Ngoja leo ni mshuhudie kuhusu miujiza ya BWANA YESU: Siku 1 nimeenda kufanya maombi mlimani
Nipo peke yang kileleni mwa mlima,nikawa nasujudu,mara nikasikia sauti kama mtu
anatembea,nikajipa moyo nikisema kama ni mnyama,nyoka,mtu MUNGU
ataniokoa,sauti ikanyamaza nikamaliza kuomba niangalie kwa uwoga unajua
kibinadamu,alafu jioni sana,namwona kijana amesimama ananishangaa
kweli,nikamkaribisha tuombe,akakubali,hizo shida zake
alizonielezea,machozi yalinitoka ni MUNGU alinikutanisha naye,namhoji
kama amekuja kusali,ananiambia,anapoteza mawazo,amekata tamaa ya
maisha,embu tafakari si alikuwa amekuja kujiua yule aisee,nilimtizama
nikahema,nikampa moyo nikamwambia kama huyu MUNGU aishivyo leo ni siku
yako,aliniambia kila alichofanya afanikiwi,analaumiwa kwao,hana
kazi,anaongea machozi yanamtoka Hadi mimi machozi yalinilengalenga,nikapiga
naye magoti,nikaomba toba,Roho ananiongoza katika sala,kumbe ni mizimu ya
ukoo(babu) yani ujue watu wamekamatwa hawajijui,niliposema tu wewe
mzimu,elewa tumepiga goti,na kufunga macho,nilisikia kivumbi kama kuku
anayechinjwa,anagaragara chini,naomba huku nimefumba macho nilisikia kishindo
kama mabawa lindege likubwa likiruka hadi nikasisimuka,namalizia
amen,jamaa namkuta amezirai,namgusa aamke,hajitambui ananisalimia kwa
uwoga,kumbe hata alikuwa fahamu zake hazipo kama yupo mlimani,nikapiga
kimya,nikamwambia karibu,nipo ndo naomba ila nenda kamshukuru Mungu upo
huru sasa,yani niliteremka mlimani nasema ni nini hii,hapo nimeenda
kujiombea na mambo yangu. Nawe leo jitoe kwa wengine,umejua Mungu anakutumia usirudi nyuma,kazana uwe msaada kwa wengine katika jina la Yesu. Amen!.By David Polle
Comments