NAOTA NDOTO NYEVU JE NI DHAMBI AU SIO DHAMBI?


shikamoo!! natumai u mzima wa afya, please naomba ushauri wako ni kwamba mara nyingi sana mtu unapofikia ule umri wa utu uzima yaani kuanzia miaka 14 na kuendelea uwa vijana tunapata ndoto nyevu(yaan unaota uko na msichana flani mnafanya tendo la ndoa) na unapozinduka ndoton unakuta kweli umechafuka )yaani kama umefikia mshndo) na kidini haturusiwi kuzini mpaka tutakapofunga ndoa je hii haiwezi kuwa ni mojawapo ya kuzini na ikawa inafaa kutibiwa?? na tufanyeje kuepukana nazo hizo ndoto maana inakuwa kama picha halisi?? MAJIBU


nashukuru sana ndugu kwa kunieleza jambo hilo kiukweli ni wachache sana wanaoweza kuomba ushauri kwa mambo kama hayo hivyo hongera sana mtu wa MUNGU. kuhusu swali lako ni kweli ndoto hizi hutokea sana kwa vijana wa kiume na wa kike na ukweli ni kwamba ndoto hizi zimegawanyika katika sehemu mbili {1]vitu vya uzazi mfano shahawa lazima zitoke kama zimezidi hivyo upo utaratibu wa kuviondoa mfano kamasi ikimaliza kazi yake hutoka au tongotongo lazima zitoke na mchakato huu wakati mwingine hutoka kwa njia ya ndoto na mfano kwa wanawake kwa mwezi lazima kuna uchafu unatoka baada ya yai kungoja mbegu ya kiume na kufikia hali ya kuharibika hivyo lazima yai lipasuke na kuwa uchafu na uchafu huo lazima utoke na kwa mwanaume ni hivyo shahawa zinapoongezeka sana inafikia mahali zinatoka na kwa maumbile ya mwanaume wakati mwingine hutoka kwa njia ya ndoto. wapendwa wengi hutaka kila jambo liwe la kiroho lakini mengine sio ya kiroho. [2] pia shetani naye hutaka kuharibu watu au kuwateka watu hivyo kwa sababu uasherati/uzinzi ni moja ya dhambi zinazoongoza kutendwa na wanadamu naye hutaka kutumia njia hiyo kuwanasa vijana mfano zamani kidogo kama miaka 8 imepita kipindi hicho nilikua na miaka 19 niliota nafanya mapenzi na dada mmoja na na shahawa zikatoka nyingi sana hadi kero na kesho yake nikamweleza rafiki yangu mmoja ushauri alionipa aliniambia nitafute msichana au nipige punyeto na mimi sikutafuta msichana ila nilipiga punyeto sana lakini na usiku nikaota tena sasa kama tatizo lilikuwa kutaka kupunguzwa shahawa je kwanini nimeota tena wakati shahawa zimeshatoka nyingi kiasi hicho kwa hiyo ndugu hiyo ilikuwa ujanja wa shetani aninase na alininasa maana nilitenda dhambi ya kupiga punyeto na mimi nilikua naota sana hizo ndoto hadi nilipookoka ndipo zilikoma na nikajua huyu alikua ni shetani kutaka kuninasa na alininasa kwa miaka mingi sana.Nilipookoka nilikaa zaidi ya miezi 10 bila kuota ndoto hizo na mwezi huo wa 10 nikaota kiukweli nilifunga siku mbili maombi ili kuua roho hiyo iliyonirudia lakini haikuwa roho kunirudia ila ilikuwa ni njia tu ya kuondoa uchafu uliozidi mwilini na baada ya hapo nilikaa tena kama miezi 5 nikaota tena hivyo kwa miaka kama 4 nimeota nadhani haivuki mara 6 na sikutenda dhambi kwa sababu ya hilo jambo. Hivyo ndugu hizo ndoto kama zinakutokea kwa wingi sana jua ya kwamba ni shetani hivyo mshirikishe mchungaji na wewe mwenyewe omba na hali hiyo itakoma maana hata mimi nilijishangaa sana nikawaza kila siku nakemea mapepo na yanatoka nimeombea watu wengi na MUNGU amewaponya sasa iweje jambo hili ina maana MUNGU hakunilinda na hili lakini ndio hivyo ni njia tu ya kuondoa shahawa zilizozidi lakini isiwe kila siku mimi naamini lazime iwe baada ya muda mrefu na pia kama ikikutokea jitahidi usitende dhambi maana shetani anaweza kuwatumia rafiki zako ambao wataliona tukio au utataka ushauri kwao maana zipo njia nyingi za shetani kutaka kuwanasa wateule wa MUNGU. la mwisho kama hujampatia YESU KRISTO maisha yako jua ya kuwa wachawi au majini wanaweza kukufanya wanavyotaka mfano wadada wengi nimeshiriki kuwaombea kanisani kwetu ambao walikuwa wanaingiliwa na majini kila siku na wakati anaingiliwa anajiona kama yuko dunia nyingine kumbe shetani na hila zake pia wakaka wengi wamekuwa wanafanya mapenzi na majini na haya yote wakati mwingine mhusika hudhani ni ndoto kumbe ni majini na ni tukio halisi. lakini kama umeokoka na uko vizuri kwa MUNGU wako hakuna jini wala mchawi atakayekugusa na mimi naamini shetani yuko kazini maana hata mimi kabla sijaokoka nilikuwa naota sana hizo ndoto yaani hata mara 2 kwa wiki lakini nilipookoka haikuwa hivyo na nikajua kabisa alikuwa ni shetani na malaika zake. MUNGU akubariki sana na kama una swali jingine uliza tu na kwa kile ninachofahamu nitakuambia.
 Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula

mabula1986@gmail.com

MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

 

Comments

Unknown said…
Nimeyapenda sana majibu ya mtumishi,

kuna baadhi ya mambo mengine huwa ni shetani tu anakuwa katika kutekeleza kazi zake ovu,

Ubarikiwe sana.
Peter Mabula said…
amen sana mtumishi wa MUNGU
Unknown said…
ukweli ohoo Mungu nikumbuke na mimi mwenye dhambi
Peter Mabula said…
MUNGU akubariki ndugu na kwa msaada wa MUNGU tutashinda ya dunia