Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
Mtumishi Gasper Madumla |
Tuangalie njia tatu kati ya njia nyingi zilizopo ;
* MAPAFU
Kila kiumbe hai kinahitaji hewa ya oksijeni ili kiweze kuishi. Kila
kiumbe kina namna ya kujipatia hewa hii muhimu kwa uhai. Kwa mfano
samaki huipata kutoka majini kwa kutumia matamvua, mimea hutumia majani
wakati wa usiku. Halikadhalika wanyama jamii ya mamalia hujipatia hewa
kwa kutumia mapafu. Binadamu ana mapafu mawili yaliyo ndani ya kifua.
Kwa maelezo zaidi kuhusu mapafu angalia mapafu.
Binadamu
hutumia hewa ya oksijeni katika kujitengenezea nishati kutoka katika
chakula kwa ajili ya matumizi mbalimbali mwilini. Miongoni ya matokeo ya
pambano la chakula na oksijeni pamoja na vimeng’enyo mbalimbali ndani
ya seli ya binadamu, pamoja na vitu vingine ni hewa ya carbondioxide.
Hewa hii husafirishwa katika damu mpaka ndani ya mapafu ambao huitoa nje
kama uchafu ndani ya mwili. Kiwango cha hewa ya carbondioxide
kinachotolewa nje kila mtu anapopumua kinaweza kufikia asilimia nne au
zaidi ya hewa yote inayotolewa nje. Zaidi ya hayo mapafu hutoa maji
mengi kwa namna ya mvuke.
* INI
Ini ni miongoni mwa
ogani muhimu katika mwili wa binadamu. Pia ini ni mojawapo ya viungo
vinavyohusika katika kutoa uchafu. Ini hutumika pia katika uhifadhi wa
chakula katika mwili wa binadamu. Chakula kinapofonjwa kuingia mwilini
katika utumbo mwembamba huelekea kwanza katika ini. Ini husafisha sumu
katika mwili. Kunapokuwa na uongezeko la chakula cha protini, ni jukumu
la ini kurekebisha. Uchafu unaotolewa na ini huingizwa katika mfumo wa
mmeng'enyo wa chakula na hutolewa pamoja na kinyesi.
[hariri] Mfumo wa mkojo
[hariri] Mafigo
* FIGO
Katika mwili wa binadamu mafigo yamewekwa nyuma ya tumbo; moja kwa kila
upande wa pingili za juu za kiuno. Sehemu ya juu ya mafigo imehifadhiwa
kwa jozi mbili za mbavu zinazoelea. Kila figo kwa umbo lake hufanana na
haragwe, lakini kwa ukubwa ni tofauti sana. Figo la kulia kwa kawaida
ni fupi na nene zaidi, nalo, kwa sababu ya ini, hukaa chini zaidi kuliko
figo la kushoto.
Mafigo yametengenezwa yawe mfano wa chombo
cha kuchujia maji. Kazi yake ni kuchuja maji na kutoa uchafu na vitu
vyote visivyohitajika mwilini vilivyochukuliwa na damu katika safari
zake. Maji hayo pamoja na vitu hafifu vilivyomo ndiyo mkojo. Mafigo
yameshehenezwa na vifereji vilivyonyongwanyongwa, navyo vyote huunganika
pamoja kufanya bomba lile litokalo katika kila figo na kufika mpaka
katika kibofu cha mkojo. Kutoka hukoo mkojo hutolewa nje kwa mshipa wa
kupitia mkojo na uume/uke.
UBARIKIWE.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments