NITATAKASWA MIMI KATIKA HAO WANIKARIBIAO


YESU KRISTO NI NJIA, UKWELI NA UZIMA NA MTU HAENDI KWENYE UZIMA WA MILELE BILA YEYE {YOHANA 14:6]

WAUMINI WAKIWA KANISANI DPC


Walawi 10:3, Ndipo Musa akamwambia Haruni, Jambo hili ni hilo Bwana alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi katika hao wanikaribiao, nami nitatukuzwa mbele ya watu hao wote. Haruni akanyamaza kimya.

Kupitia wewe unayeamini Mungu atatakaswa na kutukuzwa, jihadhari sana katika maisha yako ya kila siku yasiwe sababu ya Mungu kudharauliwa na kutukanwa na wasioamini.
Tafuta sana kumjua Mungu zaidi na zaidi ili azidi kujidhihirisha katika maisha yako mpaka watu waseme hakika Mungu ni mkuu. Wewe ni chombo kinachosababisha Mungu atukuzwe, tumia nafasi yako vizuri, angalia maisha yako kama hayampi Mungu utukufu ubadilike. Utamkuta mtu mwingine ameokoka lakini watu wasioamini wakimwangalia wanasema, "kama kuokoka ndo huku sitakaa niokoke".
Usipende kukaa kihasara hasara katika wokovu, mwombe Mungu akupe ufahamu wa kiungu na hekima ili ufanikiwe kimwili na kiroho, hata watu wakikuona wampe Mungu utukufu.

Comments