UPENDO NA UTII KWA WANA NDOA

Waefeso 5:25{Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake}

Mara nyingi wanandoa wanapofarakana utasikia Mume anasema mke wake hamtii, na mwanamke anadai mume wake hampendi, sasa nani anatakiwa kuanza? Kutii au kupenda! Kabla sijaanza kuongea juu ya sifa za Mume mwema, nitaanza kueleza falsafa ya Maneno haya mawili “Kupenda na Kutii” yanavyohitaka kutumika katika Ndoa.

UPENDO WA MWANAUME: Upendo wa kweli kwa mwanaume juu ya mke wake, ni ule tu unaojengwa na Mungu, wengine wanasema, hauna sababu, ndio maana utakuta watu wanaulizana hivi huyu mume amempendea nini?. Adam alipatiwa mke na Mungu, alichukuwa ubavu wake akamfanya Hawa, alipopelekewa AKAMPENDA. Hivyo upendo wa kweli wa Mume kwa Mke wake, huanzishwa na Mungu, ndiyo maana Paulo anamfananisha Mwanaume, kama Kristo alivyolipenda Kanisa. Wanaume wengi siku hizi hawapendi ila wanatamani au kupenda vitu Fulani. Mfano: Wengine wanapenda Makalio bila kujua kuna ya Mchina, wengine “Figure eight”, wengine Maziwa yaliyosimama – mama akianza kunyonyesha Upendo kwisha, upendo wa namna hiyo ni wa kitambo, ndoa nyingi zinaanza na upendo huo, baada ya muda mfupi Ndoa inakuwa Karaha.
UTII WA MWANAMKE: Watu wengi kwa kutokuwa na elimu ya Biblia, wametafsiri neno hili vibaya hasa wanaume. Ukisoma biblia ya lugha ya Kiingereza na lugha zingine za asili ya waandishi wa Biblia, utii wa mke kwa mume ni tofauti na utii wa Mtoto kwa wazazi au watumishi kwa Bwana zao. Utii wa Mke kwa Mume unaitwa “SUBMIT” wakati Utii wa Mtoto au watumishi unaitwa “OBEY”. Soma biblia ya kiingereza – KJV “Waefeso 5:22, 6:1, 6:5”. Wives are supposed to SUBMIT themselves to their Husbands, while children are supposed to OBEY to their parents. Mwanamke anatakiwa KUJISALIMISHA kwa Mumewe kwa UPENDO akiamini juu ya UPENDO  wa mume wake, anakubali kuwa ubavu au msaidizi wa mumewe. Wanakuwa mwili mmoja. Ukiona mwanamke kawekewa Sheria nyumbani na anatakiwa kutii kama mtoto, huo sio mpango wa Mungu, na ndoa lazima itaishia kuwa Jela Ndogo – Jambo hili ni pan asana linahitaji hekima ya Mungu kulielewa na kulitenda.

Ukielewa falsafa hiyo, mwanaume hatadai mwanamke amtii kwanza ndipo ampende, Mungu angefanya hivyo, Kristo asingekuja kutukomboa tungali wenye dhambi, alitupenda tungali wabaya. MUME MPENDE MKEO, MLEJEZE KWA UPENDO KAMA KRISTO ANAVYOTUNDEA.

Comments