NILIVYONUSURIKA KUWA MSUKULE

Kwanza kabisa nataka nimshukuru mungu kwa kuniokoa,asingekuwa huyu yesu sijui leo ningekuwa wapi hakika mungu yupo kama huamini kupitia hili la kwangu amini yupo,mimi ni msichana naitwa N.ilikuwa siku ya alhamisi ambapo nilienda nyumbani kuwasalimia wazazi wangu nilipofika nyumbani nilimkuta dada yangu ambaye tumezaliwa pamoja amerudi nyumbani kwani yeye ni mganga hakuwepo nyumbani mda ,alinipokea kwa furaha ila sikujua nafsi yake iliwaza nini juu yangu siku ya pili nikamwambia mama ngoja twende na dada sokoni tukaondoka kama kawaida tulipofika njiani dada yangu aliniambia nimpeleke kuna mahali kuna babu mmoja nataka kwenda kumuona nikamkubalia tukaenda tulipofika huko yule babu nilishangaa akimukaribisha kwa furaha kubwa na kumwambia huyu ni ndugu yako ameshakuja akasema ndio kumbe sikujua kama kuna kitu kinaendelea kati yao ,wakatukaribisha ndani baadae nikaona dada yangu akipewa maji kidogo anywe ,nikaona amekunywa pia wakanipatia na mimi kidogo na kuniambia ukinywa maji hayo utaona wachawi wako ote nikawambia sipo tayari dada alinishawishi sana hadi nikakubali na ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kupoteza faham na kujikuta nipo kwenye chumba cha giza nikiona kama watu wamelala uchi ila hawawezi kusema nilitamani kuongea lakini faham zangu zilifubwa ila niliweza tu kuona yanayoendelea baada ya hapo nilimuona dada yangu yuko pembeni akining'onga ila yeye hakujua kama mimi faham zangu zilikuwa hazijapotea sana ndipo nikasikia sauti ndani ya hiyo nyumba kuwa unaweza kurudi au kutokurudi ufaham wako ndipo sikujua kabisa chochote ila nilichokumbuka nilikuwa na simu mkononi kuna wimbo huwa napenda ulikuwa kwenye simu mara zote huwa nausikiri ni wimbo unaosema yu mwamba yesu" nilijikuta nimeponyeza na ukaanza kulia pale pale faham zangu zikanirudia na kujitambua dada yangu aliogopa sana nikamwambia tuondoke nilipofika mjini sijui aliambiwa anipake dawa hafu aniache mjini niwe kichaa alifanya hivyo nami nilikuwa tayari nishajua yote aliponipaka tu nikasema ninahari vyote kwa damu ya yesu hakika nilimuona dada yangu akiondoka mbele yangu na kuniacha mjini nikiwa natangatanga baadaye nilipata faham nikaenda nyumbani nilipo fika nyumbani nilimkuta yupo sikusema jambo ila nilimwogopa sana na nilijikuta nikitapika vitu vyote nilivyolishwa hakika Mungu ameniokoa nampenda na nitamuhimidi siku zote amen

Comments