Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps

“Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu ;ila si hekima ya
dunia hii,wala ya hao wanaoitawala dunia hii,wanaobatilika;bali twanena
hekima ya Mungu katika siri,ile hekima iliyofichwa ,ambayo Mungu
aliazimu tangu milele,kwa utukufu wetu;ambayo waitawalayo dunia hii
hawaijui hata mmoja;maana kama wangaliijua[Yesu] ,wasingalimsulubisha
Bwana wa utukufu ;” 1wakorintho 2:6-8
Hekima hii ya MUNGU ni
YESU,ambapo kwa wafalme na watawala wa dunia hii wamefichwa,ndiyo maana
hawamwamini,hawajampokea kama Bwana na mwokozi wao,wamemkataa katika
fahamu zao,na wala hawaamini kuokoka.Yesu ni hekima ya MUNGU,unapo
mpokea ndipo unapopata ufunuo wote wa kimungu ndani yako na ndipo
unapopata kumjua Mungu baba na urithi katika ufalme wa milele,na bila
Yesu hakuna uzima wa milele,hakuna kuingia mbinguni.
Hekima hii ya
MUNGU ndiyo inayofanya kazi ndani yetu tumwaminio na ni hekima ambayo
ulimwengu huu hauwezi kushindana nayo maana imepita fahamu za
wanadamu,Mungu anatukuzwa katika hiyo na matumaini ya waadamu
yanarejeshwa upya ndani yake. “Enenda pamoja na wenye hekima nawe
utakuwa na hekima;Bali rafiki wa wapumbavu ataumia”Mithali 13:20. Hekima sahihi iko kwa YESU KRISTO hivyo ni heri kila mmoja wetu akamchagua BWANA YESU ili hekima ya kimungu ifanye kazi ndani yake. MUNGU BABA wa mbinguni akubariki sana
- Get link
- X
- Other Apps
Comments