Shuhuda ya kijana Eliya ambaye alikuwa akiishi na jini bila kujua..
Eliya :-
Nilikuwa
 zanzibar kibiashara na nilikuwa nafanya biashara ya kuuza computer, 
ambazo nilikuwa nazifuata huko. Nikiwa katika mapumziko  Zanzibar maeneo
 ya forodhani, na wa dada wawili wakaja wakaniambia tunahitaji kampani, 
kwakuwa nilikuwa bar. Wakiniuliza una mtu, basi nikasema hapana, basi 
wakaja na tukaanza kunywa, baada ya muda tukiendelea kunywa. Wakaniuliza
 jina langu na shughuli zangu, nami nikawatajia.
Kesho
 yake asubuhi wakati nimetoka kutafuta riziki nyuma yangu, nikashangaa 
imesimama gari, na nikawaona wadada wale wale ambao niliwaona jana yake.
 Basi waliniomba niende nao nikawambia naenda kazini, wakanisihi ninywe 
nao supu.   Basi baada ya hapo siku ile ikapita tena.
Siku
 moja nikiwa mwenge,  gari aina ya vx lilipaki karibu nami ( namna 
alitaja ila tunaziifadhi) .  Na pale akatoka yule yule binti aliyemuona 
Zanzibar na safari hii alikuwa mmoja. Nikamwambia naenda ofisini. 
Akaniambia tuingie kwenye gari na nikapanda. Na Yule binti akanipeleka 
hotelini, basi yule binti akaniambia Nina kitu cha kunieleza 
nikamshawishi aniambie. Basi akaniambia kuwa anaomba tuwe marafiki , 
basi nikamkubalia na nikaanza kumchukulia kama dada yangu. Basi 
tukaondoka na kuendelea kuwasiliana. basi baada ya siku chache nilienda 
zanzibar na Yule dada alinisaidia kutafuta mzigo na badala ya kukaa siku
 tano akakaa siku tatu........
.......ameruka baadhi ya matukio kwaajili ya muda  kuwa mdogo.....
Nilikuwa
 msaada kwake kwa kipindi cha mwanzo, lakini baada ya muda, Mimi ndio 
nikaonekana ndiye ninaye hitaji msaada, kwa kuwa alikuwa na hela ambazo 
awali hakujidhihirisha.. Mwanzoni alikuwa Kama mtu asiye na hela.. Akawa
 ananipa hela siku baada ya siku. Basi nikafanikiwa kujenga nyumba mbili
 mlandizi, na baada ya hapo nilishangaa alikuwa anaendelea kunipa pesa, 
 mwanzoni alinipa laki 7 lakini ilifikia kipindi ananipa hadi sh. 
Milioni 40.. Na bila kujua anatoa wapi kwakuwa hakuniambia anafanya kazi
 gani. Na hapo huyo msichana akanipa gari, alinipa vitu vingi. Na baada 
ya muda mazoea yakazidi basi nikamshirikisha kuwa kama inawezekana tuwe 
pamoja kama mtu na mchumba wake. Alikubali na kwa wakati huo nilikuwa 
sijui anapoishi na hapo nikamuuliza akaniambia baba na mama yake wako 
Nugwi Zanzibar. Basi tukakubaliana tuanze kwa kwenda kwa wazazi wangu 
ambao wapo singida, 
Tukapanaga safari , tukiwa
 safarini  kuelekea singida,  Dodoma. Akapotea ndani ya gari tulilokuwa 
tumepanda. Maana yeye alikuwa amekaa siti ya dirishani hapo , 
nikawauliza abilia wengine nao walikuwa hawajui, . Na mara wakati 
tunajadili yule binti aliyekuwa akiitwa Hawa, akarudi . basi kukawa 
kimnya kila mtu alikuwa anaogopa. tuliposhuka kwa mapunziko mzee mmoja 
ambaye alikuwa abiria akaniambia nishuke.. Maana nitawaletea matatizo. 
Nikashuka naye baada ya kunisisitiza abiria kunisisitiza.
Tukiwa
 dodoma, nikatamani nimuone mguu wake, maana niliambiwa awali kuwa jini 
anakuwa na kwato. Kwa kuwa kwa wakati huo nilikuwa sijawahi kuona miguu 
yake, tokachukua chumba pale Kilimanjaro hotel Dodoma, akatoka kidogo, 
lakini nilimvizia akirudi nione miguu yake, cha ajabubbaada ya kurudi 
Yule binti akakataa kupumzika na alikataa kuvua viatu pia. Basi kwakuwa 
alikuwa na nguvu kunizidi basi nikapanga kumkimbia, kwa kuwa nilianza 
kuingiwa na hofu, nikamwambia kwa kumdanganya kuwa naenda kununua vocha.
 Lakini nilipotaka kukimbia kufika getini nikakutana naye anatokea 
ninakoelekea. Basi ikabidi nirudi ili nimuangalie miguu asubuhi wakati 
wa kuamka, Asubuhi nilipoamka yeye akaniwekea mkono kichwani hapo 
nikalala hadi akaoga akamaliza. Nakuja kuamka baada ya masaa bila kujua 
usingizi niliupatia wapi..
Basi kesho yake 
tukapanda gari lingine la kuelekea singida. Tukiwa njiani, manyoni 
polini, ghafla akaanza kupiga kelele akisema sitaki kwenda kwenu siwezi 
kwenda, na sitaki kwenda.. Basi gari likasimama manyoni singida na kwa 
kuwa sikuwa na jinsi ikabidi nishuke na tulipofika tu akatoweka tena.  
hapo nikasema sina jinsi zaidi ya kukimbia nikakimbia umbali kama wa 
kutoka Kawe hadi ubungo kufika tu nataka nipumzike nikamuona kutokea 
mbele, na akawa ananihoji unaenda wapi.. Nikamuomba msamaha nikataka 
kwenda polisi nikakutana naye anatoka polisi. Nikawa sina jinsi zaidi ya
 kumtii tu. basi tukarudi dodoma, na hapo akainua mikono yake ikamwagika
 kitu Kama maji, akanimwagia mguu akiniambia tutaona nani baba Kati yako
 na Mimi.  Baada ya hapo    .. Yeye aka toweka
Nikiwa
 Dodoma nikaamua kutafuta kanisa.. Kwakuwa alikuwa amechukua hela zote, 
Na nikapata kanisa nikamwelezea Mch. Na akaniombea na akaniambia 
nipumzike na ghafla yule binti akatokea  hofisini nilipomuelezea Mch. , 
mchungaji akakimbia kutoka ofisi na Mimi nikakimbia kumfuata mchungaji 
basi Yule Mch. Akaniambia kamtafute pastor Max. Wa ufufuo na uzima ndiye
 atanisaidia kwa kudai Mimi nitamletea matatizo.
Basi
 walinipa nauli kidogo na nikaja dar. nilipofika dar.  Nikaenda kwenye 
nyumba yangu mikocheni nikaenda lakini sikuikuta tena eneo amabalo 
ilikuwepo awali. Na nikaamua kuja kumtafuta Mch. Max. Basi nikaja 
kanisani na nikaombewa japo nilikuwa sina imani kabisa ndani.

Comments