

Na katika Yohana 1:9 imeandikwa: "Tukiziungama dhambi zetu yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote."
Maombi hutusaidia ili tuweze kutakaswa, tuweze kusafishwa. Hivyo inatupasa kuungama na kutubu dhambi zetu. Tunatakiwa tujue kwamba tukikaa katika dhambi hatutahesabiwa haki mbele za Mungu. Mungu anataka kutusaidia tushinde dhambi na kuishi maisha ya utakatifu. Yak:5:16a "Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa."
2 Nyakati 7:14 "Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuacha njia zao mbaya; basi nitasikia kutoka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.".MUNGU awabariki sana


Comments