KUJUA KUNALETA USHINDI

MACJAY ZION


Moja ya siri kubwa ya mafanikio kwa mtu yoyote yule katika maisha yake ni kuwa na siri ya kujua jambo fulani,kumjua adui yako na mbinu zake katika maisha yako,kutakufanya uishi MAISHA YA USHINDI naya tofauti katika kila eneo la maisha yako.Hakuna vita vitakavyojitokeza katika maisha yako,usiinuke na ushindi.
Utashinda hali na mazingira yoyote utakayokutana nayo,utashinda katika masomo,biashara,afya,ndoa,uchumba na katika huduma uliyokuanayo,utashinda katika mambo ya kiroho na katika hali ya maisha katika siri kubwa ya ushindi huu wa kufahamu na kutambua..
Rumi 8:37"Lakini katika mambo hayo yote tunashinda,na zaidi ya kushinda,kwa yeye aliyetupenda"
Siri kubwa ya kuishi Maisha ya Ushindi ni kumjua adui yako na mbinu zake<shetani>..Kumjua Mungu na Ukuu wake ndiyo silaha tosha yakumshinda shetani nakumuharibu,Watu wanaomjua Mungu wao hutembea na Mungu katika maisha yao,hakuna siku watakua dhaifu au wanyonge bali watafanya mambo ya ajabu na mazito
Daniel 11:32b "Lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari nakutenda mambo makuu"
Ndugu yangu mpendwa,watakao shindana na wewe ,watashindana na Bwana Yesu,na ashindanae na Bwana atapondwa katika Jina la Yesu kristo..barikiwa sana.By MACJAY ZION

Comments