MUNGU ALIMLETA HUYU KIJANA ILI NIMWOMBEE NA APONE





Ngoja leo ni mshuhudie kuhusu miujiza ya BWANA   YESU:
Siku 1 nimeenda kufanya maombi mlimani
Nipo peke yang kileleni mwa mlima,nikawa nasujudu,mara nikasikia sauti kama mtu anatembea,nikajipa moyo nikisema kama ni mnyama,nyoka,mtu MUNGU ataniokoa,sauti ikanyamaza nikamaliza kuomba niangalie kwa uwoga unajua kibinadamu,alafu jioni sana,namwona kijana amesimama ananishangaa kweli,nikamkaribisha tuombe,akakubali,hizo shida zake alizonielezea,machozi yalinitoka ni MUNGU alinikutanisha naye,namhoji kama amekuja kusali,ananiambia,anapoteza mawazo,amekata tamaa ya maisha,embu tafakari si alikuwa amekuja kujiua yule aisee,nilimtizama nikahema,nikampa moyo nikamwambia kama huyu MUNGU  aishivyo leo ni siku yako,aliniambia kila alichofanya afanikiwi,analaumiwa kwao,hana kazi,anaongea machozi yanamtoka
Hadi mimi machozi yalinilengalenga,nikapiga naye magoti,nikaomba toba,Roho ananiongoza katika sala,kumbe ni mizimu ya ukoo(babu) yani ujue watu wamekamatwa hawajijui,niliposema  tu wewe mzimu,elewa tumepiga goti,na kufunga macho,nilisikia kivumbi kama kuku anayechinjwa,anagaragara chini,naomba huku nimefumba macho nilisikia kishindo kama mabawa lindege likubwa likiruka hadi nikasisimuka,namalizia amen,jamaa namkuta amezirai,namgusa aamke,hajitambui ananisalimia kwa uwoga,kumbe hata alikuwa fahamu zake hazipo kama yupo mlimani,nikapiga kimya,nikamwambia karibu,nipo ndo naomba ila nenda kamshukuru Mungu upo huru sasa,yani niliteremka mlimani nasema ni nini hii,hapo nimeenda kujiombea na mambo yangu.
Nawe leo jitoe kwa wengine,umejua Mungu anakutumia usirudi nyuma,kazana uwe msaada kwa wengine katika jina la Yesu. Amen!.By David Polle

Comments