Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
EDMUND JOHN |
Edmund John ni mwanzilishi wa Huduma ya uinjilisti na maombi nyumba kwa nyumba(HUMANN) Iliyopo buguruni Malapa.
MAJARIBU YA NYOKA.
Edmund alikuwa ana desturi ya kufunga kila ijumaa,sasa sikuhiyo
alifunga na akiwa amefunga alipendelea sana kwenda sehemu yenye
utulivu,na sehemu yenyewe ilikuwa buguruni kipindi hicho kulikuwa ni
kichaka.alikaa huka akisali na kutafakari mpaka saa tisa
adhuhuri.Alipokuwa katika matafakari yake alimwona nyoka mkubwa sana
akitambaa mbele yake kuelekea upande wake wa kulia.Edmund alifikiri kuwa
madhali wakati ule wa jua kali nyoka labda anatafuta mahali penye
kivuli ili ajihifadì..basi Edmund hakushughulika na yule
nyoka,akaendelea kusali.
Kumbe,yule
nyoka hakwenda mbali,alikuwa mezunguka na kujiinua karibu na
Edmund.Baada ya muda Edmund alihisi kuwa kuna kitu au mtu amesimama
karibu naye upande wa kulia.Alifungua macho ili kuangalia,akamwona yule
nyoka amejisimamisha karibu na sikio lake huku akitoa ulimi wake.Edmund
alifumba macho akaendelea kusali.kisha akafumbua macho yake tena
akamwona bado hajaöndoka.(dalili ziliönyesha yule nyoka alitaka
chakula).
Sababu ya imani kubwa aliyokuwa nayo hakuwogopa yule
nyoka.Pale pale yalimjia mawazo ya ujasiri kumpa amri.Edmund
akaamuru,"Wewe nyoka,ondoka.usiniudhi wakati mimi naongea na Bwana
Yesu."mara yule nyoka akaanguka chini,akatambaa akaenda zake,wala
hakuonekana tena.
UMEJIFUNZA NINI?

- Get link
- X
- Other Apps
Comments