Skip to main content
NILIVYONUSURIKA KUWA MSUKULE
 

 
Kwanza kabisa nataka  nimshukuru mungu kwa 
kuniokoa,asingekuwa huyu yesu sijui leo ningekuwa wapi hakika mungu yupo
 kama huamini kupitia hili la kwangu amini yupo,mimi ni msichana naitwa 
N.ilikuwa siku ya alhamisi ambapo nilienda nyumbani kuwasalimia wazazi 
wangu nilipofika nyumbani nilimkuta dada yangu ambaye tumezaliwa pamoja 
amerudi nyumbani kwani yeye ni mganga hakuwepo nyumbani mda ,alinipokea 
kwa furaha ila sikujua nafsi yake iliwaza nini juu yangu siku ya pili 
nikamwambia mama ngoja twende na dada sokoni tukaondoka kama kawaida 
tulipofika njiani dada yangu aliniambia nimpeleke kuna mahali kuna babu 
mmoja nataka kwenda kumuona nikamkubalia tukaenda tulipofika huko yule 
babu nilishangaa akimukaribisha kwa furaha kubwa na kumwambia huyu ni 
ndugu yako ameshakuja akasema ndio kumbe sikujua kama kuna kitu 
kinaendelea kati yao  ,wakatukaribisha ndani baadae nikaona dada yangu 
akipewa maji kidogo anywe ,nikaona amekunywa
 pia wakanipatia na mimi kidogo na kuniambia ukinywa maji hayo utaona 
wachawi wako ote nikawambia sipo tayari dada alinishawishi sana hadi 
nikakubali na ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kupoteza faham na kujikuta 
nipo kwenye chumba cha giza nikiona kama watu wamelala uchi ila hawawezi
 kusema nilitamani kuongea lakini faham zangu zilifubwa ila niliweza tu 
kuona yanayoendelea baada ya hapo nilimuona dada yangu yuko pembeni 
akining'onga  ila yeye hakujua kama mimi faham zangu zilikuwa 
hazijapotea sana ndipo nikasikia sauti ndani ya hiyo nyumba kuwa unaweza
 kurudi au kutokurudi ufaham wako ndipo sikujua kabisa chochote ila 
nilichokumbuka nilikuwa na simu mkononi kuna wimbo huwa napenda ulikuwa 
kwenye simu mara zote huwa nausikiri ni wimbo unaosema yu mwamba yesu" 
nilijikuta nimeponyeza na ukaanza kulia pale pale faham zangu 
zikanirudia na kujitambua dada yangu aliogopa sana nikamwambia tuondoke 
nilipofika mjini sijui aliambiwa anipake dawa hafu aniache mjini niwe 
kichaa alifanya  hivyo nami nilikuwa tayari nishajua yote aliponipaka tu
 nikasema ninahari vyote kwa damu ya yesu hakika nilimuona dada yangu 
akiondoka mbele yangu na kuniacha mjini nikiwa natangatanga baadaye 
nilipata faham nikaenda nyumbani nilipo fika nyumbani nilimkuta yupo 
sikusema jambo ila nilimwogopa sana na nilijikuta nikitapika vitu vyote 
nilivyolishwa hakika Mungu ameniokoa nampenda na nitamuhimidi siku zote 
amen 
 
 
 
 
 
 
  
 
 
 
 
 
Comments