Posted by
Peter Mabula
- Get link
 - X
 - Other Apps
 

 
 BWANA YESU APEWE SIFA…
 Wapendwa wa Mungu nami niwaletee maneno ya MUNGU.
 Kwenye maisha ya kawaida ya mtu yeyote kitu ambacho humfanya ajisikie 
furaha sana ni uhuru wa mawazo na matendo, kwa hayo huamini nafsi yake 
imeridhika kwayo.
 Katika uhuru huo mtu anakuwa anawaza pia hasa 
matendo ambayo ndiyo huonekana kwa wanadamu huyatenda pia. Mtu huyo 
huyatenda na huwa haijalishi kama yanawaudhi wengine au hapana lakini 
ili mradi huufurahisha moyo wake basi huyatenda tu. Uhuru huu mtu huwa 
nao tu kwa sababu hakuna jambo au mtu yeyote ambaye anaweza kuingilia au
 kuupunguza uhuru huo. Cha ajabu ni kwamba upo wakati uhuru kwa mtu 
hubadilika, hupungua na kuanza kufanya kwa misingi ya mamlaka nje ya 
kichwa au mawazo yake. Ni wakati huu ambapo mtu hupata shida kwa sababu 
amebadilishiwa utaratibu wake wa kuishi iwe kwa kutaka au kulazimishwa 
lakini baada ya muda huwa ni maisha yake ya kawaida kwani huyazoea.
 
 Fikiria mtu anapokuwa chini ya mamlaka fulani hususani za utumishi (kuwa
 chini ya bosi). Yako mambo ambayo kwa mazoea yako ulikuwa unayatenda 
kwani ulikuwa ni uhuru wako lakini kwa sababu sasa uko chini ya mamlaka 
ya mtu huyaachakuyatenda kwani mamlaka hayo haiyapendi au ina utaratibu 
wake. Fikiria ulikuwa umezoea kuvaa viatu vya wazi/sandles na pensi, 
baadhi ya misuko kwa wadada, nguo fupi na zinazoonesha maungo ya ndani 
lakini ukifika kwa bosi anakwambia style hiyo hatuitaki vaa hivi na 
uonekane hivi la sivyo huna kazi. Kwasababu ya kuhitaji kazi mtu huyo 
hubadilika na kufuata utaratibu huo wa kazini na kuacha maisha yake ya 
kawaida, 
 
 Pia yamkini kwa sababu mtu huyo alizoea kuamka saa 
tatu pindi hana kazi baada ya kupata kazi hulazimika kuamka  saa 12 au 
saa 1 ili kuwahi kazini aendane na masharti na taratibu za kazi.(hiyo ni
 baadhi ya mifano tu) katika maisha ya kimwili ya kila siku.
 
 
Vivyo hivyo maisha ya kimungu yana sheria taratibu, na masharti yake 
pia. Unapoanza maisha ya kimungu ni lazima yako matendo na mwenendo wa 
fikra zako kubadilika pia. Mpaka unamtafuta mungu maana yake umetambua 
dhambi za maisha yako ndio maana ukazikimbia, mmhh haiishii hapo, 
inapasa kukimbiambali zaidi ktk na kuyaacha mazoea yako ili kishi maisha
 yenye msingi wa kimungu na kumpendeza mungu na  watu pia. Tunapoamua 
kumtumikia bosi wetu mungu ambapo malipo yetu ni kufika mbinguni ni 
lazima tuache baadhi ya mazoea yetu mabaya. (flp 1:27)
 
 Soma filp 3;1-10
 Nizingatie filp 3:7  lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya kristo.
 Hapa Paulo alikuwa akiwahadithia wafilipi habari za nyakati zake kabla 
ya kumpokea kristo kwamba aliyatenda kwani yaliufurahisha moyo wake, lkn
 baada ya kumpokea kristo sasa anachukua gharama ya kuyaacha. 
 Katika mengi unayoyajua  kwa uzoefu wako wa maisha mimi nitazungumzia jambo moja tu
 
 MAVAZI.
 Suala la mavazi sijui kama watu huwa wanalizingatia hussani wale wenye 
jukumu la kuhubiri au kufundisha neon la Mungu. Elewa vizuri dhana hii, 
“Mungu anaangalia moyo wako lakini wanadamu wanaangalia matendo yako, 
wakiyaona mazuri huamini lakini wakiyaona mabaya hawana haja na Mungu 
wako”
 
 Angalia habari hizi, watu Fulani wakajisemea; aaahh kwa jinsi alivyo huyu hata mimi leo nikiokoka siwezi kuvaa hivi.
 
 Mahala Fulani watu wakishuhudiwa ibada ya nyumba kwa nyumba walisema; 
aaa aaahhhh azungumze huyu lkn huyu sisi hatutaki atushuhudie kwani naye
 anahitaji kushuhudiwa (mavazi yake yalikuwa mabaya)
 
 Mhubiri 
akihubiri na hereni zake ndefu sana na madoido mengi, mshirika  mmoja 
akaulizwa umeelewa somo la leo? Alichosema aah hivi zile herein zinauzwa
 shilingi ngapi? Na zinapatikana wapi kwani makubwa!!!
 
 Mhubiri 
mmoja akiwa madhabahuni akidhani watu walikuwa wanasikiliza neon kwa 
makini kumbe watu walikuwa wanatafakari hivi kile kikofia alichovaa 
kinauzwa shilingi ngapi kwani kina mbwembwe kwelikweli.
 (hiyo ni baadhi ya matukio niliyowahi kupata kuyasikia au kuyaona kwenye huduma mbalimbali)
 
 Haijalishi kama wewe ni muhubiri, mwalimu au muumini wa kawaida je 
unajiwekaje  kimavazi mpaka wengine waseme hakika huyu amebadilika.
 
 MWISHO NIMALIZIE,
 TAFAKARI, JIPIME MWENYEWE KAMA MTU WA MUNGU NA MAISHA YAKO YAWAFUNDISHE WENGINE.
- Get link
 - X
 - Other Apps
 


Comments