Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
Edward Tibenda
|
1.Omba kwa ajili ya ufahamu sahihi na matumizi mazuri ya kanuni za
kiroho (Yakobo1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe
dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.”).
2.Fikiri sana juu ya sura unayoisoma. Hii hujumuisha pamoja na
kushirikisha mistari mingine katika neno la Mungu katika sentensi,
sentensi katika aya na aya katika sura na sura katika vitabu vingine. (2
Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda
kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la
kweli.”).
3.Jaribu kuruhusu
ufasiri wa kiroho toka katika sura hizo. Mara nyingi neno la Mungu
hulandana hata katika mazinigra na tamaduni zake. Kwa mfano uzinzi
(tendo la ndoa nje ya ndoa) hii ni dhambi katika mazingira na hata
tamaduni za kibiblia. Kwa hiyo kusudi na wazo la Biblia uzinzi hautakiwi
(Warumi 13:8-10 “Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa
maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria. Maana kule kusema, Usizini,
Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa
katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Pendo
halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.”).
4.Uaminifu ni kipimo chako kuona kama unatoka katika maandiko na
kuhusisha upuuzi wako na maandiko. Hii huhusisha ufasiri mbaya sana
mbele za Bwana (1 Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni
mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na
udhalimu wote.”) na hata mwenendo wa kiimani (Wakolosai 2:6 “Basi kama
mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye”).
Wanafunzi itakuwa vizuri kusoma Zaburi ya 51 na wanakili mambo fulani
toka katika toba ya Daudi aliyoifanya juu ya dhambi aliyoifanya kwa
Bethsheba (2 Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika
imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo
yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.”).
5.Tembea katika neema
na Imani. Mtume Paulo anatuambia “basi kama mlivyompokea Yesu Kristo
Bwana enendeni vivyo hivyo katika yeye.” (Wakolosai 2:6). Tumepokea kwa
neema kwa njia ya imani (Waefeso 2:8-9 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema,
kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha
Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.”) na hivyo
hatuna budi kutenda matendo yanayolingana na neema tuliyoipokea.
(Waefeso 2:10 “Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende
matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende
nayo.”). MUNGU awabariki. by
Edward Tibenda
- Get link
- X
- Other Apps
Comments