanza kujitokeza,
hata kwenye uwanja wa mpira, mambo yanaanza kuharibika, AMRI kama za
jeshi zinaanza kutumika kwenye chumba cha faragha, ni "Mguu pande - Mguu sawa, nyumaaaaaa geuka! mwiliiii legeza !!!!!".
Wapendwa! sehemu za kutuliza mawazo zinageuka kuwa KARAHA!. Hali kama
hizo zinatoka wapi? na tufanye nini kuepukana na hali hizo?
Tatizo
kubwa ni kukosa elimu juu ya Ndoa na Kutomruhusu Mungu aliyemwanzilishi
wa Ndoa kutawala maisha ya wanadoa. Leo naomba uelewe jambo hili: NDOA
ni muunganiko wa WATU WAWILI WENYE MAPUNGUFU walioamua kuungana kuwa
mwili mmoja. Kwakuwa wengi wanaingia kwenye ndoa bila kujua jambo hili
wanapata shida wanapoanza kuona tabia za wapenzi wao zikibadilika. Mara
nyingi TABIA huwa hazibadiliki, ila ni Tabia za ASILI ambazo Zilikuwa
sio rahisi kuonekana wakati wa uchumba, ni Mungu peke yake aliyekuwa
anajua madhaifu hayo. Zingatia kuwa Hujaoa au hujaolewa na Malaika, kila
binadamu aliyezaliwa katika ulimwengu wa Dhambi ana Mapungufu ambayo -
Ni Mungu pekee anayeweza kuwafanya wana NDOA kuchukuliana, ndani ya
UPENDO wa KWELI unaotokana na Mungu mwenyewe.
Hesabu
ya 1 + 1 = 1, Ni ngumu kuielewa kibinadamu, hesabu hiyo ukifanya
kibinadamu lazima utatoa jibu ambalo ni 2, kwa upande wa Mungu jibu hilo
ni KOSA. Hiyo ndiyo shida Mambo ya Mungu tunataka kuyatolea Majibu kwa
kutia akili zetu, tutakwama tu. Hebu Mungu atusaidie kutupatia uwezo wa
kutambua maana ya NDOA, ili ndoa zipone. Kwa leo naishia na utangulizi
huu mfupi - Tutaendelea siku zijazo, usije ukakosa mada hizi, kwani
MUNGU yupo kwa ajili ya kutusaidia.

Comments