NIMEKUSAMEHE

MOJA YA MAMBO YANAYOUMIZA WATU WENGI NA KUACHA MAJERAHA MENGI NI VITA MFANO HAWA NI M23 HUKO WAKIWA GOMA MASHARIKI YA KONGO MAZINGIRA KAMA HAYA YA VITA HUACHA MAJERAHA MENGI SANA

Moyo wangu hauna nguvu wala nafasi ya kubeba chuki dhidi ya walionikosea katika maisha yangu yaliyopita.


 Mpendwa je wewe ni mtu ambaye kuna watu wame/likukosea kila ukikumbuka walivyokufanyia unashindwa kuwasamehe?

Kama wewe ni miongoni mwa wasioweza kusamehe ningependa kukufahamisha kuwa unapohifadhi chuki moyoni mwako anayeumia ni wewe.

Mbali ya kuwa kuhifadhi chuki kwa kushindwa kusamehe kunaweza kukuletea  maradhi kama vidonda vya tumbo,depression,magonjwa ya moyo n.k pia  ni chukizo mbele za Mungu.

Kabla hujaendelea kuwawekea vinyongo watu waliokukosea inabidi ujiulize je ni mara ngapi umemkosea Mungu lakini kila ulipotubu alikusamehe na kusahau kabisa?

Wakati mwingine mtu anaweza kuwa yeye ndiye aliyekukosea ila akawa anajitahidi kuwashawishi watu tena kwa machozi juu  LOL kuwa wewe ndiye uliyemkosea ili watu wakuone kuwa wewe ndiye mbaya.Hata watu wa aina hii pia ni wakuwasamehe na kukabidhi kila kitu kwa Mungu.
Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziye mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote." - 1 Wathesalonike 5:15

Comments