Waefeso 5:25{Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake}
UPENDO WA MWANAUME: Upendo
wa kweli kwa mwanaume juu ya mke wake, ni ule tu unaojengwa na Mungu,
wengine wanasema, hauna sababu, ndio maana utakuta watu wanaulizana hivi
huyu mume amempendea nini?. Adam alipatiwa mke na Mungu, alichukuwa
ubavu wake akamfanya Hawa, alipopelekewa AKAMPENDA. Hivyo upendo wa
kweli wa Mume kwa Mke wake, huanzishwa na Mungu, ndiyo maana Paulo
anamfananisha Mwanaume, kama Kristo alivyolipenda Kanisa. Wanaume wengi
siku hizi hawapendi ila wanatamani au kupenda vitu Fulani. Mfano:
Wengine wanapenda Makalio bila kujua kuna ya Mchina, wengine “Figure
eight”, wengine Maziwa yaliyosimama – mama akianza kunyonyesha Upendo
kwisha, upendo wa namna hiyo ni wa kitambo, ndoa nyingi zinaanza na
upendo huo, baada ya muda mfupi Ndoa inakuwa Karaha.
UTII WA MWANAMKE:
Watu wengi kwa kutokuwa na elimu ya Biblia, wametafsiri neno hili
vibaya hasa wanaume. Ukisoma biblia ya lugha ya Kiingereza na lugha
zingine za asili ya waandishi wa Biblia, utii wa mke kwa mume ni tofauti
na utii wa Mtoto kwa wazazi au watumishi kwa Bwana zao. Utii wa Mke kwa
Mume unaitwa “SUBMIT” wakati Utii wa Mtoto au watumishi unaitwa “OBEY”. Soma biblia ya kiingereza – KJV “Waefeso
5:22, 6:1, 6:5”. Wives are supposed to SUBMIT themselves to their
Husbands, while children are supposed to OBEY to their parents. Mwanamke anatakiwa KUJISALIMISHA kwa Mumewe kwa UPENDO akiamini juu ya UPENDO wa
mume wake, anakubali kuwa ubavu au msaidizi wa mumewe. Wanakuwa mwili
mmoja. Ukiona mwanamke kawekewa Sheria nyumbani na anatakiwa kutii kama
mtoto, huo sio mpango wa Mungu, na ndoa lazima itaishia kuwa Jela Ndogo –
Jambo hili ni pan asana linahitaji hekima ya Mungu kulielewa na
kulitenda.
Comments