AMOS OKELLO AKIWA NA MCHUNGAJI ELLY BRIGHTON BOTO WA KANISA LA KAWE PENTECOSTAL CHURH (KPC)
Mimi naitwa amos omela
nimezaliwa mkoa wa Shinyanga. kunako mwaka 2012 mwezi wa kwanza niliugua
tumbo nilienda Hospitali ya kijeshi ambayo ni Lugalo kwa ajili ya kupata
matibabu nilifanikiwa kumuona Doctor akanifanyia kipimo cha Ultrasound pia
akaniandikia nipime tena kipimo kingine kiitwacho X-ray kwa bahati mbaya naenda
kufanya hicho kipimo umeme ukakatika na baada ya muda ukarudi akanipima tema na nikagundulika na tatizo la figo imevimba
inafeli kusukuma mkojo akanipa rufaa ya kwenda Hospitali moja iitwayo Tmj kweli
nikaenda kumuona Doctar nilifanikiwa kupiga X-ray doctor alisikitika nakusema ''pole sana kijana'' basi kwa maneno yale nikaingiwa na hofu nikakata tamaa nikajua
nimekufa tayari paleple mchozi yakanitoka doctor akasema jipe moyo kuna dawa
nitakupa utumie siku kumi ila nakuomba Muombe sana MUNGU akusaidie wewe ni mtoto
mdogo sana kufanyiwa oppression ya namna hii pia dawa za kukupa hazipo maana kwa sasa hizo dawa zimeisha na ili tukuagizie India unatakiwa ulipie Tsh. 60,000
nitakupigia simu baada ya siku mbili akanipa tahadhali kuwa hali
ikibadilika niende Muhimbili akanipa barua ya zarula kweli nikafanya hivyo
.Nikaondoka pale kuelekea nyumbani siku hiyo mvua ilikuwa inanyesha na kwa bahati nzuri nilikuwa na mwamvuli maana niliiona dalili mapema,wakati nasubiri gari kuna dada mmoja akatokea pale nilipo sijui
alitokea wapi akaniomba nimkinge mwamvuli asije akaloana na mvua kweli
nikamkinga akaniuliza kwanini huna amani nikasema dada acha tu maana sikutaka
kila mtu nimuelezee matatizo yangu Yule dada hakukata tamaa kuniuliza tena mara
ya pili nikamjibu nikamwambia kuwa ni ''matatizo ya dunia dada acha tu'' akaniambia naweza kukusaidia hata kwa mchango
wa mawazo kaka mpaka nikaona kero, gari nazo haziji ikabidi ni mwambie ukweli
uliopo kuwa dada mi naumwa figo akasema usiogope utapona tu kaka unak,a wapi
hapa Dar nikamwambia nakaa kawe aniambia kuwa tamka mara kumi neno hili (KWA KUPIGWA KWAKE YESU SISI TUMEPONA) kila siku kwa siku kumi alipo maliza tu kuniambia hivo gari
likaja nikapanda sikujua kama na yeye alipanda gari au la nikakaa kusubiri
kupigiwa simu nikachukue zile dawa kweli nilipigiwa nikaenda kuchukua doctor
akanisisitiza tena kuwa muombe sana MUNGU asaidie hizi dawa kweli nikawa
najuhudi kuomba kila ninapo taka kumeza naomba kwanza MUNGU kwamba atie nguvu hizo dawa
nikisema pia 'Baba nakuomba nilifanya hivo mpaka siku kumi zikafika nikaenda kufanya checkup na niwe mzima.'' Baada ya siku 10
nikaenda Hospitali moja inaitwa IMTU sikufanikiwa kufanya vipimo vyovyote nikarudi
nyumbani kesho yake nikaenda TMJ Hospitali bahati nzuri nikamkuta Yule doctor wa
mwanzo akaniuliza vipi kijana unaendeleaje? nikamwambia afadhali kidogo na nimekuja kufanya
check up nione naendeleaje akanipima naendelea vizuri nikarudi nyumbani kesho
yake nikaenda Amana Hospitali kufanya uchunguzi tena wa uhakika hakika kweli nikafankiwa
kumuona doctor nikapima vipimo vyote naendelea vizuri nikarudi nyumbani kesho yake sikuenda popote
