NINGEOMBA UNIANDIKIE SALA AMBAYO NITAUMIA WAKATI WA USIKU NA ASUBUHI

{Ningeomba uniandikie sara ambayo ntaitumia wakati wa usiku na asubuh kazi njema} NI SWALI LILILOULIZWA NA NDUGU MMOJA KATIKA PAGE YETU YA MAISHA YA USHINDI KATIKA FACEBOOK NA HAYA NDIO MAJIBU ALIYOJIBIWA AMBAYO YATASAIDIA NA WENGINE WANAOOMBA MAOMBI YA KUKARIRI}
asante sana kaka kwa kile ulichoniomba nikuandikie sara ya kuomba usiku au mchana.Kaka maombi halisi ambayo MUNGU anataka si yale ya kukariri bali MUNGU anataka uombe kana kwamba unamwomba rafiki yako ila katika maombi yako muda wote nakuomba zingatia yafuatayo;                                        1.katika maombi yako anza na kumshukuru MUNGU kwa ulinzi wake kwako                                                                                                              2.tubu kwa MUNGU hata kama hujui kama umetenda dhambi yeyote maana sisi wanadamu wakati mwingine huwa tunatenda dhambi pasipo kujua hivyo tubu kwanza maana Biblia inasema maombi ya mtu mwenye dhambi MUNGU hayajibu hivyo kama unataka MUNGU ajibu maombi lazima utubu kwanza                                             3.omba chochote kwa MUNGU na yeye atakujibu                                                                                                                                       4.baada ya maombi yako yoyote shukuru kwa MUNGU kwani hata huo muda wa kuomba MUNGU ndio aliyekupa. ukiomba kwa kuzingatia hivyo vipengere MUNGU lazima atakujibu maombi yako lakini lazima licha ya kufanya yote hayo lazima uwe umeshampa YESU maisha yako kwanza. kaka zingatia tu hivyo vipengere  4 yaani kushukuru,kutubu ,kupeleka mahitaji yako kwa MUNGU na kushukuru. pia kumbuka maombi yako yote omba katika jina la YESU na hitimisha katika jina la YESU. ni hayo tu kaka ubarikiwe sana na nakutakia siku njema na ukizingatia hayo lazima utaona matokeo na lazima pia uombe kwa imani pia soma mistari hii katika Biblia ili ikusaidie katika maombi yako; YOHANA 14:14, ZABURI 136:1-26,WAEBRANIA 11:1 NA WAEBRANIA 11:6.AM
HAKUNA ATAKAYEMWONA MUNGU  PASIPO UTAKATIFU HIVYO HATA KWA MAOMBI YAKO HAKIKISHA UNAOMBA UKIWA  MTAKATIFU KWANI MUNGU NI UTAKATIFU
JEHOVAH NI MUNGU ANAYEPONYA
TUKIOMBA MUNGU HUJIBU MAOMBI YETU

Comments