UJANA NI MAUA


Ayubu 14:1-2“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke, siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile UA, kisha hukatwa; hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe”

TAFAKARI:
Rafiki! Leo tunatafakari juu ya UA, wote tunajua kuwa UA LIKICHANUA KINACHOFUATA NI KUNYAUKA, na Jambo la kuvutia zaidi ni kuona linavyopendeza na kuvutia, mbali na wanadamu kupenda MAUA, hata wadudu pia utakuta wamejazana.
Maisha ya Mwanadamu ndivyo yalivyo, kama UA linavyonyauka ghafla ndivyo maisha yanavyokatika, kumbuka sisi sote ni marehemu watarajiwa wasiojua muda wa kifo.
Vijana! Mwisho wa UA kuchanua ni kunyauka, wengi huutumia wakati huo vibaya, HAWATULII, Utakuta Binti mzuri eti anajirusha na Libaba ambalo halina Mpango wa kumuoa ili mradi ana Vijisenti – Hao ni WADUDU WAHARIBIFU. Tunaona baadhi ya MAUA yanavyoharibiwa na wadudu waharibifu, yanatobolewa na kuchafuliwa, ndivyo vijana WANAVYOPOTEZEWA DIRA YA MAISHA. Akili zikiwarudia na kutaka Kuolewa au kuoa wanajikuta wamechelewa – UMRI WA KUCHANUA UMEPITA, hata wakitumia MAKE UP, hazisaidii, wadudu wote wamekimbilia maua mengine yanayochanua.
Vijana! Habari za ku “PASS TIME” na vija wenzenu kwa maisha ya Ngono, Ulevi, Muziki n.k. yanawapotezea DIRA ya Maisha, tumeshuhudia wengi wanasukumwa na TAMAA, na  Wengi wanatumika kama VYOMBO vya kukidhi tama za wengine, mwisho wake ni kuachwa kwenye Mataa. MAISHA YOYOTE YA DHAMBI NI TANZI YA UHARIBIFU.
VIJANA WENGI WANAJUTIA KWA YALIYOPITA NA WENGINE NDIO WAMEZAMA.
SULUHISHO NI KUMTEGEMEA MUNGU – KWAKE YOTE YANAWEZEKANA
NAWATAKIA SIKU NJEMA NA WEEK END NJEMA YENYE BARAKA TELE

Comments