Kumb la torati 6:6-7[Na
maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe
uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba
yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo}
Kila
kunapokucha tunashuhudia mpasuko mkubwa wa maadili kwa watoto na vijana
wetu, pamoja na baadhi ya watoto kuwa na akili za kuzaliwa, watoto
wengi wameharibikiwa na akili. Wengi ukiwaona wana uwezo mzuri, ila
akili zao zimeharibiwa na malezi. Kumbuka Mungu anasema “Kumcha Bwana ni chanzo cha Maarifa…” Mithali 1:7. Wazazi wengi tunawalaumu watoto kwa kutokuwa waadilifu, ni jambo la kawaida kusikia “Heri nisingezaa kuliko kuwa na watoto kama hawa”. Mambo yafuatayo yanachangia kuharibu akili ya watoto:
1. Wazazi
hawana Muda wa kuwafundisha watoto neno la Mungu ambalo ndilo chanzo
cha Maarifa yote ya uadilifu na kuwa na Hekima katika jamii, kuna wasomi
wengi lakini sio wa kutegemewa katika jamii “They are hopeless”. Wazazi
wengi wanakazania elimu ya kawaida, hiyo ni sawa, lakini elimu bila
Mungu ni hatari, na ndicho tunachokiona siku hizi.
2. Ugonvi wa
Wazazi na Maisha yasiyo na Amani na Upendo kati ya wazazi – Watoto
wanaathirika kisaikolojia wanapoona Baba na Mama wanagombana, hasa
wanapoona mmoja anaonewa, na mwingine kuonekana katili. Watoto
wako “very sensitive” na jambo hilo, na wakati wote wanakuwa ni “Upset
Minded”, hali hii inaathiri uwezo wao wa akili. Wazazi acheni magonvi
mbele ya watoto ni hatari.
3. Malezi
ya Mtoto yanaanzia Tumboni, hakikisheni mama akiwa mja mzito, ale
vyakula vyenye virutubisho kwa ajili ya kujenga Afya na Akili ya Mtoto. Hasira na Moyo wa huzuni kila mara huathiri mtoto tumboni. Vileo havitakiwi kabisa, vina athari kubwa kwa mtoto.
4. Kumbuka
chochote unachonena na kutenda mbele ya mtoto ndiyo elimu
unayomfundisha. Kuna watu midomo haina Breki, wanaporomosha matusi hadi
ya nguoni, ni wakali, na kila saa midomo iko juu, na tabia ya
kuwadanganya watoto kuwa huyu ni Uncle, na usiku anahamia chumba cha
baba na Mama, huo ni Uasherati na uzinifu, watoto lazima wataiga tabia
hizo, na wakiwa vija wakubwa unaanza kuwalaumu.
5. Chumba
cha kulala kiwe na faragha, wazazi wengi wanalala na watoto, na vitoto
vya siku hizi vinakomaa kabla ya wakati, utafikiri kamelala kumbe
kanajisikilizia, huku kamefumba macho kabla hakajaiba kuchungulia. Hivi
unafikiri michezo ya watoto ya Baba na mama unafikiri wanaitoa wapi? wanaigiza
hata mama anavyolia, kilio cha furaha. Kwa ujumla hayo ndiyo yanajaza
akili zao hadi wanaenda kuchora kwenye karatasi za mitihani.Wazazi
wasilale na watoto chumba kimoja, pia chumba kiwe na milango inayofaa
na dari lisiwe wazi, liwe na “sealing board”. Siku hizi nyumba za
kupanga zimekuwa changamoto kubwa kuharibu tabia za watoto na vijana.
Vyumba havina siri, Vijana na watoto hawapati usingizi usiku kwa sababu
ya starehe kutoka vyumba visivyo na faragha. Wazazi watawajibika kwa
kuharibu akili za Vijana na watoto wasipozingatia ushauri huu.
Comments