PAPA MPYA APATIKANA NI JORGE MARIO BERGOGLIO



Jorge Mario Bergoglio ambaye ndiye Papa Francis I kutoka Argentina
Moshi mweupe, Papa mpya!

Hatimae Jopo la Makardinali 115 wa Kanisa katoliki wamemchagua Kardinali wa Buenos Aires kutoka Latin Amerika Jorge Mario Bergoglio (76) kuwa kiongozi mpya atakaye chukuwa nafasi ya  Papa Benedict aliyejiuzuli hivi karibuni.Papa Mpya alichaguliwa katika duru ya tano ya upigaji kura uliofanywa na makadinali 115 waliokuwa wakikutana katika kanisa la Sistine Chapel huko Vatican , Roma.
Jorge Mario Bergoglio ambaye ni Muagrgentina tayari amechagua jina la atakalo litumia katikakipindi chake cha Uongozi kuwa atatambulika kama Papa Francis I.
Jopo la Makardinali wamemchagua Cardinali kutoka Latin America Cardinal Jorge Mario Bergoglio, kushika wadhifa mpya wa  Papa katika uchaguzi uliofanyika kwa mara ya tano kwa kura zilizopugwa na Makadinali 115 waliokuwa wakikutana katika kanisa la Sistine Chapel huko Vatican , Roma.
Maelfu ya watu walikuwa wamefurika katika eneo la la St. Peters huko Vatican huku mamilioni wengine wakishuhudia Papa huyo mpya akitangzawa mbele yao.

Comments