Fahamu ni mapenzi ya Mungu wewe ufanikiwe katika mambo yako yote,Ni
mapenzi ya Mungu ufanikiwe rohoni mwako na katika afya yako yote neno la Mungu linasema
hivi “ Mpenzi naomba
ufanikiwe katika mambo yako yote na kuwa na afya yako,kama vile roho yako ifanikiwavyo” (3YOHANA
1:2) Yohana alimuombea Gayo maombi ya namna hiyo,fahamu hata
wewe leo hii unatakiwa ujue kuwa ni mapenzi ya Mungu umuombe akufanikishe katika mambo yako yote,Fahamu hata
Bwana Yesu Kristo anatufundisha sisi kuwa tunatakiwa tumuombe Mungu atupe riziki zetu zote za kila namna za
siku zote, “Utupe leo
riziki yetu” (MATHAYO 6:11),Watu wengi sana wanaogopa kumuomba Mungu
awabariki au awafanikishe kweli-kweli, Sikia mpendwa unatakiwa umuombe Mungu akubariki sana,fahamu ni mapenzi
yake akubariki tatizo liko kwako humuombi ili akupe riziki zako kila siku,watu wengi wanamuomba Mungu awape
riziki zao siku za jumapili tu wanapoisema sala kuu ya Bwana! Ukisoma maneno ya Mungu
kwa makini utagundua kuwa Mungu yupo tayari kutupatia riziki zetu,ila anachokitaka ni kumuomba,sikia ikiwa
wewe humuombi ili akufanikishe katika maisha yako fahamu hutafanikiwa,Yohana alilijua jambo hilo ndio maana
akaamua kumuombea Gayo afanikiwe katika “mambo yake yote”. Fahamu Mungu anataka ufanikiwe katika mambo yako
yote,si mpango wa Mungu ufanikiwe sehemu Fulani tu,Mungu anataka ufanikiwe katika mambo yako yote, kwahiyo
ndugu unatakiwe ufahamu kuwa ni mapenzi yake Mungu umuombe akufanikishe sana katika mambo yako yote! Ngoja
nikuulize unamambo gani? Muombe akufanikishe katika jambo hilo ulilonalo,sikia si mpango wa Mungu ufanikiwe
katika mambo ya kiroho tu,anasema anataka ufanikiwe pia hata katika afya yako(uchumi), fahamu huwezi leo
ukawa na afya nzuri ikiwa huna uchumi mzuri! Kwa maana hiyo fahamu kuwa ni mapenzi ya Mungu umuombe ili
akufanikishe sana katika uchumi wako au afya yako na ya familia yako.
Sikia maombi haya ya mtu mmoja aitwaye Yabesi,jinsi alivyo muomba Mungu na
Mungu akampa alichokiomba kwani aliomba maombi hayo sawasawa na mapenzi ya Mungu. Ebu
sikia “ Naye Yabesi alikuwa
mwenye heshima kuliko nduguze;na mamaye akamwita jina lake Yabesi,akisema,ni kwa sababu nalimzaa kwa
huzuni,huyo Yabesiakamlingana Mungu wa Israeli akisema,lau kama kwamba ungenibarikia kwelikweli,na
kunizidishia hozi yangu na mkono wako ungekuwa pamoja nami.nawe ungenilinda na maovu,ili usiwe kwa huzuni
yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba”(1NYA 4:9-10), Yabesi alimuomba Mungu amfanikishe kwelikweli(kiuchumi),fahamu Mungu alimpa haja ya
moyo wake, sikia ni mapenzi ya Mungu umuombe ufanikiwe wewe na familia yako.pia ni mapenzi ya Mungu uwaombee
wacha Mungu,ili Mungu awape afya na baraka tele, neno la
Mungu linasema hivi “ Hao
makuhani wahudumu wa Bwana na walie kati ya patakatifu na madhabahu,na waseme uwaachilie watu wako,Ee
Bwana,wala usiutoe urithi wako upate aibu,hata mataifa watawale juu yao;kweli waseme kati ya watu,yu wapi
Mungu wao?” (YOELI 2:17)
Neno la Mungu linamwagiza kila kuhani aseme au aombe mbele za Mungu kuwa
Mungu awaondolee aibu watu wa urithi wake,fahamu katika agano jipya Mungu ametufanya watu wote tumwaminio Yesu kuwa
makuhani sikia neno lake lisemavyo“….. Kwakuwa ulichinjwa,ukamnunulia
Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu
wetu; nao wamiliki juu ya nchi” (UFU 5:9-10),Fahamu wewe uliyenunuliwa kwa damu ya Yesu Kristo,Mungu amekufanya wewe kuwa kuhani wake.
Sasa kila kuhani ameagizwa ahakikishe ana simama mbele za Mungu na kumuomba Mungu awaondolee aibu watoto
wake,na moja ya aibu ambayo kuhani wewe unatakiwa umuombe Mungu aiondoe katika jamii ya watu wa muaminio
Bwana Yesu ni umasikini,fahamu ikiwa wewe umokoka na ni masikini asilimia kubwa maisha yako yatakuwa ya aibu!
Huta mtukuza Mungu kwani kila mara utakuwa ni mtu wa madeni na hata watu watakuchoka kwa
kuombaomba msaada,Sikia ndugu ukiwa masikini hata ndugu zako na jamaa wote wanaokuzunguka hawata kusikiliza
na kukuheshimu, hata kama umeokoka,neno la Bwana linasema wazi kuwa hekima ya masikini
haisikilizwi, “Ndipo nilipo
sema,bora hekima kuliko nguvu;walakini hekima ya masikini hudharauliwa,wala maneno yake hayasikilizwi”
(MHUBIRI 9:16), Fahamu hilo ndugu,kuwa ikiwa leo hii unataka
usikilizwe katika jamii ni lazima uhakikishe unamuomba Mungu sana akupatie mafanikio kiuchumi,fahamu
kama kweli leo hii unataka uwaambie watu maneno ya Mungu na wakae na kukusikiliza unatakiwa usiwe
masikini! Ebu jiulize swali hili,ni kwanini watu wengi leo hii hawasikilizi neno la Mungu? Fahamu moja ya
sababu kubwa inayosababisha watu wasisikie neno la Mungu ni umasikini uliowakalia watu wengi waliokoka! Ebu
angalia mikutano ya injili jinsi inavyoandaliwa,kwa mwaka inaandaliwa mala moja,kisa ni kwa sababu ya
umasikini! Ukiuliza ni kwanini mnaandaa mkutano kwa mwaka mala moja? Jibu utasikia ni kwa sababu hakuna
fedha! Watu wengi waliokoka ni masikini,sasa ili waandae mkutano inabidi wachangishane wee!wadundulize wee
ndipo wauandae uomkutano wa injili, mikutano mingi ya injili ikiisha viongozi huwa ni siri yao tu,kwani mara
nyingi hujikuta katika teso la madeni! Kwani vijipesa vilivyokusanywa havikutosha,na ili mkutano usiahilishwe
viongozi walienda kukopa kwa mtu furani,sas ukiisha mkutano viongozi badara ya kufikilia kuwalea watu
waliozaliwa upya akilizao zina hamia katika suala la kulipa deni
linalowakabili.
Comments