Mapepo hayawezi kustahimili kusikia Neno la Mungu.
Wakati fulani nilirudi nyumbani kutokea kanisani na
nikawa nasoma Maandiko. Niliinua macho na kuyaona mapepo kadhaa. Nikaanza
kumwomba Mungu anisaidie. Sikuwa nina hofu lakini nilikuwa tu sijisikii amani
kuyaona. Wakati nikiwa namwomba Mungu anisaidie, nilisikia sauti moyoni mwangu
ikisema, “Soma Maandiko.”
Nikauliza: “Nini?” Sauti ile ikarudia tena: “Soma
Maandiko.” Nilitii na nikaanza kusoma Maandiko. Lakini baada ya muda
kidogo, Mungu akaniambia: “Soma kwa
sauti.” Nikawa kama nimechanganyikiwa kidogo, lakini Mungu akarudia tena: “Soma
Maandiko kwa sauti.” Nilipoanza
kusoma Maandiko kwa sauti niliona kuwa mapepo yale yanafunika masikio yao kwa
mikono yao yenye makucha na kuanza kuhangaika kwa mateso makubwa. Hivi ndivyo
nilivyojifunza kuwa mapepo hayawezi kustahimili kusikia Neno la Mungu. Neno la
Mungu likitumika kwa imani na kweli, ni silaha kubwa dhidi ya nguvu za giza.
Tangu hapo, nimejenga tabia ya kusoma Neno la Mungu
kwa sauti. Pia nimepakua kutoka kwenye intaneti Agano Jipya la sauti (lililo
katika fomati ya MP3). Nikiwa nyumbani, karibu muda wote huwa nimefungulia
Biblia hiyo. Huwa naisikiliza nikiwa nakula, napika, najipamba, nk. Mara kadhaa
Mungu amekuwa akielekeza umakini wangu kwenye mistari ya muhimu sana na
kunieleza maana yake wakati nikiwa nakula au najiandaa kwenda kazini. Mwenzangu
mmoja aliniuliza ni rekodi ya aina gani hii ambayo huwa naisikiliza karibu saa
24 kila siku. Nilimweleza na kumshirikisha sababu zangu za kufanya hivyo,
lakini najua kuwa hakunielewa kikamilifu.
Vilevile nilipakua Agano Jipya kwa ajili ya
kompyuta yangu ya mfukoni. Kila ninapopata nafasi, huwa najaribu kusikiliza
Maandiko niwapo kazini. Mara nyingi ninapopatwa na mashambulizi ya adui nikiwa
kazini, huwa naamua kusikiliza Biblia hiyo kama njia yangu mojawapo ya
kunisaidi kushinda vita.
Pia nilijifuza kwamba mapepo huteswa sana hasa na
Kitabu cha Ufunuo, na hususani sura ya 17, 18, 19, pale ambapo Maandiko
yanazungumzia kuhusu hatima yao ya mwisho. Hayawezi kabisa kusikiliza mistari
kuhusu Babeli ulioanguka na mistari kuhusu ibilisi na manabii wake wa uongo
kutupwa kwenye ziwa la moto.

Katika majaribu ya Yesu ya siku 40 kule jangwani –
pale shetani alipomjaribu – je, Yesu alifanya nini? Alimjibu shetani kwa
kutumia mistari sahihi kutoka kwenye Neno la Mungu. Alishindana na shetani kwa
kutumia upanga wa Roho Mtakatifu, ambao ni Neno la Mungu. Shetani anamnukulia
Yesu Neno lakini si kikamilifu; anataja nusu ukweli. Ukweli nusu mara zote huwa ni uongo uliokusudiwa
kudanganya wanadamu na kupoteza makusudi ya Mungu kwa ajili ya wanadamu. Yesu
alimnukulia shetani Kweli yote kwa 100% ... na shetani hakuwa na kitu chochote cha
kushindana na mbinu ya mapambano ya Yesu. Shetani alishindwa kwa 100% kwenye
vita hivyo. Mungu hakuruhusu jambo hili liandikwe kwenye Biblia kwa bahati tu
ili kujaza nafasi. Shindana na
mashambulizi ya mapepo kwa kutumia kwa usahihi Neno la Mungu.
Lijue Neno ... Liamini Neno ... Fahamu lini pa kulitumia
kwa usahihi (usinukuu tu Neno nje ya uhalisia wa hali yako; mapepo
watakucheka!); kisha tamka Neno la Mungu kwa sauti, imba nyimbo zinazotokana na
Maandiko; omba Neno wakati wa maombi yako na kuyaambia mapepo yanayokuzunguka,
(japo huenda hutakaa uyaone) – sikiliza Neno la Mungu linapoongelewa dhidi ya
matatizo yanayokukabili, lakini kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu.
Mambo yote yanaweza kushindwa lakini haiwezekani
kwa Neno la Mungu kushindwa maana Roho Mtakatifu ndiye anayelifanya litende
kazi. Mungu hawezi kusema uongo; hivyo Neno la Mungu nalo haliwezi kuongopa.
Wanadamu hapa duniani wanaweza wasilielewe Neno la Mungu, hivyo wakalitumia
kimakosa katika hali zao, lakini hilo haliwezi kutokea kwa msaada wa Roho
Mtakatifu. Hilo kila mara hutokea kwa sababu ya nguvu za kipepo na mawazo ya kimwili
ya wanadamu ambao hawana ufunuo kamili wa Neno la Mungu, au huenda
wamelipindisha bila wao kujua, na kulifanya liseme kitu ambacho Mungu hajasema.
Kama Mungu alivyoandika: "Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu
hayatapita kamwe.” (Tazama:
Mt. 24:35; Mk 13:31; Lk 21:33). Mtu anapopokea ufunuo kamili kwamba Yesu
Kristo ndiye Neno, haishangazi basi
kwamba halitapita kamwe. ![]() | ||
BIBLIA TAKATIFU
|
Comments