nikampigia simu mama yangu akiwa shinyanga nikamwambia ''mama mimi nakufa nimepewa angalizo ya
kufanyiwa oppression kutoa figo natakiwa kwenda India'' mama akasema mwanangu
nakuja nikamwambia subiri kwanza mama nitakupa jibu kesho kweli mama akanielewa
kesho ikafika asubuhi mnamo saa nne asubuhi Yule dada niliekutana nae akaja
kunijulia hali wakati simjui na najua hafahamu ninapokaa na mimi sifahamu anapokaa na kubwa zaidi lililosumbua kichwa changu ni kafikaje pale nyumbani yule dada?. akamsalimia kaka maana nilikua naishi na kaka yangu na baada ya hapo akanisalimia na mimi na akamwambia kaka ''nimekuja kumuona huyu ndugu yangu'' kaka akajua
najuana nae huyu dada hakumuuliza unanakaa wapi basi Yule dada akaaga aondoke
lakini kaka akamzuia akamwambia subiri tunywe chai Yule dada akawa amekataa basi
kaka akamruhusu aende akasema asante kwakuja kututembelea dada akasema asanteni pia
basi Yule dada nikamsindikiza huku tunaongea na akiniambia kuwa muda wa kupona kwangu umefika, huku tukitembea na mimi nikiwa mbele na yeye akiwa nyuma yangu maongezi yaliendelea na ghafla nikageuka nyuma na kukuta hakuna mtu yaani ni kana kwamba nilikua naongea na sauti tu bila mtu mwenyewe kuwepo nikajua labda amesahau kitu chake amekirudia nikasubiri
hatokei ikabidi nirudi kwenda kumuangalia nikamuuliza kaka Yule dada yuko wapi
kaka akajibu si mmeondoka wote? ndiyo tumeondoka wote nashangaa simuoni nyuma maana
nilikuwa nimetangulia mbele kidogo tu kumpeleka barabarani kwenda kupanda gari kaka
akasema huyo ni mchawi ametumwa aje akumalizie wambie nyumbani kuwa amekuja mtu
halafu kapotea gafla kaka anamaliza kusema hivo mara nikasikia sauti ikisema ''UMEPONA USIOGOPE'' na sauti hiyo ilikua kama mwangwi sauti ni ya Yule yule dada nikajua na
kaka amesikia hiyo sauti kumbe hakusikia basi toka muda huo nikajisikia nimepona
kabisa hakuna maumivu ya aina yeyote yale nikagundua Yule hakuwa mtu wa kawaida
nikakaa siku tano nikaenda kumuona doctor bingwa wa figo muhimbili namshukuru MUNGU nilikuwa sisumbuliwi kuwaona madoctor kwa muda mfupi akasema mbona figo
zako ziko safi hakuna tatizo nikajua kweli ile sauti ilifanya kweli uponyaji wa kweli
bila kuachia makovu .Basi huo ndo ushuhuda wangu wapendwa katika BWANA YESU
nawaomba tujipe moyo mtetezi yupo hata kama jaribu limeshindikanika vipi amini
neno la MUNGU na jua ya kuwa BWANA YESU alikuja hata kutusaidia katika dhiki zetu na huyu dada mimi naamini alikua ni malaika aliyetumwa na MUNGU BABA ili kuleta uponyaji kwangu maana hali ilikuwa ni mbaya sana na ajabu ambayo huwa nashangaa ni jinsi alivyoniomba tujikinge wote mwamvuli na jinsi baada ya siku kadhaa alivyofika nyumbani na hatimanye alivyopotea na baadae sauti ya ushindi aliyotoa na baada ya hapo nikawa mzima na MUNGU akubariki amina. Na hakika kuwa kwa YESU ni raha sana
AMOS
OKELLO( MWENYE BGUO NYEKUNDU ALIYESHIKA MIC ISIYO WARELESS) AKIWA NA
BAADHI YA WANAKWAYA WENZAKE WA KPC CHOIR WAKIFANYA MAZOEZI
NIKIWA NA AMOS OKELLO NJE YA KANISA LA P AG KAWE AU MAARUFU KAWE PENTECOSTAL CHURCH (KPC)
Comments