shikamoo!! natumai u mzima wa afya, please naomba ushauri wako ni kwamba mara nyingi sana mtu unapofikia ule umri wa utu uzima yaani kuanzia miaka 14 na kuendelea uwa vijana tunapata ndoto nyevu(yaan unaota uko na msichana flani mnafanya tendo la ndoa) na unapozinduka ndoton unakuta kweli umechafuka )yaani kama umefikia mshndo) na kidini haturusiwi kuzini mpaka tutakapofunga ndoa je hii haiwezi kuwa ni mojawapo ya kuzini na ikawa inafaa kutibiwa?? na tufanyeje kuepukana nazo hizo ndoto maana inakuwa kama picha halisi?? MAJIBU
nashukuru
sana ndugu kwa kunieleza jambo hilo kiukweli ni wachache sana wanaoweza
kuomba ushauri kwa mambo kama hayo hivyo hongera sana mtu wa MUNGU.
kuhusu swali lako ni kweli ndoto hizi hutokea sana kwa vijana wa kiume
na wa kike na ukweli ni kwamba ndoto hizi zimegawanyika katika sehemu
mbili {1]vitu vya uzazi mfano shahawa lazima zitoke kama zimezidi hivyo
upo utaratibu wa kuviondoa mfano kamasi ikimaliza kazi yake hutoka au
tongotongo lazima zitoke na mchakato huu wakati mwingine hutoka kwa
njia ya ndoto na mfano kwa wanawake kwa mwezi lazima kuna uchafu unatoka
baada ya yai kungoja mbegu ya kiume na kufikia hali ya kuharibika hivyo
lazima yai lipasuke na kuwa uchafu na uchafu huo lazima utoke na kwa
mwanaume ni hivyo shahawa zinapoongezeka sana inafikia mahali zinatoka
na kwa maumbile ya mwanaume wakati mwingine hutoka kwa njia ya ndoto.
wapendwa wengi hutaka kila jambo liwe la kiroho lakini mengine sio ya
kiroho. [2] pia shetani naye hutaka kuharibu watu au kuwateka watu hivyo
kwa sababu uasherati/uzinzi ni moja ya dhambi zinazoongoza kutendwa na
wanadamu naye hutaka kutumia njia hiyo kuwanasa vijana mfano zamani
kidogo kama miaka 8 imepita kipindi hicho nilikua na miaka 19 niliota
nafanya mapenzi na dada mmoja na na shahawa zikatoka nyingi sana hadi
kero na kesho yake nikamweleza rafiki yangu mmoja ushauri alionipa
aliniambia nitafute msichana au nipige punyeto na mimi sikutafuta
msichana ila nilipiga punyeto sana lakini na usiku nikaota tena sasa
kama tatizo lilikuwa kutaka kupunguzwa shahawa je kwanini nimeota tena
wakati shahawa zimeshatoka nyingi kiasi hicho kwa hiyo ndugu hiyo
ilikuwa ujanja wa shetani aninase na alininasa maana nilitenda dhambi ya
kupiga punyeto na mimi nilikua naota sana hizo ndoto hadi nilipookoka
ndipo zilikoma na nikajua huyu alikua ni shetani kutaka kuninasa na
alininasa kwa miaka mingi sana.Nilipookoka nilikaa zaidi ya miezi 10
bila kuota ndoto hizo na mwezi huo wa 10 nikaota kiukweli nilifunga siku
mbili maombi ili kuua roho hiyo iliyonirudia lakini haikuwa roho
kunirudia ila ilikuwa ni njia tu ya kuondoa uchafu uliozidi mwilini na
baada ya hapo nilikaa tena kama miezi 5 nikaota tena hivyo kwa miaka
kama 4 nimeota nadhani haivuki mara 6 na sikutenda dhambi kwa sababu ya
hilo jambo. Hivyo ndugu hizo ndoto kama zinakutokea kwa wingi sana jua
ya kwamba ni shetani hivyo mshirikishe mchungaji na wewe mwenyewe omba
na hali hiyo itakoma maana hata mimi nilijishangaa sana nikawaza kila
siku nakemea mapepo na yanatoka nimeombea watu wengi na MUNGU amewaponya
sasa iweje jambo hili ina maana MUNGU hakunilinda na hili lakini ndio
hivyo ni njia tu ya kuondoa shahawa zilizozidi lakini isiwe kila siku
mimi naamini lazime iwe baada ya muda mrefu na pia kama ikikutokea
jitahidi usitende dhambi maana shetani anaweza kuwatumia rafiki zako
ambao wataliona tukio au utataka ushauri kwao maana zipo njia nyingi za
shetani kutaka kuwanasa wateule wa MUNGU. la mwisho kama hujampatia YESU
KRISTO maisha yako jua ya kuwa wachawi au majini wanaweza kukufanya
wanavyotaka mfano wadada wengi nimeshiriki kuwaombea kanisani kwetu
ambao walikuwa wanaingiliwa na majini kila siku na wakati anaingiliwa
anajiona kama yuko dunia nyingine kumbe shetani na hila zake pia wakaka
wengi wamekuwa wanafanya mapenzi na majini na haya yote wakati mwingine
mhusika hudhani ni ndoto kumbe ni majini na ni tukio halisi. lakini kama
umeokoka na uko vizuri kwa MUNGU wako hakuna jini wala mchawi
atakayekugusa na mimi naamini shetani yuko kazini maana hata mimi kabla
sijaokoka nilikuwa naota sana hizo ndoto yaani hata mara 2 kwa wiki
lakini nilipookoka haikuwa hivyo na nikajua kabisa alikuwa ni shetani na
malaika zake. MUNGU akubariki sana na kama una swali jingine uliza tu
na kwa kile ninachofahamu nitakuambia.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.


Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.


Comments
kuna baadhi ya mambo mengine huwa ni shetani tu anakuwa katika kutekeleza kazi zake ovu,
Ubarikiwe sana.